Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZUBEDA H. SAKURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha mchango wangu kuhusu hoja ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la siasa vyuoni limeendelea kuwa mwiba kwa baadhi ya vyuo vikuu nchini. Menejimenti za vyuo zimekuwa zikiingilia Serikali za wanafunzi, lakini pia kuwanyima haki wanafunzi wanaoshiriki katika nafasi za uongozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro mkubwa wa uongozi baina ya menejimenti ya Chuo cha Dodoma na Serikali iliyoondolewa madarakani kwa shinikizo la menejimenti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu si tu umechochewa na menejimenti ya chuo lakini pia umelenga kuwanyima wanafunzi waliochaguliwa kihalali na wanafunzi kuongoza Serikali ya wanafunzi pamoja na kuwasimamisha chuo kinyume na hukumu ya mahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, binti Rose Maruchu mwanafunzi wa mwaka wa tatu alichaguliwa na wanafunzi wa UDOM alisimamishwa chuo miezi miwili tu kabla ya kumaliza chuo lakini pia wakati kesi ikiwa mahakamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi ilifunguliwa kabla ya tarehe 11/4/2016 lakini cha kushangaza kesi ikiwa mahakamani Bi, Maruchu alipokea barua ya zuio la kuendelea kuwa kiongozi na menejimenti ikaunda Serikali ya mpito kinyume cha sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na hata wakati kesi ya zuio inaendelea kusikilizwa mahakamani, wakili wa UDOM alitoa barua kuwa Maruchu amesimamishwa chuo tangu tarehe 11/4/2016. Waziri si tu kuwa menejimenti ilidharau mahakama lakini pia imelenga kumkomoa Rose ambaye alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa UDOSO kihalali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote hukumu iliyotolewa dhidi ya Chuo cha Dodoma ilimpa ushindi Bi. Rose Maruchu na kuamuru chuo kimruhusu Rose kuendelea na masomo pamoja na majukumu yake, Rose hajarudishwa chuo huku akiwa amebakiza miezi miwili tu kumaliza chuo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haki iko wapi Mheshimiwa Waziri? Tunawapaje motisha wasichana waliopo vyuoni kugombea nafasi za uongozi wakati wakiwekewa mazuio na vikwazo vya maksudi? Menejimenti ya UDOM inapata wapi jeuri ya kukaidi amri ya mahakama? Kukaa kimya kwa Serikali ndiko kunakoinua malalamiko kuwa inashiriki kushinikiza menejimenti za vyuo kukandamiza na kuingilia Serikali za vyuo hasa zinazoongozwa na wanafunzi wenye mitazamo kinzani na menejimenti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri naomba usimamie haki ya Rose Maruchu, kama Waziri mwenye dhamana lakini zaidi kama mama. Imagine unaona ndoto za mwanao zinazimwa kwa kutetea maslahi ya wenzake? Ni uchungu gani mzazi anaobeba kuona ada na jitihada zake kwa binti yake zinazimwa miezi miwili kabla ya kuhitimu miaka mitatu, cha uchungu wa gharama za kusomesha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwako si tu kuitaka menejimenti kumrudisha Rose kama kiongozi, bali kutaka menejimenti ya UDOM kumrudisha chuo na kumwachia binti huyu haki zake kama mwanafunzi ikiwemo kufanya majaribio (tests), assignments zote na mitihani ili ahitimishe miaka yake mitatu. Nawasilisha.