Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kwanza kumpongeza sana Waziri wa Fedha na Naibu wake kwa kazi nzuri waliyoifanya kuwasilisha mpango huu wa maendeleo wa miaka mitano, mpango wa tatu. Naomba nijielekeze katika njia gani ambazo nazipendekeza zinaweza zikaongeza mapato katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Nchi ya India kabla ya mwaka 2005 ilikumbana na changamoto ya wananchi wake kuhitaji kuwa na uraia pacha. Tatizo hili lilikuwa kubwa, lakini Serikali ya India ilikaa chini na kufikiria jinsi gani inaweza ikatatua tatizo hili na wananchi wake wakaendelea na maisha yao hivyo, wakaanzisha, wakawapatia kitu kinachoitwa Over Seas Citizen of India Card. Kadi ile iliwawezesha raia wote ambao ni wahindi by original kuweza kuingia India kwa wakati wowote na muda wowote wanaotaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kufanya hivi waliweza kutatua matatizo matatu. Kwanza lile takwa la wananchi wa India kuwa na uraia pacha liliondoka kwasababu, lengo lao lilikuwa kuingia India na kushiriki katika shughuli za kiuchumi. Kwa hiyo, kwa kuwapatia hizi kadi za Over Seas Citizen of India raia wa India wanaoishi nchi mbalimbali waliweza kuja India bila matatizo yoyote na ku-maintain uraia wao. Kwa hiyo, Watanzania wengi wenye asili ya India ambao wako hapa Tanzania wanazo kadi hizi Over Seas Citizen of India. Hata raia wanaoishi Uingereza, Marekani, n.k.

