Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kupata fursa hii kuweza kuchangia, nitachangia maeneo machache ya dawa na bima kwa wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa dawa, tumepokea malalamiko mengi yanayohusiana na ukosefu wa dawa na tunakiri kuyapokea malalamiko hayo na sisi tunapenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba sasa Wizara imechukua mwelekeo mpya wa kihistoria wa kuboresha upatikanaji wa dawa nchi hii ili huu wimbo ukosefu wa dawa ufikie tamati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mabadiliko gani? Tumeamua kwa dhati kama wazalendo kuanza sasa kununua dawa sio kwa middle men, sio kwa washitiri yaani unaletewa dawa unanunua kwa mtu wa tano aliyenunua kutoka kiwandani. Tunakwenda kiwandani huko huko kuzinunua hizi dawa na hivi ninavyosema MSD tayari imeshapeleka order toka Novemba mwaka jana kupitia bilioni 43 zilizokuwa zimetolewa na Serikali na makontena yako bandarini yanakuja mapema Machi yanafika. Yakifika hizo dawa zitakuwa nyingi na zitasambazwa na vituo vitanunua kwa bei nafuu dawa hizo tofauti na awali. Kwa hiyo kuanzia Machi mwanzoni hapa dawa zitakuwa zimeingia nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiacha hilo, MSD imechukua mwelekeo sasa wa kuanza kutengeneza dawa kupitia viwanda vyake, imeongezea hilo jukumu na linaendelea kukamilishwa ili lianze. Hata hivyo, kuna vile viwanda ambavyo Serikali tulikuwa tuna-share ndogo, kwa mfano pale Keko, shares zimepanda mpaka asilimia 70 na tayari MSD alishazalisha dose milioni 25 za erythromycin mwaka jana Desemba na kuzisambaza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunahamasisha wawekezaji wa viwanda vya dawa nchini waache kuwekeza Ulaya maana gharama inakuwa kubwa, wanakuja kuwekeza hapa nchini kwetu. Sambamba na hilo, sisi wenyewe tumefanya mabadiliko makubwa kwenye Hospitali zetu za Kanda, Taifa pamoja na Hospitali za Mikoa zinachukua direction ya kutengeneza zile dawa na vifaatiba vidogo vidogo ambavyo viko ndani ya uwezo wetu. Yote hii ni kupunguza mzigo mkubwa wa Serikali kununua vitu hivi kutoka kwa middle men. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la vifaa. Kwenye direction hii tuliyoichukua vifaatiba vikiwemo vya dialysis vinavyotesa sana wananchi pamoja na kwamba tunaimarisha suala zima la kinga, watu wasipate magonjwa haya yasiyoambukiza, lakini gharama zitashuka kutoka 300,000 mpaka 100,000 kwa maamuzi haya ambayo tumeyachukua. Hata ule mpango wa SADC kuanza kuipa contract MSD sasa utatekelezeka vizuri. Sambamba na vifaa hivyo kutakuwepo na uwekezaji kwenye oxygen plants ili tuache kuwa tunanunua oxygen kutoka kwenye maeneo ambayo ni bei ghali sana kwa sababu tutawekeza na ku- produce hapa nchini na vifaa vya uzazi na watoto na ICU, yaani kwenye yale magonjwa ambayo ni very critical. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo kuhusu vituoni; dawa zinapotea sana, tunafanya ukaguzi wa kihistoria nchi hii. Tunaomba ushirikiano wa Wabunge na Bunge lako Tukufu. Tutachukua maamuzi ya kihostoria vile vile; kwa wale wanaodokoa dawa na kupoteza dawa sambamba na kuhujumu mapato yatokanayo na ukusanyaji wa dawa. Kwa hiyo tunapodhibiti kuanzia kwenye production, tunakuja kudhibiti kwenye matumizi, tutakuwa tumehitimisha wimbo wa upungufu wa dawa katika nchi hii na tutaulizana kwani mwanzoni ilikuwaje? Utakuwa ni wakati muafaka ambapo nchi imefunguka chini ya kiongozi wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli anayetupa ujasiri, maana vita sio wingi wa silaha, ni ule ujasiri wa kutumia silaha uende mbele. Kwa hiyo, nathibitisha kwamba suala hili linakwenda vizuri na kuanzia Machi tutegemee dawa, tamati ya ukosefu imefikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Bima ya Afya kwa wote tumelipokea kwa mikono miwili, tunakamilisha huu Muswada ambao utaingizwa huko Bungeni ili tuwe na Bima ya Afya kwa wote na hii itachangia sana kumaliza matatizo ya wananchi wetu wengi wanaoshindwa kupata huduma stahiki mahali popote. Tunapofanya haya mabadiliko yanakwenda sambamba na kusogeza hizi huduma karibu na wananchi. Kwa mfano huduma za dialysis, sasa hivi tunaanza kuongelea kwenye hospitali za mikoa, kwa sababu baadhi ya hospitali za mikoa kama kumi zimeshapelekewa mashine. Tulishindwa kuzianzisha kwa sababu ya gharama ya kuvipata hivi vifaa. Kwa hiyo kuelekea Machi tutakuwa tayari tunaanza kutoa hizo huduma kwa sababu tuna access ya dawa na vifaa kwa bei rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea mambo mengine yote, tutayafanyia kazi na kuyaleta kwenye Bunge lako Tukufu la Bajeti kipindi kinachokuja. Hivyo, naomba kuwasilisha. (Makofi)