Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kunipa nafasi ya kuchangia. Kwanza kabisa nikiri kwamba mwaka 1999 na kuelekea mwaka wa 2000, Taifa letu la Tanzania lilipata msiba wa kuondokewa na Hayati Baba wa Taifa letu Mwalimu Nyerere. Taifa lilishuka sana na Watanzania waliingiwa na majonzi na wengi wakajiuliza nini itakuwa hatma ya Taifa letu. Hata hivyo, kutokana na uongozi madhubuti na uimara wa chama kilichopo madarakani Chama Cha Mapinduzi, Taifa la Tanzania liliendelea kuwa stable na nchi iliendelea kuwa moja na maendeleo ya kiuchumi na kijamii yaliendelea kuonekana katika nchi Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, pia mwaka huu pia Taifa la Tanzania lilimpoteza Rais wake ambaye alikuwa kipenzi cha Watanzania, Rais ambaye alikuwa mzalendo, shujaa, jasiri, mwenye kuongoza njia, Rais aliyeaminiwa na umma ambaye na kuleta imani kubwa duniani, kifo chake na maombolezo yake yamedhihirisha namna gani Watanzania na dunia kwa ujumla ilikuwa na imani kubwa na rais huyu, lakini Watanzania wengi waliingiwa na hofu wakaona sasa Tanzania itakwenda wapi. Kuonesha umahiri wa chama kilichopo madarakani kwamba ni chama kinachoweza kuwaandaa viongozi, leo tunapozungumza kila nchi, Raisi aliyepo madarakani Mama Samia Suluhu Hassan, kila mmoja anatoa makofi na pongezi kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachoweza kusema ni kwamba Chama Cha Mapinduzi ni ngalawa imara inayoweza kuwaandaa viongozi wa kuliongoza Taifa wakati wowote wa shida na raha. CCM ni tanuru la kuandaa viongozi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika,, naomba niende kwenye hotuba yangu. Sasa nakwenda kuzungumzia maeneo makubwa mawili hasa katika sekta ya kilimo. Nashukuru namwona kaka yangu Bashe huwa ni Naibu Waziri msikivu sana, mara nyingi Wabunge wanapozungumza huwa ana-take note kwa manufaa ya Taifa. Naomba nitoe takwimu zifuatazo:-

Mheshimiwa Spika, Nchi ya Misri, ambayo kwa asilimia karibu sabini kama sio themanini ni jangwa; nchi ya Israel ni jangwa. Naomba Bunge lako Tukufu lisikilize takwimu zifuatazo: Taifa la Misri katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji licha ya nchi kuwa imezungukwa na mto mkubwa ambao kimsingi chanzo kikubwa cha mto huo kinatoka Tanzania, ukiangalia takwimu zinaonesha Taifa la Egypt moja ya vyanzo vikubwa vinavyofanya nguvu za kiuchumi za Nchi ya Egypt ni kilimo cha umwagiliaji. Kama haitoshi takwimu zinaonesha Taifa la Misri limewekeza zaidi ya hekta milioni 3.4 kwenye Sekta ya irrigation peke yake.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia takwimu suitability ya land ya Misri na Tanzania ni tofauti kama mbingu na ardhi. Availability za resources kama maji, manpower na mengine, ni sawa na mbingu na ardhi, kwa maana ya kwamba Tanzania hiko katika competitive advantage ya ku-invest kwenye kilimo cha umwagiliaji, lakini angalia takwimu kwa nchi yetu. Namwomba kaka yangu Mheshimiwa Bashe na Mheshimwa Waziri wameaminiwa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Mchango wangu wa kwanza nilipoingia kwenye Bunge hili nilizungumzia habari ya sekta ya Irrigation, that was my first mchango kwenye Bunge la Tanzania. Nilitoa mifano na nikatoa ushauri, namna gani Serikali ya Chama Cha Mapinduzi tunaweza tukalipindua Taifa hili likawa Taifa la ku- export mazao duniani kote na watu wote tukainua uchumi wa Taifa, kwa Tanzania sasa tunapozungumza eneo ambalo tumelitumia peke yake kwa umwagiliaji ni hekta elfu 19 wakati Egypt they have 3.4 million na hawana suitable land kwa ajili ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, natoa takwimu hizi huku nikiwa natambua kabisa, Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi, kama kweli wataamua kudhamiria kusaidia kilimo cha nchi hii katika sekta ya umwagiliaji, nakwenda kutoa mfano, nimekuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga kwa miaka takribani minne. Irrigation scheme kubwa katikja Mkoa wa Tabora iko Wilaya ya Igunga inaitwa Mwanzugi. Production inayofanyika kwa lile shamba dogo, nataka nikuhakikishie, ndio irrigation inayolisha mchele wote wa Rwanda, Uganda pamoja na nchi za Burundi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa takwimu hizo, nilitoa mchango wangu nikashauri, suitable land tunayo ambayo inafaa kwa irrigation, kwa Tanzania tuna potential ya 2.1 million hekta za irrigation katika nchi zetu. Nilitoa mfano tukiamua kuwekeza, Mheshimiwa Bashe kaka yangu na Wizara na wataalam wakaenda pale Igunga peke yake wakaamua kuyatenga yale maji ya Mto Manonga, wakatengeneza mabwawa, irrigation peke yake Mkoa wa Tabora tuna uwezo wa kulisha nchi zaidi ya nne kwa chakula na mazao mengine ya kibiashara tunaweza kuyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi, hili Bunge ndio mahali peke yake ambapo tunaweza kutoa mawazo ya kuisaidia Serikali, inapotengeneza mipango, Taifa hili likapiga hatua. Kama Rais Hayati Magufuli alivyokuwa anasema, Taifa hili sio maskini, nchi hii tunakosa kuwa na mipango mikakati na mambo ya vipaumbele ambavyo vinaweza vika-turn upside down maendeleo ya nchi hii. Niiombe sana Wizara ya Kilimo, kama kuna eneo Bashe na watu wako na Wizara wanatakiwa kufanya waende wakawekeze katika kilimo cha umwagiliaji, hicho peke yake kitaleta suluhu ya kuongeza export nje ya nchi na kufanya Taifa letu liweze kuendelea.

