Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mimi nami pia nichukue fursa hii kumpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, kwa Presentation nzuri ya Mpango huu wa Maendeleo wa Miaka mitano lakini pia Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti kwa presentation nzuri pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti na timu yake nzima kwa kuliona suala la Bandari ya Bagamoyo ambayo hata Mheshimiwa Spika ameliwekea msisitizo hapa. Labda kwa haraka, nadhani mpango unao maeneo matano makubwa ambayo Waziri ame - present hapa lakini kwasababu ya muda mimi nitaongelea mbili tu. Nitaongelea kwenye kuimarisha uwezo wa Viwanda na utoaji wa huduma, lakini pia kukuza uwekezaji na biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani mara ya kwanza kabisa niliposiamama wakati nachangia nilisema kwamba nimekuwa katika viwanda kwa takribani miaka 14 nikifanya kazi kama engineer, kwa hiyo nina uzoefu mkubwa kidogo katika suala la viwanda; na bahati nzuri nipo kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara kwa hiyo sana naongea kwa experience yangu ambayo ninajua nimeiishi kama kazi lakini pia yale ambayo nimekuwa ninayaona huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, ila labda tu niweke angalizo. Tunapokuwa tunachangia hapa sio kusema tumetumwa labda na mabosi zetu wa zamani au tunakuja kumsemea mtu yeyote hapa. Tunachangia kwababu tunahakika na tunajua kila ambacho tunakifanya ni sehemu ya expertism yetu. Kwasababu ninakumbuka mara ya mwisho hapa kuna mtu aliniambia au hao wafanyabiashara wanawatuma mje kuwasemea, na hawapo humu by the way kwa hiyo tupo hapa kwa ajili ya kuwasemea kwababu tunajaribu kuangalia mianya ya kutengeneza kodi, mianya ya kukusanya fedha ili zile fedha ambazo Waziri hapa amewasilisha Trilioni 40 kwa miaka mitano tuweze kuzipata; tutazipata huko kwenye private sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani mmemsikia mchangiaji aliyepita Abbas Tarimba. Jana nimeona we are proud kwamba kuona Mtanzania sasa anakuwa recognize na nchi kubwa ambayo imeendelea kiviwanda kama South Africa. Kwa hiyo lazima tujue tunazo hazina hapa, kwa hiyo sasa ni jukumu la Mheshimiwa Waziri kuwaangalia wafanyabiashara wakubwa walioko kwenye nchi hii aweze kuwatumia. Maana najua ameweka mpango wa trilioni 40 kutoka sekta binafsi, anataka atengeneze ajira milioni nane kwa muda wa miaka mitano, mpaka 2026. Hizi ajira milioni nane hataweza kuzipata kama hatatafuta hawa watu wenye viwanda huko nje. Watu kama akina Dewji hawa na wafanyabiashara wengine wakubwa. awatafute akae nao na tuje na hii mipango mikubwa ambayo tunayo hapa, maana tunataka tutengeneze ajira, tunataka tukuze uchumi lakini huu uchumi hatutaweza kukukuza kama wenzetu huko nje hawajui mipango yetu sisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo nikuombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha tafuta muda wa kukaa na wafanyabiashara wakubwa na ni sisitizo usikae nao kupitia kwenye taasisi zao zile, kaa nao mmoja mmoja, mtafute mmoja baada ya mwingine, mwite, mwambie tuna mpango huu, unaweza ukawekeza kwenye nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana niko huku kwetu kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara tunahangaika kutafuta wawekezaji kutoka nje tuwalete hapa, lakini bado wapo wawekezaji wa Kitanzania wakubwa ambao wanaweza wakafanya biashara kutokaea hapa kuliko hata kumtafuta mtu wa nje ukamtumia mfanyabiashara wa Kitanzania aliyekuwepo hapa hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hili ambalo ameliona, hasa suala la Kodi maana mimi last time tumefanya ziara EPZA pale Ubungo niliumia sana, kwamba pale kuna Mtanzania ambaye anafunga kiwanda chake anakipeleka Uganda. Sasa nikawa nafikiria unapofunga kiwanda, leo sasa tunatafuta wawekezaji wa kuja kuwekeza hapa ila Mtanzania ambaye alikuwa ameweka mle ndani, anaondoa anakipeleka kiwanda kwenye nchi Jirani. Maana yake ni nini, obvious unapoenda kule watakuuliza kuna nini huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini haya mazingira ambayo Rais amesema mwende mkakae na wawekezaji. Ninaomba uyafanyie kazi haraka ili Watanzania ambao ndio watu wa kwanza kuwaleta watu wa nje kuja kuwekeza hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina experience kidogo, nilikuwa natoa mfano. Ukienda katika nchi ya Egypt, kuna sehemu ile ya ukanda wa Suez nimetembelea pale, mimi nikaona, yaani lile eneo utafikiri ni kama nchi ya China imehamia pale. Walichokifanya cha kwanza ni kwamba ili uweze kumvutia mwekezaji aje pale lazima uwe na Bandari. Ile Bandari ya Black Sea pale ndiyo inayotumika. Wachina wameletwa pale wakapewa eneo, bandari imejengwa wamejenga viwanda vingi sana maeneo yale. Kwa hiyo wanachokifanya wanaleta vitu vyao wanafanya process pale Bandari ipo wana-export kwenda Europe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo badala ya kuchukua mzigo kutoka China uusafirishe kwenda Europe kutoka Egypt kuushusha mzigo Ulaya inakuwa rahisi Zaidi, ndiyo kazi kubwa wanayoifanya hapa, sasa na sisi kama Kamati ya Bajeti ilivyo-suggest, tunayo nafasi kubwa zaidi ya kutumia Bandari ya Bagamoyo, kwasababu lile eneo la Bagamoyo ambayo tayari tulishalitenga na lilishalipiwa fidia takriban bilioni 27 zimewekwa pale. Hatuwezi kusema kwamba tuitelekeze.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukiweka pale na umwambie mfanya biashara atoke Dar es salaam anatoa mzigo Bandari ya Dar es Salaam anausafirisha mpaka Bagamoyo, aanze kuzalisha pale akimaliza kuzalisha ausafirishe tena kuurudisha Bandari ya Dar es Salaam afanye export, huo muda haupo, maana ni cost ya transportation ya kuja na kurudi, lakini vile vile na logistic inakuwa ngumu. Kwa hiyo nishukuru na niomba Waziri wa Fedha pigana unavyoweza bandari ile inyanyuke pale ili sasa fidia zile ambazo tumezifanya na uwekezaji mkubwa tunaotaka kuufanya Bagamoyo uweze kufanyika pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kilimo, kwababu tunaongelea viwanda vinavyoweza kuzalisha mazao haya ya kilimo mazao ya mifugo na pia uvuvi na madini. Labda upande wa kilimo Mheshimiwa Waziri kwa kushirikiana na Waziri wa Viwanda Waziri wa Killimo na hali kadhalika Waziri wa Fedha, mjaribu kutuangalizia njia sahihi ya kufanya. Wakulima wa nchi hii wanahangaika sana. Mimi ninaweza nikatolea wakulima wa upande huu wa Kagera; nilikuwa ninajaribu kufuatilia. Nchi ya Ecuador ndio nchi ambayo inaongoza kwa ku-export banana, ndizi hizi, 3.3 billion dollar per year, ina-export ndizi, hiyo ni hela nyingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika lakini sisi tupo pale, tulihamasishwa ndizi, watu wa Kagera mnaelewa, tumelima ndizi sasa hivi ndizi za mtwishe si zipo kule zimekaa hatuna hata watu wa kuwauzia tena? Maana unalima ndizi, Mkungu ambao hata hauwezi kuunyanyua shilingi 5,000 hatupati mteja tena. Sasa Mtusaidie. Maana nilikuwa ninaangalia hapa kwa Tanzania tume- export kwa mwaka tani 258. Tani 258 ukipiga kwa bei ya tani moja dola 300 katika World Market unaongelea dola elfu 75. Yaani mtu ana – export ndizi kwa dola 3.3 bilioni wewe hata dola laki moja haifiki, na bado tuna wakulima wanalima ndizi hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Unaongelea nchi kama Egypt, nimekuwa Egypt. Ukitoka Egypt, kama unatoka Cairo unaenda Alexander ile njia yote unapotembea imejaa zabibu, imejaa migomba na vitu vingine; nikawa najiuliza hawa watu wanafanyaje hawana maji hawana chochote kile. Wanachofanya zile ndizi wanatumia Irrigation.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unashangaa mtu hana mvua ana irrigate ndizi zile, ana export ndizi anapeleka Dubai ndilo soko lao kubwa. Sasa mimi hapa nina m vua ya Mungu ndizi zinaozea kule mtusaidie ili sasa tuweze kufanya biashara na tuweze ku-export ili ndizi hizi ambazo tunazilima katika kanda hizi ziweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najua wako Mbeya wako Kilimanjaro Mzee Mheshimiwa Dkt. Kimei amekuwa anaongea sana suala la ndizi kwa hiyo, haya ni mambo ambayo Serikali ikiingia kati ikaangalia jinsi ya kutusaidia itatutoa hapa tulipo itusogeze mbele maana hatuwezi kuongelea pamba tu hatuwezi kuongelea vitu vingine nadhani mmesikia hapa bei inashuka na kuongezeka. Lakini bado tunazo fursa nyingine za kupeleka matunda huko nje na vitu vingine vikaweza kutusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado dakika tano suala lingine niongelee suala la Liganga na Mchuchuma Mheshimiwa Waziri nimefika kule