Mheshimiwa Naibu Spika, na wahindi hawa wanapofika India wanapata privilege zifuatazo, kwanza wanaweza kushiriki katuika shughuli za uchumi ndani ya nchi ile. Kwa hiyo, wahindi wameweza kuwekeza, wameweza kupeleka uchumi, kupeleka mitaji India kwasababu sasahivi wamekuwa hawana tena pingamizi la kwenda India. Muda wowote na wakati wowote wanaweza kwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili. Raia wa India na huyo ambaye haishi India wana haki sawa. Haki ambazo zinamuwezesha raia wa India, mfano haki za kushiriki katika shughuli za maendeleo, raia wa India na huyo ambaye anakaa nje ya India anafanya wakati mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini waliweka utaratibu wa kuwazuia hawa wenye Over Seas Citizen of India wasifanye mambo yafuatayo; kwanza waliwaambia tunawapatia hizi kadi, hizi sio passport kwa hiyo, wewe sio raia wa India ila tunakutambua kama muhindi mwenzetu. Kwa hiyo, hutaweza kupiga kura katika nchi yetu, hutaweza kushiriki katika shughuli za kiserikali au hautakuwa kiongozi wa kuchaguliwa. Na hautakuwa ukafanya shughuli za kununua ardhi ndani ya India, lakini unaweza ukawekeza katika nchi yetu. Kwa hiyo, India waliweza kuvutia mitaji mingi sana ndani ya nchi yao ndani ya utaratibu huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilikuwa naomba tujaribu kuiga utaratibu wa India. Tunao Watanzania wengi ambao wako nje ya nchi yetu wana uwezo na wana pesa za kuja kuwekeza ndani ya nchi yetu. Lakini hawataki kuukana uraia wa hizo nchi. Na sisi hatuna utaratibu wa raia pacha, tuwapatie kadi tuwaite Over Seas Citizen of Tanzania. Wakija hapa waje kwenye shughuli za kiuchumi tu, hata ruhusiwa kupiga kura, hata ruhusiwa kuchaguliwa, hata ruhusiwa kununua ardhi, lakini ataweza kuwekeza ndani ya nchi yetu. Nina imani kabisa tutakuwa na uwezo wa kuwavutia wahindi wengi, waingereza wengi, wajerumani wengi, ambao walikuwa raia wa nchi hii, wamarekani wengi wakaja na wakawekeza ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu huu umewezesha nchi ya India kuinua sana uchumi na vijana wengi wameajiriwa, lakini pamoja na hivyo India waliweza kuvutia teknolojia kwasababu, nchi mbalimbali zilikwenda na wakaweza kuleta teknolojia mbalimbali. Kwa hiyo, halikadhalika kwa nchi yetu nina uhakika kabisa tutakapotumia utaratibu huu tutapata knowledge za mataifa mengine ndani ya nchi yetu; madaktari watakuja kwetu, ma- engineer watakuja kwetu na wataalamu wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa pili ambao naupendekeza, sisi nchi yetu ya Tanzania, natoka Wilaya ya Nanyumbu. Wilaya yangu inapakana na nchi ya Msumbiji. Mheshimiwa Mtenga alipokuwa anaelezea daraja la Mtamba Swala liko ndani ya wilaya yangu. Amezungumzia kutokuwa umuhimu wa lile daraja katika maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lile daraja lilijengwa purposely kwa ajili ya kuinua uchumi wa watu wa Kusini, tatizo ambalo lipo upende wa pili wa lile daraja miundombinu ni mibovu. Naomba sana Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje watumie nafasi hii waishauri Serikali ya Msumbiji waweze kuimarisha barabara kutoka Mtamba Swala kwenda mkoa unaofuata ambao hauko kilometa nyingi. Sasa hivi ninavyozungumza mbao zote zinazokuja Dar-es-Salaam, mbao ngumu, zinatoka Msumbiji zinapitia Daraja la Mtamba Swala. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunanufaika sana kuwepo kwa lile daraja. Vijana wa Mtwara, vijana wa wilaya yangu wanafanya biashara na mkoa wa jirani wanapeleka mahindi, wanapeleka mchele, wanapeleka samaki, wanapeleka dagaa. Nina imani kabisa endapo miundombinu itaboreshwa upande wa pili wa lile daraja hali ya kiuchumi wa wananchi wetu itaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu naomba sana ndugu zangu viongozi wetu Mawaziri, hawa wawekezaji tulionao tuendelee kuwa-maintain. Kuna tabia ambayo sasa hivi imejengeka, hawa wawekezaji tulionao tunawakatisha tamaa. Tunao wawekezaji wanaofanya biashara ya kuingiza faida, lakini pia tunao wawekezaji wanaotoa huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule kwetu tuna Hospitali ya Ndanda tuna Hospitali ya Nanyangao na majirani zetu pale Tunduru wana Hospitali ya Mbesa. Kuna watu wa foreigners wanaoendesha zile hospitali wanapata tabu sana ku-renew vibali vyao. Unashangaa mtu anamkatalia daktari ku-renew mkataba wake; unajiuliza huyu anatafuta nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi nawaomba; hawa watu wanao-renew mikataba ni watalam, na kitendo cha hawa kuwepo wanaongeza utaalam kwa local staffs wetu. Leo unamwambia muda wako umekwisha ondoka aje mwingine. Uapomfukuza yule mtaalam maana yake unaiua ile Hospitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi ningeomba, Mheshimiwa Waziri, mama yangu, shemeji yangu, Mama Jenista; hawa wataalam wetu wanatuangusha. Haiwezekani leo unamnyima daktari kuongeza mkataba. Daktari anakataa kuongezewa mkataba wanatutakia mema watu hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, unapomkatalia daktari hata wagonjwa hawaendi tena. Kuna watu wanakuja kwa sababu Doctor Yahya yupo pale. Leo unamwambia rudi kwenu halafu ile hospitali unamuachia nani? Ningeomba sana Mheshimiwa Waziri aliangalie hili, wataalam wetu wanakotupeleka siko, waangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini linguine, kuna baadhi ya missions, mashirika ya dini wanatoa huduma za uchimbaji wa visima. Kuna mashirika kule kwetu wanachimba visima kwenye shule bure. Yule m-mission mkataba umekwisha amekataliwa kuongezwa, anachimbia shule kumi, kumi na tano bure, unamkatalia unapata nini? Amekuja na pesa zake, amekuja na utaalam wake amekuja na vyombo vyake unamwambia muda wako umekwisha rudi kwenu, maana yake wewe hutaki wananchi wetu wapate maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana wataam hawa waangaliwe; hasa hawa ambao wanatoa huduma. Mashirika yetu ya dini wana watu wa namna ile wanaanza kufukuzwa eti kwasababu muda umekwisha, jambo hili kwakweli halikubaliki katika uchumi wetu…

NAIBU SPIKA: Ahsante sana, muda umeisha, …

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naomba kuunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)