Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami ya kuchangia kwenye Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite kwenye vitu vitatu na vyote viko kwenye eneo la kilimo. Nitatumia lugha mchanganyiko. Eneo la kwanza ni effective utilization of labour force, post-harvest loss na productivity kwenye agriculture.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye effective utilization of labor force; ukiangalia Tanzania majority age group ni vijana ambao ndiyo tunawategemea waweze kuzalisha. Hawa vijana kama ambavyo nimechangia mchana wakati mzungumzaji alipokuwa anachangia pale walio wengi ni wale waliomaliza kidato cha nne, wengine darasa la saba na wengine wametoka vyuo vikuu. Hawa vijana kama nilivyokuwa nimegusia mwanzoni wanaposikia shughuli za kilimo, ufugaji, iwe ni kulima ni kama vile hiyo kazi ni ya watu fulani ambao sio wao wenyewe. Kwanza wanaumia, hawako tayari kwenda kufanya hizo kazi, kwa hiyo kama Taifa hatuja-harness vizuri ile nguvu ya wale vijana katika kuzalisha mali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia China, Wachina wanafanya kazi kama nyuki, angalia Vietnam, Vietnam wanafanya kazi kama nyuki, njoo Tanzania. Saa tatu kamili za asubuhi, mtu ameshatoka shambani yuko nyumbani amekula kishoka. Saa nne kamili za asubuhi tayari ameshakunywa aina ya maji, ameshaanza kuchangamka mpaka saa sita anazungumza Kiingereza. Matokeo yake kama Taifa hatujanufaika vizuri na matumizi ya nguvu za vijana katika kuzalisha ili tuweze kupata mafanikio tunayoyataka kama Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo ya haya, vision na mission tuliyonayo kama Taifa huko tunakoelekea kwa spidi, sisi tunaelekea huku, wananchi ambao ni wazalishaji tumewaacha huku. Hivyo kama Taifa nina ushauri sasa, kwenye eneo hili la matumizi sahihi ya nguvu kazi za vijana kwenye kujenga Taifa nashauri mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo la kwanza, vileo vipigwe marufuku kuuzwa na kunywewa mida ya kazi. Ni rahisi sana, kama Mheshimiwa Waziri Mkuu alisimama akakataza viroba na vikapotea, vivyo hivyo katazo linaweza likatolewa wananchi wakabaki wanakunywa muda wa weekend.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo la pili, nashauri turejeshe mfumo wa kufundisha vijana wetu uzalishaji wakiwa shuleni, nenda sekondari, ukienda sekondari mwanafunzi anasoma kuanzia form one hadi kidato cha sita hajawahi ku-practise ufugaji wala kilimo. Naishauri Serikali kwenye Mpango huu unaokuja wa miaka mitano turejeshe haya mashamba darasa kwenye shule zetu. Hawa ambao wameshamaliza muda wao umepita tuwaache, lakini hawa ambao wako kwenye shule zetu tuwafundishe kulima na tuwafundishe ufugaji. Wale watakaobahatika kuendelea na Vyuo Vikuu, wataendelea. Wale ambao hawatabahatika waweze kuona hizi shughuli za kilimo kama sehemu ya ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nihamie upande wa kuongeza uzalishaji (increasing productivity). Tanzania tumebahatika kuwa na mito, mabonde na ardhi nzuri yenye rutuba. Eneo linalolimwa ni dogo, mkuu wa kaya ambaye mara nyingi ni baba, unakuta kwenye kaya zetu ukienda vijijini hata hapa Dodoma mtu amelima nusu eka, amelima eka moja, ana vimbuzi viwili nyumbani, akiongeza na ng’ombe watatu amemaliza, watu wameridhika. Hii kasi tuliyonayo sisi kama Serikali kwamba watu tufanye kazi people are relaxing, hawana haraka, ameridhika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, kupitia mifumo iliyopo ya kuhudumia na kusimamia maendeleo tutoe maelekezo. Tutoe target kwa kila mkoa, wilaya na kijiji, ili familia zote za vijijini ziweze kuzalisha. Badala ya kulima eka moja au mbili ziweze kuwa eka nyingi ili nguvu ya Serikali inayoenda kuwekezwa kwenye kilimo iweze kuonekana ndani ya kipindi cha miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la post harvest loss sijaweza kulizungumzia, ila niseme tu kwamba naunga mkono hoja. Ahsanteni sana. (Makofi)