kwenye ziara yetu ya Kibunge lile eneo ni pori maana mwanzoni nilikuwa nawaza labda kuna hata majumba kuna hata nini ukifika kule mambo yale yanashangaza lakini umeiweka kwenye mpango humu vipaumbele sita ambavyo inabidi tuende navyo Liganga na Mchuchuma imo humu na mbaya zaidi Serikali tayari imeshaanza kuwekeza fedha nadhani mnajua tunajenga barabara ya zege tusingeweza kujenga barabara ya zege ya kilomita 50 sasa ya kuruhusu magari yaende kule kwenye ile migodi ile ni pesa nyingi sana ambayo tumeweka pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niombe nadhani kuna mambo ya kimkataba au mambo mengine ambayo yamekuwepo hapa biashara ni maelewano lazima ifikie stage ushuke ukae chini. Nimewahi kutoa mfano siku moja nimekuja kufuatilia biashara nimekuwa nafanyakazi kama Sales Manager kwa muda mrefu saa nyingine unaenda mpaka usiku hunywi pombe unakaa na mtu bar hapo unatafuta biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna siku nimeenda siku moja mchina mmoja anavuta sigara akipuliza moshi unaniingia puani lakini siwezi kumwambia usipulize maana nimekuja kutafuta biashara. Kwa hiyo, saa nyingine mkubali kushuka chini wafanyabiashara hawa tunapokuwa tunawatafuta kubalini kushuka chini twende tukae chini na hawa wachina, maana unashangaa hivi Mungu huyu aliwaza nini kipindi anakileta hiki kitu kwamba hapa kuna makaa ya mawe na hapa kuna mlima wa chuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwenyezi Mungu ametuletea kitu cha kufanya sasa niombe hiki kitu tuondoke sasa hivi Mheshimiwa Waziri jaribu kupigana waiteni hawa watu tukae nao chini tuongee kama huu mradi kweli una faida kubwa kama hiyo ni lazima huyu mwekezaji hawezi kuja kushindwa kuwekeza hiki kitu hapa ili tuondoke sasa kwenye hii stori ya Liganga na Mchuchuma ambayo tumeisoma tangu Shule ya Msingi mpaka leo watu tunapata mvi na haijawahi kufanyakazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe Mheshimiwa Waziri hili suala lichukulie serious ili sasa itutoe hapa maana matatizo mengine madogo madogo tunayoyasema yatakwisha na yatakwisha kabisa yatamalizika. Maana najua tunawekeza hela nyingi sana kwenye bwana la Mwalimu Nyerere lakini ile ni megawati 2115 hapo unaongelea megawati 650 almost 1/3 tu sasa 1/3 tunashindwa kukomboa pale maana ni vitu vingi tutapata chuma tutapata umeme, tutapata makaa ya mawe vitu vyote vitamalizika pale na bado Serikali itapata pesa ya kuweza kutusaidia kufanya miradi kwa hiyo niombe na hilo uweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia suala la kumalizia niombe viwanda nimekuwa naongea hilo jambo hata kwenye kamati Mheshimiwa Waziri ukijaribu kuangalia wenzetu ningeomba mfanye kitu kimoja kama Serikali na kama Wizara tunazungukwa na nchi tisa hapa ambazo zinatumia Bandari ya Dar es Salaam leo hatuna haja ya kuacha Toyota wana-assemble magari Japan halafu Toyota wana export magari ambayo yako assembled wanayaleta hapa? Why don’t we sit down na Toyota tujaribu kuangalia Serikali ni mteja mkubwa wa Toyota tuangalie tuongee na Toyota tunavyokuja kutengeneza sehemu hii ya Bagamoyo special economic zone, tumuombe Toyota aje aweke hapa akiweka plant yake yaku-assemble tu maana yake ni kwamba nchi zote Jirani ambazo zinatumia magari ya Toyota tutapata advantage magari yanakuwa assembled hapa kutoka kwenye bandari yetu wanakuja wanachukua hapa kiwanda kinakuwa cha kwake analeta watu wake lakini tunapata ajira pia na uzoefu wa kuweza kujifunza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maana nimeona hiyo sehemu nyingi hata Nairobi leo tukiongelea pump za KSB Waziri wa Maji yuko hapa nimalizie hiyo dakika moja Waziri wa Maji yuko hapa pump za KSB the needing company ni Wajerumani wale lakini leo assembly inafanyika Nairobi ilikuwa inafanyika South Africa lakini leo assembly inafanyika Nairobi wenzetu wamefanya bidii ya kwenda ku-lob kule hatimae ikaja hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe brand kubwa ambazo wengi wana export kwa kutumia bandari ya Dar es Salaam Mheshimiwa Waziri angalia Serikali muangalie kama tunaweza kuonana na hawa watu waje waweke viwanda vyao hapa wafanye assembly hapa vitu vitakuwa vinatoka vimekamilika vinaenda kwa wenzetu naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)