Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwamba, Mheshimiwa Shangazi ambaye atakuwa wa pili baada ya mimi amenipatia dakika tano zake kwa sababu, anadhani naweza kuwapa mambo mengi mazuri. Halafu… (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Profesa sasa changamoto ni kwamba, kipindi hiki unachangia tu dakika kumi. Kwa hiyo, zile za kwake inabidi labda umgawie mtu ambaye hayupo kabisa na achangie hizo tano peke yake kwa hiyo, muda wako utaanza sasahivi wa hizo dakika kumi.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, haya. Ombi lingine ni kwamba, dakika kumi nikijadili tu la Liganga/Mchuchuma hazinitoshi kwa hiyo, kama Bunge mnataka kusikiliza ya Liganga/Mchuchuma mniombee dakika tano badaye. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Waheshimiwa Wabunge naomba nichangie na kutoa ushauri huu. Ni kwamba, mpango tulionao makusudio makubwa kwanza ni suala la ukuaji wa uchumi uende zaidi ya asilimia 8, mbili ajira, tatu ustawi wa jamii na maendeleo, yote yameelezwa humo, ila mimi ninaboresha na kuongezea.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huu unahitaji kuhudumia watu, sasa hivi tuko watu karibu milioni 61 mwaka 2025 tutakuwa takribani watu milioni 70 kwa hiyo, huu mpango lazima uwahudumie hawa watu. GDP per capita yetu iliyotuingiza kwenye nchi za kipato cha chini (lower middle income) ni dola 1080. Maoteo ni kwamba, tukifika mwaka 2025 GDP per capita yetu itakuwa ni dola 1400. Hizo bado ni fedha kidogo ndugu zangu, inamaanisha mwaka 2025 kipato cha Mtanzania kila mwezi kitakuwa dola 117.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nikaja na hesabu angalao tufike dola 150 maana yake kwamba, GDP per capita yetu itakuwa dola 1800 tukifika mwaka 2025 ambayo wenzetu wa Kenya tayari wanayo. Sasa kinachohitajika hapa na ugomvi mwingi wa kodi, task force, nionavyo ni kwamba, hata kodi zetu tufanyeje tatizo bidhaa ni hizohizo na walipa kodi ni haohao. Na huu uchumi tukitaka ukue kwa zaidi ya asilimia 8 ni lazima tutafute bidhaa mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwenye bidhaa mpya naomba mnisikilize kwa makini. Tumefanya utafiti kutoka miaka mingi karibu miongo mitatu, tumeangalia nchi zilizokuwa na mafanikio makubwa ambazo uchumi ulikuwa kwa zaidi ya asilimia 10 kwa mwaka tumegundua kwamba, uwekezaji wao mkubwa namba moja ulikuwa kwenye utafiti. Ninaomba huu mpango tulionao uweke mkazo kwenye utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Jirani yangu hapa alivyosema tumeshakubaliana nchi za kiafrika 1% of the GDP iende kwenye research and development. Kwa hiyo, mpango huu tunaomba utoe fedha nyingi kwa ajili ya utafiti, lakini kwa hali ya sasa tuliyonayo, COSTECH tuliyonayo haiwezi kufanya hiyo kazi kwasababu muundo wake ni kama idara ndani ya Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimefanya kazi na ma- funding agencies mengi sana duniani, lakjini hayana muundo kama wa COSTECH. Bajeti ya COSTECH ni ndogo, ukichukua 1% ya 50 billion US Dollars ya mwaka, sasa hivi nadhani GDP yetu karibu iko kwenye around 60 billion uchukue 1% hiyo, mnajua hesabu, uipatie COSTECH, COSTECH haiwezi ku- manage hizo fedha kwa ajili ya muundo na haiwezi kufanya utafiti. Kwa hiyo, cha kwanza kabisa kwenye mpango wetu turudi kwenye utafiti. Kilimo ni utafiti, maji ni utafiti, ujenzi ni utafiti, hatuwei kulikwepa hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nije kwenye bidhaa mpya ambazo zitaleta 8% au 10%. Cha kwanza kabisa nadhani msemaji mmoja jana alisema kwenye sekta ya madini lazima tubadilike ndio maana nilisema ya Liganga siwezi kuongelea mambo ya iron. Dunia inabadilika kuna madini yanatakiwa sasa hivi duniani kwa hiyo, kwenye ripoti zetu kuwa tunaongelea kila siku dhahabu, tanzanite, ni kama tunapitwa na wakati kidogo lazima tulete madini mapya ambayo ndio yatafanya uchumi ukue kwa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, na haya madini mapya yanahitajika kwenye fourth industrial revolution, mabadiliko, hata kama sisi hatuhusiki tutachukuliwa tu kama ma- passenger, passive passengers in the fourth industrial revolution ndio sisi, lakini tunayo hayo madini. Kwa hiyo, mpango wetu badala ya uongelee vizuri dhahabu, ongelea tanzanite, lakini hiyo ni monotony, madini yanayohitajika sasa hivi naomba niyasome; lithium kwa ajili ya mabetri, cobalt, nickel, platinum, chrome, manganese, copper. Hayo yote nchini yapo, lakini hatuna mgodi hata mmoja, badala ya kila siku kufukuzana na dhahabu tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na niwasaidie tena. Dhahabu sasahivi imepanda bei kutoka kwenye dola 1700 mpaka dola 2000 kwa ounce, lakini nyuma ilikuwa chini yad ola 1400. Kwa hiyo, hesabu zetu mtu akisema sekta inafanya vizuri anasahau kwamba, bei kule imepanda ndio maana tumepata fedha nyingi, lakini haijamaanisha sekta inafanya vizuri migodi ni ileile. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna madini ambayo ni muhimu sana. Wote wenye iphone hapa, kama kuna mtu ana iphone, madini yaliyomo humo rea earth elements ni manane, specific eight. Madini haya yako 17 na haya ndio madini yanahitajika sasa hivi duniani zaidi kuliko chuma kwa hiyo, tuwekeze huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado dakika tano?

