Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuwa mchangiaji katika mpango huu. Lakini awali ya yote kwanza naomba nichukue fursa hii kuwapongeza Wabunge wenzangu ambao wameteuliwa katika portfolio mbalimbali nataka niwaahidi tu kwamba sisi tutaendelea kuwapa ushirikiano katika nafasi zao walizonazo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kama hivyo haitoshi vile vile nilikuwa naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Waziri wa Fedha kwa uwasilishaji wake mzuri ambao ameweza kuuwasilisha katika suala zima la mpango huu.

Mheshimiwa Spika, lakini kama hivyo vilevile haitoshi nimshukuru mwenyekiti wetu wa kamati ya bajeti kwa vile vile kuweza kuwasilisha na kuweza kutoa maoni mazuri zaidi kuhusiana na suala la mpango huu.

Mheshimiwa Spika, kubwa kuliko lote nimshukuru Mheshimiwa Rais wetu mama yetu mama Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri sana kwa kuweza kuwatia matumaini watanzania ambao walikuwa tayari wameshapoteza matumaini na walikuwa na vilio ndani ya nafsi zao. Lakini mama ameanza vizuri sana na naomba tu nipite katika kauli yake niseme wale ambao wanakusudia kumzingua mama basi tutakwenda kuzinguana nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba ni nichangie mpango huu katika maeneo mawili tu. Eneo la kwanza ni suala zima la tax base na eneo la pili ni suala zima la performance of the projects hizi kubwa kubwa ambazo tunaendelea nazo sisi kama nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika suala zima la kuchangia kwenye tax base kuongeza wigo wa tax base nilikuwa naomba kidogo nitoe ushauri hapa kwa Serikali. Hizi tough decision kuzichukua wakati mwingine kuzichukua zinakuwa ni ngumu lakini they are wealth taken mimi nilikuwa naomba niishauri Serikali tuangalie uwezekano wa ku-reduce cooperate tax rate tukifanya hivyo tafsiri yake ni nini tutakwenda kutengeneza kitu kinachoitwa multiply effects tunapo reduce cooperate tax rate tunawa-encourage cooperate citizen siyo tu wale kutoka nje lakini hata hawa wa local investors wale wenye mitaji iliyokuwa iko ndani sasa watatoka na watakwenda ku-invest maeneo tofauti.

Mheshimiwa Spika, sasa tunakwenda kutengeneza multiply effect kwa kufanya hivyo. Tafsiri yake pana ni kwamba anapokuja mtu aka-invest, mndengereko kama mimi nikawa na hela yangu ya mkopo nikachukuwa, nikaenda ku-invest kwenye kiwanda, ni kwamba nitaajiri watu. Ninavyoajiri watu, kinachofuata maana yake ni kwamba tunakwenda kuongeza wigo wa tax; na wale watu wanaokwenda kuajiriwa pale, tuta-improve their standard of living.

Mheshimiwa Spika, hii ni very basic economics ya form four sijui form five na nafikiri Mheshimiwa Waziri you know better than this. We have to reduce the corporate tax rate, lazima tucheze na fiscal policy ili sasa tuweze kuwa- encourage investors waje waweze ku-invest. Mama yetu alisema hii katika hotuba zake katika mambo aliyokuwa anazungumza, kwamba lazima tutumie fursa mbalimbali ili kuhakikisha kwamba hatuwakumbizi wawekezaji, tunawavuta ili tuendelee kuwa nao. Kwa kufanya hivyo, tafsiri yake ni kwamba lazima tuchukue tough decision. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna nchi ambazo zimeweza kufanya hivyo. Marekani katika miaka ya nyuma huko waliweza ku-reduce tax corporate rate na athari yake ni kwamba, kukawa na viwanda vingi, wawekezaji wakawa wengi waka-increase vilevile rate employment. Tukifanya hivyo, ile corporate tax base tunaiongeza.

Mheshimiwa Spika, wale watu ambao tunawakamua; nakumbuka kuna Mheshimiwa Mbunge mmoja; mwanangu mmoja kutoka Mtama aliwahi kuzungumza kwamba ng’ombe tunamkamua mpaka inafikia hatua sasa hakuna cha kumkamua. Tafsiri yake ni kwamba we do have to expect kwamba hawa larger tax payer ndio watakuwa wao tu peke yao wanaweza waka- finance hizi fedha ambazo tunaenda kuzikusanya kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo ndani ya nchi.

Nilikuwa naomba nishauri katika eneo hilo. Eneo la pili katika suala lazima la kungoze hii tax base…

SPIKA: Mheshimiwa Twaha, mwanao anakuangalia.

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, mwanangu ananiangalia!

SPIKA: Mh! Endelea Mheshimiwa. (Kicheko)

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Sawa. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, vile vile katika suala la kuongeza hii tax base nilikuwa naomba niishauri Serikali tuongeze wigo, tumefanya vizuri sana katika suala zima la electronic stamp, tumefanya vizuri sana kule kwenye wine katika mambo ya spirit tumefanya vizuri sana kwa sababu tumeweza ku- increase ile collection. Kwa mfano tumeweza ku-increase domestic collection 74.4 percent katika quarter ya kwanza ya 2020.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, Value Added Tax ilikuwa imeongozeka 22.8 percent, vile vile tumeweza ku- increase suala nzima la makusanyo ya soft drinks kwenye asilimia 11.7. Hapa tumefanya vizuri. Sasa ni muhimu vile vile Serikali tukaongeza ile electronic stamp katika point of production kwenye maeneo mengine. Kwa mfano katika sekta nzima ya uzalishaji wa cement, kule bado hatujakugusa.