Mheshimiwa Spika, nimetoa mifano Egypt peke yake ukingalia statistic za dunia, fedha wanazoingiza Egypt kutokana na kuuza matunda, ulitupa fursa mwaka juzi, tulikwenda Egypt na timu ya Taifa, tulikwenda kutembelea miradi. Ile ilikuwa ni fursa ya kimichezo, lakini tulijifunza kitu, tulienda kutembelea Irrigation za zabibu, tukatembelea irrigation mbalimbali, Egypt is complete desert. Hata hivyo, kinachozaliwa nilipoona yale mashamba nikaangalia baraka za nchi yangu Mungu aliyonipa hii Tanzania, I was so much embarrassed. Tuna uwezo Tanzania tunakwama wapi? Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye mipango yetu waandike, walete fedha, wasaidie kilimo cha umwagiliaji kwenye Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, ulikuja kunizindulia kampeni kwenye jimbo langu, mahali pekee yake ulipokuja kuzindua kampeni pale Mgungila, pale tuna maji ambayo yanapotea na nakwambia leo tunavyozungumza Mkoa wa Singida, mchele wote karibia asilimia 75 unatoka Mgungila, lakini wale wakulima they are just doing agriculture on their own skills, hakuna mipango ya Serikali, bonde kubwa lina…

Mheshimiwa Spika, haya mambo jamani, napata shida sana. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Kingu, watu wa kilimo kila wakileta bajeti ni ya kununua laptop, kunuua pikipiki, zinatakiwa zielekee huko.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimwa Spika, kabisa kabisa, yaani hili Taifa nawaambia, tukidhamiria kufanya mambo na hakika kwa hii style ambayo Serikali yetu ilikuwa inakwenda, nakwambia nchi hii in next ten years to come hili Taifa halitasogelewa na nchi yote kwa Afrika kwa sababu kila kitu tunacho. (Makofi)

Mheshimwa Spika, jambo la pili, kwa mfano tumechukulia hata ukiangalia katika kilimo amechangia kaka yangu pale, amezungumza habari ya pesa tunazotumia, sasa hivi potential iliyopo ya ku-import mafuta ya kupika, inakwenda karibia dola billion 275, that is the potential. Sasa tukiamua kufanya PPP aliyokuwa anaisema kaka yangu, tukashirikiana na Serikali, wakafungua block farming ambazo huwa tunazungumza na Mheshimiwa Bashe ya alizeti, nasema, fedha tunazozitumia kuagiza mafuta peke yake kwenye kilimo, block farming zikiwepo za mfano, sisi Singida tumemwambia Mheshimiwa Bashe, tuko tayari kumpa maeneo ya kutosha ya alizeti kufungua block farming ambazo zitakuwa mfano ili Taifa liweze kuzalisha mafuta.

Mheshimiwa Spika, hii nchi tunaweza kufanya mambo makubwa na mazito endapo Serikali itapokea ushauri wa Wabunge na kuacha kuona Wabunge tunaoshauri kama maadui. Maana kuna Mawaziri wengine ukiwashauri, we have to be honest, anakuona adui, yaani unaona kabisa Waziri anakuona huyu mtu adui. Kuna Waziri mmoja nilishauri kwa nia njema, Waziri mwenyewe ni Mheshimiwa Mwambe, nikasema angalieni kuna shida ya masoko ya Watanzania. Mheshimiwa aknijibu in very arrogant way, mimi ni Mbunge mwakilishi wa watu, Mawawiri tunapotoa michango tuheshimiane, we are doing this for interest ya nchi. Jibu alilonipa; wewe bwana kama nyama yako imekosa soko…, mimi siuzi nyama. Nikizungumza hapa kwa niaba ya wafanyabaishara, nisichukuliwe nimetumwa, wale ni Watanzania na sisi ni sauti yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, I am very sorry kama nitakuwa nimem-offend, lakini I was so embarrassed, hilo siyo jibu la Waziri anayetokana na Chama Cha Mapinduzi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho, naomba nizungumzie upande wa marketing. Upande wa marketing natoa mfano mdogo, Taifa la Ethiopia lilifungiwa kupata market ya kuuza nyama kwa nchi za kiarabu, in within three days, Mawaziri zaidi ya sita walifunga safari kwenda kufungua masoko ya watu wao. Sisi hapa kwetu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, naunga mkono hoja. (Makofi)