Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ESTHER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango wangu kwa kuzungumza ndani ya Bunge bado nimeona ni vyema niweze kuwasilisha mchango wangu wa maandishi kwa maslahi mapana katika kuboresha elimu ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliposema kuna haja ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu kushuka vyuoni kote nchini Tanzania ili kujionea changamoto za walimu pamoja wanafunzi hapa nilimaanisha yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo michango ya wakuu wa vyuo vikuu kutumia madaraka yao vibaya ilhali universities charter ikiwa inatoa kinga ya wakuu hawa kutoingiliwa katika utendaji wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo wakuu wa vyuo wamekuwa wakimiliki magari mawili hata matatu wakitengea mafuta lita 500 mpaka 1200 kwa mwezi kwa ajili ya shughuli za kiutendaji na shughuli za familia zao. Hii ni kukosa utii ku-abuse nafasi yao na usaliti wa misimamo ya Mheshimiwa Rais katika dhana nzima ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo wakuu wa vyuo vikuu wanaolindwa na security, mathalani auxiliary police 12 hadi 18 kwa siku moja tu na wakati huo wanafunzi wamekuwa na matukio ya kuumizwa na wezi na vibaka kwa kukosa ulinzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoangalia suala la misuse of public resources kwa upande wa wakuu wa vyuo vikuu ninapata feelings kwamba at sometimes we need to break the rules for example university charter inatumika kama sehemu ya kuiibia Serikali kwani pamoja na kutumia nafasi zao kwa maslahi yao binafsi lakini pia tumeona Serikali inavyoibiwa kwa miradi inayoendeshwa na baadhi ya vyuo ambapo Wizara husika inafika hata kukosa taarifa rasmi za kiasi gani chuo husika kinazalisha kwa mwezi kupitia miradi ya ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo masuala ambayo yana maslahi mapana kwa taifa hili hususan katika dhana nzima ya utumishi uliotukuka. Katika masuala ya TCU ambayo mengi yametugusa mimi binafsi napenda nikiri kuwa nimeridhia kabisa kwa suala la kutodahili wanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi 489 wameonekana wamekosa sifa na vigezo katika kudahiliwa kwenye vyuo vikuu, lakini hii haimaanishi tunaitoa TCU katika kujibu hoja zetu za msingi.
Mathalani kwa kuwa TCU ndiyo inayosimamia ubora wa elimu (Higher learning institutions) na ndiyo inayoweka vigezo vya udahili, ndiyo inayokagua na kupitisha mitaala na ndiyo inayokagua ubora endelevu wa taasisi za umma nchini Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mathalani Chuo Kikuu cha St. Joseph, ni nini sasa hatma ya vijana hawa 489 ambao wameonekana kukosa sifa na vigezo? Je, watawapeleka shambani wakalime ili ndoto ya ajira kwa vijana hawa ikapate kutimia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninahoja maswali haya kwani kimsingi Serikali imepoteza kiasi cha fedha kupitia udhamini wa mikopo iliyowahi kutoka huko nyuma, lakini pia kibinadamu vijana hawa wameathirika kisaikolojia. Ni vyema Wizara ikawa na mkakati maalum katika kumaliza changamoto za namna hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na adhabu ya Mheshimiwa Waziri katika kusimamisha Bodi ya TCU lakini itoshe kusema adhabu hii haitoshi kwani katika kusimamisha bodi hii na watendaji wakuu bado mishahara wataendelea kuchukua, hivyo ni vyema Tume ya Uchunguzi ilichukulie hatua stahiki mapema iwezekanavyo ili Mheshimiwa Waziri aweze kupata timu sahihi ya watendaji itakayoweza kwenda sambamba na kiu ya Mheshimiwa Waziri katika kuleta ubora wa elimu ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hitimisho langu ningependa niombe mwongozo wa Mheshimiwa Waziri kuna sababu gani ya msingi iliyoilazimu Wizara ya Elimu katika kutenganisha mamlaka ya Bodi ya Mikopo na TCU kwani kimsingi TCU ina kurugenzi zote muhimu zinazoweza kusimamia mikopo ya elimu ya juu tofauti na leo tunapoona loans board inatengwa na TCU.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya TCU kuna kurugenzi ya udahili admission, accreditation, quality, assurance pamoja na finance. Nia nini haswa kilichopelekea kutenganisha mamlaka ya loans board na TCU? Ahsante, naomba kuwasilisha.