Mheshimiwa Naibu Spika, bidhaa nyingine ambayo inabidi kutuletea hizo fedha ni nishati. Nishati tutumie nyumbani, nishati tuiuze. Tumeshajenga transmission lines kwenda Kenya, transmission lines kwenda Zambia yaani kwenye soko la SADC na kwenye soko la East African community kwa hiyo, umeme tulionao ni mdogo. Kila siku nasikia mnaimba hydro, ukweli ni kwamba, anayejua mambo ya umeme hydro kukupatia faida umewekeza hela nyingi unahitaji miaka u-re-crop ile faida ndio umeme uwe wa bei ya chini wa maji. Sio tu kwamba, leo nikimaliza bwawa hapohapo bei ni ndogo, labda kama hutaki kurudisha fedha zako.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndugu zangu tulitengeneza energy mix. Na projections ni kwamba, Bara la Afrika litakuwa na ukame tutakuwa tunapoteza kati ya GDP 1% to 2% zitapotea. Je, mabwawa yetu yakikumbwa na ukame nini kitatokea?

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana tunataka energy mix, hydro, natural gas, coal. Tunaenda renewables, wind, solar, geothermal, biomass, tides and waves. Umeme huu tunahitaji na tulishapanga zaidi ya megawatts 10,000 ndio target. Kwa hiyo, huu mpango lazima ujielekeze kuzalisha zaidi ya megawatt elfu kumi kwa miaka mitano ijayo; hii mingine yote haitoshi, tuzalishe tuuze, bidhaa hiyo nyingine mpya hiyo. Na tukipata bidhaa hizi tukauza tukapata fedha nyingi hata tutapunguza hizi kodi tunazopigana kila siku kwa sababu ni bidhaa zilezile ni watu walewale, sasa tulete bidhaa mpya.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuzalishe tuuze bidhaa bidhaa hiyo nyingine mpya hiyo, na tukipata bidhaa hizi tukauza tukapata fedha nyingi hata tutapunguza hizi kodi tunazopigana kila siku kwasababu ni bidhaa zile zile ni watu wale wale sasa tulete bidhaa mpya. Bidhaa mpya nyingine ni ya gesi tumesimama LNG yetu uwekezaji ndio ungelikuwa mkubwa kwa historia ya nchi hii, ni thirty billion, sisi ni thirty billion. Msumbiji vita yao huku Cabo Delgado ikitulia uwekezaji wao unatuzidi, wao wako kwenye sixty billion tumechelewa kwasababu hatujafanya maamuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo LNG ndugu zangu, natural gas ni bidhaa mpya ambayo nchi kama Qatar ina GDP per capital ya zaidi ya sixty thousand USD per person per annum, na sisi tulipokuwa tumepanga kufika Dola elfu 3,000 per Person per annum tutafikia kwa kutumia uchumi wa gesi. Kwa hiyo huo mpango kama tunataka kufanikiwa mimi sioni kwanini tusirudi kwenye mipango yetu ya uchumi wa gesi, bila hivyo ndugu zangu hatuwezi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine bidhaa mpya nimekuja nayo ambayo tunabidi kuifanyia kazi ni gesi ya helium ambayo inatakiwa duniani. Wote huwa mnaenda kwenye MRI Scanner. Unajua scanners zote za dunia nzima zinatumia helium, simu zote tulizonazo kuna helium. Kwa hiyo nimechukua bidhaa ambazo zinatumika duniani kwa watu wengi ndio bidhaa mpya. Kwa hiyo ndugu zangu na hiyo nayo tuiendeleze.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ya mwisho hii niliongea wakati ule kwamba agriculture yetu ichukue mazao manne ambayo yanatumiwa zaidi ya nusu ya wakazi wa dunia hii. Sasa hivi tupo watu bilioni 7.8, tukifika mwaka 2025 tutakuwa takriban kwenye bilion tisa. Hawa watu wote hayo madini niliyokwambia wana simu, wana laptop, wanaenda kwenye electric cars na kwa hiyo watatumia hivyo vitu; ndiyo bidhaa mpya ya kufanya uchumi wetu ukue.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mwisho ni kilimo kwa kuwa kinaajiri wengi. tulime na tufuate ile Maputo Declaration. Mwaka 2006 nchi za Kiafrika zilipokuwa Maputo zilikubaliana kwamba angalau asilimia 10 ya pato la Serikali iende kwenye bajeti za kilimo, lakini sisi bado tuko kwenye asilimia tatu hadi nne. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kilimo, hiyo irrigation mliyokuwa mnaongea jana itafanyiwa kazi, utafiti utafanyiwa kazi, tuzalishe haya manne; yaani Mahindi, Mpunga, Ngano na Mihogo, hayo ndiyo mazao ambayo zaidi ya 50 percent of the world population wanafanya consumption.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hili la Liganga; muda umekwisha au bado upo?

