Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikupongeze wewe kwa kazi nzuri na namna ambavyo unaliongoza Bunge hili Tukufu. Pia nimpongeze Mheshimiwa Jenista Mhagama kwa vile ambavyo anasimamia Kanuni hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi imara wa Mheshimiwa wetu, Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo ameweza kufanikiwa kuingia katika uchumi wa kati kabla ya kipindi kilichokuwa kimetazamiwa. Kwa namna ambavyo tumeweza kuingia kwenye uchumi wa kati Benki ya Dunia wameshangazwa na kasi ya Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, naomba kuishauri Serikali iendelee kuweka mkazo kwenye Halmashauri zetu ili ziweze kuwekewa fedha za kutolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili wawe kuendesha maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kufanikiwa zaidi kwa namna ya kuendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais kwenye uchumi wetu wa kati, ili kasi iendelee kuhusiana na namna ya kutoza kodi kwa wafanyabiashara, naomba elimu kwa upande wa wafanyabiashara imekuwa ni ndogo. Kipindi cha nyuma mfanyabiashara anapokuwa anafanya biashara mfanyakazi wa TRA alikuwa ni rafiki wa mfanyabiashara lakini sasa hivi hali imekuwa siyo, wafanyabiashara wamekuwa wakilalamika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo napenda kuishauri Serikali kuanzia elimu ya msingi, sekondari na vyuo ikiwezekana kuwe na elimu kuhusu kodi kwa maana Mtanzania yeyote pindi anamaliza chuo asijute kwamba anaonewa namna ya kutoa kodi aone ni uzalendo kutoa kodi kwa maana ya kuendesha nchi yetu. Maana nchi inaendeshwa kwa kulipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa Watanzania wanaelewa vizuri sana kazi ambayo ameifanya Mheshimiwa Rais wetu ya kuijenga nchi yetu ya Tanzania. Mheshimiwa Rais wetu baada ya kuchaguliwa 2015 ndani ya siku mia moja alipongezwa kwelikweli hata wananchi mbalimbali wengine walisema Mheshimiwa Rais akae miaka 100, wengine walisema miaka 40, kila mtu aliongea la kwake kwa namna ambavyo amekuwa akiendesha nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kusema kwamba Mheshimiwa Rais ameweka nidhamu Serikali lakini ameweka nidhamu mpaka kwenye ndoa za Watanzania. Naongea hivyo kipindi cha nyuma watu walikuwa wakilalamika sana baba anarudi nyumbani usiku wa manane, mama anarudi nyumbani muda atakao akilalamika kwamba kuna foleni kubwa. Baada ya kuingia Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kama Rais, baba na mama wanawahi nyumbani kupanga mipango ya maendeleo ya familia zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hayo miaka ya nyuma mara nyingi sana tulikuwa tukiwashuhudia hawa watu wa Kilimanjaro ikifika Disemba wanarudi nyumbani kwao, kwetu haikuwa hivyo. Hata hivyo, baada ya kuingia Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli sasa hivi wazazi wanafurahia watoto wao, watoto wao walikuwa hawaonekani mikoani mwingine anakuwa hajaenda hata miaka mitano, mitatu mpaka kumi lakini sasa hivi ikifika Disemba magari yanapishana huko mikoani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana sana Watanzania tumuelewe Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Watu wanasema pesa haziko mifukoni lakini maendeleo yamekuwa ni makubwa, ukipita mitaani huko barabarani unaona jinsi wananchi wanavyojenga nyumba tena wanaezeka mabati ya m-South au tunapenda kuita mabati ya rangi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuendelee kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi nzuri anazoifanya. Ahsante sana. (Makofi)