Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kama kuna kosa kubwa mtalifanya ni kuviweka vyuo vya walimu chini ya NACTE. Kwanza jambo hili litashusha nidhamu za walimu tarajali, jambo ambalo ni hatari kwa mustakabli wa elimu nchini. Pia jambo hili litafanya sekta hii muhimu ya utoaji wa mafunzo kwa walimu kusimamiwa na watu ambao hawana ujuzi wala uzoefu katika masuala ya mafunzo ya walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni suala la kudharau mafunzo kwa vitendo kwa walimu tarajali. Kazi ya walimu inadharaulika, wanafunzi walimu mnawapa shilingi 2,000 wanapokwenda BTP, ili wakanunue nini? Sekta ya elimu ni sekta muhimu na lazima Serikali ioneshe seriousness katika kuratibu, kusimamia na kuongoza sekta hii.
Mheshimiwa Waziri, jambo lingine ni Idara ya Ukaguzi. Hivi kwa nini Idara hii haiwezeshwi kipesa iweze kufanya kazi ya kusimamia utoaji wa elimu na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa. Tafadhali sana wezesheni Idara ya Ukaguzi ili ifanye kazi yake ipasavyo. Jambo hili ni muhimu sana, ahsante