Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hon. Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami niungane na Watanzania wenzangu kutoa pole kwa Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan, Mheshimiwa Spika wa Bunge na wewe mwenyewe kwa sababu Rais aliyetangulia alikuwa sehemu ya Bunge. Pia nitoe pole kwa wakazi wa Chato na Biharamulo kwa ujumla sababu sisi ndiyo wenyeji zaidi pale kwa hiyo, msiba ule ulikuwa nyumbani na nawashukuru wote walioungana nasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye kuchangia ninayo mambo mawili ya kumuelezea Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Cha kwanza kila binadamu anapozaliwa ana mambo mawili makubwa katika dunia hii. Incident mbili kubwa katika dunia kwa mwanadamu, kwanza ni kuzaliwa na pili kugundua kwa nini umezaliwa. Watu wengi tunaishi hatujui kwa nini tumezaliwa au kwa nini tupo hapa duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa kesi ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aligundua purpose ya Mungu kumleta duniani. Nakumbuka mwaka 1990 nikiwa mdogo akiwa anagombea Ubunge kwa mara ya kwanza Biharamulo kila alichokuwa anakifanya au statement yake kila mmoja alikuwa anamuelezea. Tukiwa wadogo tunaambiwa kuna mtu anaitwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli that time yuko Chato mimi niko Biharamulo.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwa Mbunge kwa mara ya kwanza mwaka 1995 nyote ni mashahidi, Naibu Waziri wa Ujenzi kila alichokigusa aliacha alama. Hakuna sehemu Raisi Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amepita hakuacha alama. Mmemsikia Rais Jakaya Kikwete juzi kwenye suala la ujenzi, ardhi, uvuvi na hata alipomrudisha ujenzi. Hatimaye Watanzania na Chama cha Mapinduzi kikaona na kumuweka kuwa Rais. Alipokuwa Rais alama ile aliyoiweka katika maisha yake kwamba kila anachokabidhiwa kufanya lazima akifanye kwa hundred percent haikukoma. Watanzania wote ni mashahidi ujasiri wa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kuamua mambo, ujasiri wa katika kuipigania nchi hii haukuanza akiwa Rais umeanza back-and-forth na alipokuwa Rais mambo aliyoyafanya ni makubwa mmeyasikia hatuna haja ya kuyarudia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo moja kubwa ambalo nilimuuliza Mungu wakati ule napokea taarifa hizi, nikasema why God, kwa sababu niliumia sana nikajiuliza kwa nini uruhusu hili jambo katika wakati kama huu? Ila nikarudi katika Maandiko Matakatifu nikamkumbuka Musa alivyopigana na wana wa Israel, najua safari ilikuwa ngumu hata safari ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imekuwa ngumu kwa sababu kipindi anaenda hivi kuna wengine walitaka kurudi nyuma na wengi wamekuwa wanapigana kurudi nyuma lakini hakukata tamaa. Nikakumbuka Musa alipopandishwa katika mlima ule na akaoneshwa nchi ya ahadi kule lakini akaambiwa kazi yako imeishia hapa na hautarudi huko na wala hutaiona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka kuwaambia ni nini? Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliletwa na Mungu kwa ajili ya kazi maalum katika nchi hii, amemaliza kazi ile ambayo Mungu alimleta aifanye, tuendelee kumuombea na kuyaishi yale aliyofanya. Ninachotaka kuwasihi Watanzania na Wabunge wenzangu baba huyu aliletwa kwa purpose, akagundua purpose iliyomleta hapa, kafanya sehemu yake na amemaliza. Hata sisi sasa tunachotakiwa tumuenzi nacho kila mmoja ajitafakari ajue purpose yangu mimi kuwa duniani ni nini na purpose ya wananchi walioniamini kunileta Bungeni ni nini. Tukiyajua hayo basi tukaisimamie Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili maendeleo haya ambayo Rais wetu alitamani kuyaona aweze kuyaona yakifanyika na Watanzania waweze kuyapokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka kuwasihi Watanzania na Waheshimiwa wabunge wenzangu, baba huyu aliletwa kwa purpose akagundua purpose iliyomleta hapa kafanya sehemu yake amemaliza. Hata sisi, tunachotakiwa tumuenzi nacho, kila mmoja ajitafakari ajue purpose yangu mimi kuwa duniani ni nini? Purpose ya wananchi walioniamini kunileta Bungeni ni nini? Ili tukiyajua hayo tukaisimamia Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ili maendeleo haya ambayo Rais wetu alitamani kuyaona aweze kuyaona yakifanyika na Watanzania waweze kuyapokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo labda, nirudi kwenye suala mama pia, kumpongeza mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme neno moja tu; watu wote wameongea katika habari ya wanawake, lakini mimi niseme hakupewa nafasi ya Makamu wa Rais kwa sababu ni mwanamke, alipewa nafasi ya Makamu wa Rais kwasababu ame-demonstrate na ameonesha uwezo wa kupata nafasi ile. Kwa hiyo tunaposimama hapa, tusimame hapa tukijua tunaye Rais mwenye uwezo ambaye aliaminiwa na Chama mwaka 2015 kipindi Magufuli anaingia, akiwa hajulikani kama atayafanya haya halikadhalika Mama Samia aliingia akiwa hajulikani kama atayafanya haya. Lakini chini ya uongozi imara, chini ya Ilani ya CCM wakayasimamia wakatufikisha hapa walipotufikisha. (Makofi)

Labda neno moja tu la biblia ambalo nataka niliseme kwa ajili ya Mheshimiwa Rais, nikikaribia kukaa, maana najua wote tumeshaongea mengi. Tuki-refer katika Kitabu cha Ezra 10:4 inasema “Inuka maana kazi hii inakuhusu wewe. Na sisi tu pamoja nawe, uwe na moyo mkuu ukaifanye”.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba Wabunge tuko na Rais wetu, Watanzania wako na Rais wetu, ameambiwa ainuke na maandiko hayo tuko pamoja naye, awe na moyo mkuu akaifanye. Tunachotakiwa ni kumuombea ule moyo mkuu ambao umesemwa, uwe juu yake akaifanye. Nina uhakika itafanyika vizuri na tunashukuru Mungu kwa sababu ya Dkt. Philip Mpango ambaye ameteuliwa leo, Mungu awasaidie watufikishe katika nchi ya maziwa na asali ambayo ilikuwa tamanio la Rais wetu Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na niseme ninaunga mkono hoja hizi ambazo zimetolewa hapa. Ahsante sana. (Makofi)