Mheshimiwa Spika, watu wengi sana wanatumia cement na action ambayo inafanyika kule, we can not control it. Katika maeneo mazima ya mambo ya nondo, mabati, we cannot control it. Kwa hiyo, ili sasa ili tuweze ku- extend ile tax base, mambo ya namna hii lazima tuweze kuyashungulikia. Tumefanya vizuri, lakini naomba kuishauri Serikali tuendelee kuweka msisitizo katika maeneo hayo mengine ili sasa tusije tu tukawabana wale larger tax payers peke yao. Wanatukimbia, wanaondoka.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana mama yetu wakati anahutubia Taifa, watu wengi sana waliweza kupongeza hotuba ya Mheshimiwa Rais. Wakati nikiwa hapa, Wandengereko wenzangu kutoka Kibiti walikuwa wanapiga simu na kutuma message kedekede wakisema kwamba sasa jembe limekuja na tunakwenda kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ni lazima tuangalie, hii tax burden tuweze kui- balance. Tukifanya hivyo, nafikiri tutafanya vizuri sana, collections zetu za ndani zinaweza zikaongezeka.

Mheshimiwa Spika, sehemu nyingine ambayo nilikuwa naomba niichangie ni katika suala la zima la PPP. Mimi ni mgeni hapa Bungeni, lakini I know for sure, kwa kupitia paper works nilijua kuna Sheria ya PPP ililetwa hapa na ikaja mwaka 2018 kufanyiwa some amendments. Nilikuwa naomba niishauri tena Serikali, kama kuna upungufu katika sheria ile, basi iletwe tena tuweze kuishungulikia, kwa sababu miradi mikubwa mikubwa hii ni lazima tuifanye kwa kupitia PPP. Tukifanya hivyo, tafsiri yake ni kwamba haka kasungura kadogo, fedha zetu hizi za ndani tunazozikusanya zinaweza zikaenda kutusaidia ili kuweza kuendeleza huduma za jamii.

Mheshimiwa Spika, mfano katika Sekta za Afya na katika mambo mengine fedha hizi zinaweza kutumika. Kwa hiyo, miradi mikubwa mikubwa hii ili tuweze kuiendeleza vizuri zaidi, basi ile idea ya PPP tuilete tena hapa kama ile sheria ina upungufu. Kwa sababu tunapozungumzia PPP, tunazungumzia mifano tunayo pale ndiyo, tumejenga mabweni, lakini tuzungumzie substantial, ile miradi mikubwa mikubwa kama Serikali. Tunakwenda kutengeneza pale mradi wa Mwalimu Nyerere. If not, twendeni kwenye PPP. Najua tunatumia fedha zetu za ndani, ni suala la busara zaidi.

Mheshimiwa Spika, kama hivyo haitoshi, siyo vibaya vile vile, tukiona kwamba mazingira siyo rafiki and of course it has to be so, twendeni tukatumie PPP ili sasa kwa namna moja ama nyingine, miradi hii iende sambamba na iweze kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, uliweza kutoa hapa maelezo kidogo kwamba mabehewa siyo lazima tu yashughulikiwe na watu wengine, sisi wengine tuliwahi kupata bahati kukaa kwa Wandengereko nchi za nje huko, tuliona. Ukienda pale UK utakuta zile British reli zinazokuwa zinazunguka, siyo zote zinakuwa controlled na British Government. Unaweza ukakuta kwamba kuna tajiri tu mmoja anashughulikia eneo fulani, tajiri mwingine anashughulikia eneo fulani lakini mambo yanakwenda.

Mheshimiwa Spika, when you talk about infrastructure in UK it is superb, ipo namba moja. Sisi twendeni tukaige mambo haya, wakati ndiyo huu. Mama tunaye, Mheshimiwa Samia anatupa sana uwezo sisi Watendaji. Ameweza kutupa fursa kusema kwamba tumieni vipaji mlivyonavyo ili tuweze ku-extend tax base tuweze kuongeza maendeleo.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba sana nichangie katika haya maeneo mawili. Hata hivyo, katika suala hili la tax base nitakwenda kwa Mheshimiwa Waziri kwa wakati maalum kumpa takwimu ambazo ni research ambayo nimeweza kuifanya kwenye Commercial City pale Dar es Salaam. If you look at the number from 2015 to date, the number of corporate citizen ambazo tayari zimeshafungwa they are so many.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia amount of tax tunazo- collect zina-increase katika decreasing rate, iko pale Dar es Salaam. Mheshimiwa Waziri akiniruhusu, mimi nitakwenda, nitamfuata, nitampa research ambayo tulikuwa tumeifanya. Sasa ni lazima tuchukue maamuzi magumu ili tuweze kusonga mbele na tuweze kum-support mama yetu katika kuweza kuleta maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru, naunga mkono hoja. (Makofi)