Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme elimu kwanza iwe ya darasani au mitaani. Kama Serikali ingekuwa makini katika vipaumbele vya nchi elimu ingewekwa ya kwanza nchini ili kupata matokeo makubwa. Hivi bila elimu hata mimi nisingeweza kuchangia, Daktari, Mbunge, Waziri, Rais, Mwalimu, viongozi na wataalum wote wasingekuwepo. Sasa kwa nini Serikali inafanya mzaha katika suala la elimu? Jamani tusione aibu, tuseme tulikosea sasa tushirikishe wadau tuanze upya ni kweli tumejikwaa na kujikwaa si kuanguka, bado hatujaanguka tujipange.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na matatizo mengi ya walimu nchini lakini naomba nizungumzie matatizo yanayowapata walimu katika Jimbo la Mlimba, pia miundombinu ya shule, upungufu wa walimu na elimu ya awali pia watoto walemavu wanaoishi katika Jimbo la Mlimba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shule za sekondari kata changamoto ziko tofauti, kuna uwekaji wa umeme wa jua ambako REA haifiki katika shule za sekondari za Kiburubutu, Uchindile, Matundu Hill na Mofu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ununuzi wa samani (meza na stuli) za maabara kwa shule zote za Serikali zilizoko katika Jimbo la Mlimba ambazo ni Masagati, Utegule, Mutenga, Kamwene, Mlimba, Tree farms, Chisano, Chita, Mchombe, Kiburubutu, Nakangutu, Mbigu, Mofu na Matundu Hill. Pia ujenzi wa hosteli shule za sekondari za Chisano na Matundu Hill.
Aidha, kuna uhitaji wa madarasa 1,166 yaliyopo 467 hivyo hakuna madarasa 699; nyumba zinahitajika 1,036, zilizopo ni 199, hakuna nyumba 837; vyoo mahitaji ni 897, vilivyopo 290 hakuna vyoo 607
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nitawasilisha hali halisi ya hali ya elimu Jimbo la Mlimba.
Mheshimiewa Mwenyekiti, Jimbo la Mlimba kuna kituo kimoja tu cha ufundi kilichopo Mchombe. Kituo hicho cha ufundi stadi kina changamoto ya uchakavu wa madarasa ya nadharia na vitendo, upungufu wa zana na vifaa vya kufanyia kazi katika fani zote za useremala, uashi, chuma na sayansi kimu pia walimu. Hivyo naomba ukiangalie kwa jicho la pekee kituo hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hali ya shule za awali na msingi ni duni sana, hali ya walimu ndio kabisa, nyumba za walimu ndio usiseme, ukizingatia ni Jimbo la vijijini na miundombinu ya barabara ni mbaya hivyo wanahitaji kuwezeshwa usafiri angalau wa pikipiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni matumaini yangu kuwa utalipa kipaumbele Jimbo la Mlimba kwa kuwapelekea walimu wa shule za sekondari na msingi katika ajira zijazo. Mahitaji sahihi nitakupatia, ahsante.