MBUNGE FULANI: Bado.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Haya, kumbe nimeenda kasi, kumbe nimeenda vizuri. Sasa ndugu zangu Liganga ni hivi …!!!

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Profesa naambiwa kengele ya pili imegonga.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, bado wanataka ya Liganga kidogo Mama Mheshimiwa.

NAIBU SPIKA: Dakika mbili malizia.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, haya dakika mbili, jamani ya Liganga Historia yake ni kwamba utafiti ulianza tangu miaka ya 70. Miaka ya 80 Profesa Marehemu Nicas Mahinda alifanya Ph.D yake kuhusu Liganga. Wakati wa miaka ya 80 watu kwenye hiyo Liganga walikuwa wanataka chuma peke yake, lakini ndani yake kuna titanium na vanadium. Kwa hiyo discussion ilikuwa tutatoaje?

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana huu mradi nadhani sijui kama tulifanya vizuri kumpatia mtu mmoja miradi yote miwili; sidhani. Lakini wakati ule mawazo ilikuwa lazima tumpe anahitaji umeme mwingi ili atenganishe Iron kutoka kwenye Titanium na vanadium, zile zilionekana ni madini yasiyotakiwa wakati ule; lakini tekinolojia ya sasa tunayahitaji mno, titanium na vanadium tunayahitaji sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi pendekezo langu kwenye huu mradi, huyu tumempatia vyote, na Makaa na Mawe ya Mchukuma yalikuwa yazalishe six hundred megawatts, megawatts 250 azitumie kwenye mambo ya plant yake megawatt 350 apeleke kwenye national grid. Sasa sijui, kosa tulilolifanya yeye kama huku haweze kuzalisha umeme inamaanisha hata huku kwenye chuma hata zalisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi nilikuwa nashauri, NDC haina uwezo wa kuendesha huu mradi kwasababu imekaa nao tangu miaka ya 80, lazima tufanya maamuzi huu mradi upelekwe kwa watu wenye ujuzi, wanaoyajua hayo madini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile NDC wamepewa soda ash kule Engaluka, hawawezi na wenyewe watolewe hii miradi hao NDC ipelekwe chini ya Ofisi ya Rais kwamba kila Waziri pale anaitwa au Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini NDC ikibaki viwanda na Biashara kama imeshindwa kuendeleza huu mradi kwa miaka zaidi ya 40 sidhani kwamba wana uwezo huo, na hawana uwezo huo ukweli ndio huo. Sasa ambacho mimi nilikuwa nimemuomba yule mwekezaji ni wa kutoka China; na mimi napokea ripoti zote za mambo ya madini takriban ya dunia nzima. Nikampendekezea kwamba wewe mimi nadhani mtaji wako na teknolojia yako inaweza ikakufanya huu mradi usiutekeleze. Nnikamuomba balozi wa wakati huu tukakaa, mimi na balozi na yule. Nikasema kwakuwa huyu ameshawekeza hela zake sisi tutafute kampuni nyingine kubwa ya China ishirikiane nae,

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ndugu zangu China ni miongoni mwa wazalishaji wa chuma wakubwa na watumiaji wa chuma wakubwa yaani na wao wataenda kwa speed yao. Kwa mfano mpaka Ijumaa iliyopita walikuwa na tani zaidi ya milioni 100 kwenye bandari zao 43; wanaita stock pile, sasa kama mtu ana stock pile ya tani zaidi ya 110 kwenye Bandari 45 za China je, atakuwa na moto wa kuja kuchimba chuma yetu? (Makofi)