Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nichukue nafasi hii kukishukuru Chama changu cha Mapinduzi na Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano. Kwanza kabisa nitamke tu kwamba naiunga mkono hoja, lakini mimi ni muumini wa uchumi wa soko na ninashukuru kwenye mpango tulioletewa sura ya tatu unaongelea ushiriki wa sekta binafsi kama chachu ya uchumi shindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kidogo nitaongelea sekta ya kilimo. Kilimo kama tunavyosema ni uti wa mgongo wa nchi hii au Taifa letu, lakini ukiangalia maendeleo ya kilimo chetu hayaoneshi kwa vitendo kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa hili, nikiangalia kwenye mpango wenyewe tumeambiwa kilimo mpaka sasa kinachangia asilimia 27 ya GDP, lakini pia kinachangia asilimia 24 ya mauzo nje ya nchi. Nikilinganisha na nchi jirani nchi nyingine ndogo ambazo ukiangalia ukubwa wa Taifa lenyewe wao kilimo kinachangia asilimia 35 ya GDP na asilimia 40 ya mauzo nje ya nchi. Tunayo kazi kubwa ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo chetu kimebubikwa na mambo mengi ambayo nadhani katika mpango huu lazima tuyapatie wajibu, mojawapo ya haya matatizo tuliyonayo Taifa letu limekumbwa limekumbwa na ugonjwa wa kanuni na tozo nyingi kwenye sekta hii, kanuni zetu zimekuwa mnyororo zimekuwa broke ya kutufanya tusonge mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya yangu ninayotoka zao kubwa tulionalo ni zao kahawa, lakini zao hilo wakulima wanalima, wanajitahidi, wanakwenda kuuza na kanuni tuliyonayo mpaka leo kwamba mkulima akishalima lazima auze kwenye vyama vya msingi/ vyama vya ushirika na anapokwenda kuuza anayo matatizo yake, lakini awezi kulipwa pesa itabidi asubiri mwezi moja, wa pili, wa tatu na wakati mwingine miezi minne, lakini wakati huo huo tunavyo viwanda vinavoongeza thamani ya kawaha.

T A A R I F A

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO:Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naongelea zao la kawaha Wilaya Muleba na Mkoa wa Kagera kwa ujumla kwamba kulingana na kanuni tulizonazo kwamba mkulima hawezi kuuza kahawa yake moja kwa moja kwa wafanyabiashara katika mkoa huo, lakini wakati Naibu Waziri wa Kilimo akijibu swali baadhi ya mazao wanaruhusiwa na pale Muleba wapo wafanyabiashara ambao wamewekeza kwenye kusindika zao la kahawa, lakini hawaruhusi kuuza kahawa hiyo moja kwa moja kwenye vile viwanda na kama tunavyofahamu kilimo na viwanda lazima tuvioanishe, matokeo yake wenye viwanda wanalazimika kununua kahawa hiyo kutoka vyama vyetu vya msingi kwa bei ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inayo madhara makubwa sana kwa uchumi, kwanza bidhaa wanayozalisha kutokana na kupata malighafi kwa bei ya juu haiwezi kushindana kwenye soko, lakini pia wakulima ambao wanauza bidhaa yao kwenye vyama vya msingi hawapati bei nzuri na wakati mwingine inawachukua muda kulipwa pesa yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni muda muafaka sasa kuruhusu wafanyabiashara ambao wamewekeza kwenye viwanda ambavyo vinasindika mazao yanayopatikanika katika maeneo mahalia badala ya kufungwa na kanuni ambazo zinazorotesha na kuumiza uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo taasisi ambazo zinashughulika na masuala ya ushindani, tuziruhusu kampuni binafsi zishindane na vyama vyetu vya ushirika na vyama vyetu vya msingi ili kuleta tija katika masoko yetu na kuhakikisha kwamba wakulima wanapata bei nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine na lamsingi na nzuri tukiwaruhusu wafanyabiashara hao kununua mazao moja kwa moja kutoka kwa wakulima ambao ni zao la kahawa, watahakikisha kwamba wanawapa pesa nzuri lakini pia wanaweza kuwafuatilia wakulima wale kuhakikisha kwamba wanazalisha na wanapatia msaada kuhakikisha kwamba mazao yao na mashamba yao yanakuwa bora muda wote na kilimo kinakuwa endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)