Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii niweze kuchangia Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Taifa wa Miaka Mitano. Mpango huu wa Tatu wa Miaka Mitano unajengeka toka kwenye Mpango wa Pili wa Miaka Mitano ambao tumeukamilisha utekelezaji wake mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja katika mambo makubwa ambayo yamebebwa na Mpango huu, ni dhana ya kujenga misingi ya uchumi wa viwanda. Na hapa nitaweka mkazo, kujenga msingi wa uchumi wa viwanda. Maana yake nini, tuliamua, kwenye ujenzi huu wa uchumi wa viwanda au ujenzi huu wa msingi wa uchumi wa viwanda uzingatie viwanda vyenye sifa kubwa mbili. Sifa ya kwanza, viwanda vinavyotumia malighali ya ndani. Lakini sifa ya pili, ni viwanda ambavyo vitatoa huduma au vitakuwa na impact kwa watu wengi, kwa maana ya critical mass. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunapoongea viwanda vinavyogusa au viwanda ambavyo vitatumia malighafi ya ndani, moja katika eneo muhimu sana ambalo lingetupa malighafi ambayo sio tu yanakwenda kutengeneza viwanda lakini nayo ni msingi wa viwanda ni chuma ya Liganga na Mchuchuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasikitika huu ni karibu ni mwaka wa 20 au zaidi tunaongea kuhusu kwenda kuchimba chuma ya Liganga. Labda niseme mawili au matatu kuhusu hii Chuma ya Liganga. Kwanza inaambatana na uzalishaji wa umeme megawatts 600. Megawatts 600 ni robo ya umeme wote ambao tulikuwa nao mpaka mwaka 2015. Robo, yaani asilimia 25 sio mchango mdogo kwa uchumi wa Taifa letu. Kwa hiyo, ule mradi sio kitu kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili, mradi wa Liganga na Mchuchuma unaenda kuzalisha iron owl chuma ngumu, tani milioni moja kwa mwaka. Sio jambo dogo, lakini sasa manufaa ya malighafi ya chuma ni makubwa sana kwa uchumi wetu wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, chuma ya Liganga ingeweza kuzalisha viwanda vya nondo vya kutosha na vya kumwaga nchi hii, Chuma ya Liganga ingeweza kuzalisha viwanda vya mabati nchi hii, ingeweza kuzalisha viwanda vya baiskeli na vipuri vya magari vya kutosha kwa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, jaribu kufikiria ni viwanda vingapi na vya aina ngapi vingeweza kuzaliwa kutokana na uchimbaji wa chuma ya Liganga na Mchuchuma ukiachilia mbali suala zima la ajira kwa watanzania walio wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo nyakati pia tujifunze kwenye mataifa mengine Marekani, waliamua kuchelewesha ujenzi wa reli ili kujenga uwezo wa ndani wa kuchimba chuma yao ili wajenge reli yao kwa kutumia chuma yao. Maana yake ndio soko la kwanza la chuma yao ilikuwa ujenzi wa reli yao. Sisi nasi tuna fursa kubwa kwenye eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwenye eneo hili nimuombe sana Waziri wa Fedha, Ndugu yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, arejee kwenye ajenda zetu tangu mwanzo huwezi kujenga uchumi wa viwanda Tanzania kama hutaki kwenda kuchimba chuma ya Liganga. Tutadanganyana, tutapiga kelele hapa, miaka itapita, nyakati zitabadilika na vizazi vijavyo vitatushangaa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili, tulivyosema tunataka tujenge viwanda ambavyo vitatumia malighafi ya ndani na vina critical mass tulisema viwanda ambavyo vita- absolved bidhaa na mazao ya wakulima kwa asilimia kubwa. Mambo niliyotarajia niyaone kwenye Mpango wa mwaka 2015/2016 – 2020/2021 moja nilitaka nione viwanda vingi vya kusindika mazao ya kilimo na mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ametoa mifano ya viwanda lakini ukivipima kwa mizani, viwanda ambavyo vina critical mass effect ni vi chache sana ambavyo vinagusa mazao ya ngozi, vinagusa mazao ya kilimo. Mheshimiwa wa Wiziri wa Fedha ulikuwa kwenye Wizara ya Kilimo, unajua huwezi kukuza kilimo kama hutakuza viwanda vinavyosindika mazao ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nina aamini, wakati huu upele umempata mkunaji na mkunaji ndio Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba ulikuwa kwenye sekta ya kilimo sasa upo kwenye Wizara ya Fedha peleka fedha kwenye kilimo, peleka fedha kwenye ku-facilitate kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huwezi kupata mapinduzi ya viwanda kama hutaki kuwekeza kwenye utafutaji wa masoko ndani na nje ya mipaka yetu ya Tanzania. Leo tunaongelea barabara za mipakani bado hazipitiki hazina lami, soko kubwa la Mazao ya mkoa wa Ruvuma tunategemea Msumbiji lakini tunatumia barabara ya vumbi. Hatuwezi kujenga uchumi kama hatutaki kutengeneza miundombinu ambayo itakuza biashara, itakuza viwanda. Na mimi naamini hii kengele ya kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninazo hoja tatu za haraka. Eneo la tatu, uwekezaji kwenye biashara unahitaji facilitation na hapa tuna mifano mingi sana leo, tunataka tuingie kwenye soko la Dunia lakini hatujaweka mechanism ya kutosha kuwawezesha wafanyabiashara wa Tanzania kuweza ku-meet vigezo kwa maana ya quality and quantity demands za soko la nje, hatutaweza! Hatutaweza kufika huko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja zilizobaki nitazihifadhi lakini nilitaka niseme tunapotaka kubadilisha uchumi wa nchi yetu pia lazima tuwekeze kwenye diplomasia ya uchumi, lazima tuwe na mazuri na majirani zetu, lazima tuunganishe nguvu zetu za ndani na nje ili tulete mapinduzi ya uchumi kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)