Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa fursa hii. Kwanza nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia na kutoa maoni katika masuala yanayohusu sekta ya Kilimo. Sisi kama Wizara tunachukua sehemu kubwa na maoni yao na mabadiliko makubwa watayaona katika bajeti tutakayokuja nayo katika Bunge lijalo Mwenyezi Mungu akijalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu niweze kutoa highlight katika baadhi ya maeneo. Hatua ya kwanza, Waheshimiwa Wabunge wamechangia sana kuhusu suala la udongo, ugani na mbegu na hasa za mafuta. Kuhusu suala la ugani na suala la kupima afya ya udongo, Wizara tutakuja katika bajeti ijayo na mpango wa kuanzisha Agricultural Centre katika kila halmashauri na tutagawa katika kila Halmashauri, lab equipment ambayo ni mobile equipment itakayotumika kupima afya ya udongo na kutoa huduma ya afya ya udongo kwa wakulima bure ili kila mkulima aweze kupimiwa kipande chake cha ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni teknolojia rahisi,; kama Wizara tumeamua kuchukua hatua hii kwa sababu sasa hivi mkulima kupima afya ya udongo, kila sample inamgharimu kati ya shilingi 40,000/= mpaka shilingi 100,000/= kutokana na umbali wa eneo na maabara anayotumia. Kwa hiyo, tutatumia simple technology, lab equipment ambayo itakwenda kufanya soil analysis na soil profile na kumpatia hati mkulima kumwonyesha kwamba udongo wako huu una sifa hizi na unafaa kwa zao hili na unatakiwa kutumia hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili katika hizi Agricultural Center tutakazoweka katika kila Wilaya, tutagawa pikipiki 7,000 kwa Maafisa Ugani wa Nchi nzima katika msimu ujao na kila pikipiki tutaifunga GPS. Sasa hivi tumeanzisha ile call centre hapa Wizarani ambayo GPS hizi zitakuwa monitored from the centre kuweza kujua Afisa Ugani kama anafanya kazi katika eneo lake na tutawapatia ipad ambayo watakuwa wanajaza taarifa za call sheet za kila siku kuonesha wame-visit shamba gani na kumtembelea mkulima gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo wameongelea sana Waheshimiwa Wabunge ni suala la research and development na mbegu. Tumeamua kama Serikali suala la research and development kutegemea donor funding, halitakuwepo. Tutaanzisha Research Fund ambayo ipo kwa mujibu wa Sheria ya TARI ili kuweza ku-mobilize fund kwa ajili ya research and development. Kwa kuanza katika bajeti ijayo tutaleta mpango wa kuzalisha tani 5,000 za OPV za alizeti ili katika msimu ujao wa kilimo tuweze kuwagawia wakulima na tuweze kupata metric tonnes, 123,000 za mafuta za alizeti kutokana na input ya hii seed. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pembejeo, tumeamua kubadili mfumo na nataka niwahakikishie Wabunge tumefanya pilot kwenye pamba na tutaifanya kwenye korosho msimu ujao. Mwaka huu kwenye pamba tumewagawia wakulima mbegu bure. Tumewagawia wakulima dawa bure na gharama za dawa hizi tunazipata kutokana na mjengeko wa bei. Tutafanya hivyo hivyo kwenye korosho, tumeshatangaza tender safari hii tutagawa dawa za korosho kwa wakulima bure na tutawapatia dawa hizo na tumefanya kwa bulk procurement na hii itatupunguzia gharama na tunatarajia sulphur safari hii itapungua bei itakayoenda kwa wakulima na tuta-recover gharama kutoka kwenye mjengeko wa bei. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu zao la chai; tumeanza mchakato wa kuweka soko letu Dar es Salaam ambalo litakuwa ni kwa ajili ya kuuza zao la chai moja kwa moja, lakini vile vile Kiwanda cha Mponde nacho kitafunguliwa na mwaka huu tutasafirisha korosho zote kwa kutumia gunia za katani. Nitumie Bunge hili kumwambia mwekezaji ambaye ana viwanda viwili vya magunia cha Morogoro na Kilimanjaro tunampa kazi, akishindwa tutapeleka mapendekezo Serikalini kumnyang’anya viwanda hivi tuwape wawekezaji wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu irrigation tutatumia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda umekwisha Mheshimiwa, ahsante sana.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: … tutatumia mfumo wa force account na hii itaonekana katika Halmashauri kama tunavyojenga miradi mingine ya shule. Kwa hiyo nataka niwaambie tu Wabunge kwamba waisubiri bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mwenyezi Mungu akitujaalia. Ahsante sana. (Makofi)