Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuhitimisha Hoja ya Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya Wabunge 23 walipata nafasi ya kuzungumza. Iingie kwenye kumbukumbu za kudumu za Bunge kwamba hoja hii ni moja katika hoja chache sana ambazo ndani ya Bunge lako zimepata kibali toka pande zote za Wabunge bila kuyumba. Sababu ni kwamba Waheshimiwa Wabunge wote wanaamini kwamba mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, hayawezi kutenganishwa kamwe na mafanikio ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambaye alihudumu kama Makamu wa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna eneo moja limezungumzwa kwa namna ambayo linahitaji kidogo tulifafanue; hoja ya demokrasia na uhuru wa Habari. Kwamba Mheshimiwa Khatib na baadhi ya Wabunge humu ndani kuweza kuhama kutoka kwenye Chama cha CUF na kwenda ACT Wazalendo na kuweza kushiriki katika Uchaguzi na kushinda na kuzungumza ndani ya Bunge hili ni demokrasia ya kiwango cha juu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, demokrasia huanzia ndani ya vyama. Kitendo cha Chama Cha Mapinduzi kuendelea na utaratibu wa kubadilisha wenyeviti wao kila miaka kumi ni kielelezo cha kutosha cha ukomavu wa demokrasia ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeshauri vyama vingine vifuate utaratibu huo kwa sababu huwezi kuwa na legitimacy ya kupigania demekrasia nje kama hujaimarisha demokrasia ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, tafsiri sahihi ya demokrasia; na hapa namnukuu Balozi Dkt. Wilbrod Slaa; demokrasia ya kweli ni demokrasia ya kuwasikiliza na kuwahudumia watu wanyonge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wa Tano alifanya kazi hii kwa uaminifu mkubwa akishirikiana na Rais wetu wa sasa, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Kote walikopita Watanzania wamelilia elimu, maji, huduma za afya, mahitaji ya mitaji kwenye biashara na yale yote yaliyowekwa kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na hayo yote ndiyo yaliyobebwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema maneno hayo, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.