Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. KABULA E. SHITOBELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii ya kuchangia katika Mpango huu wa Maendeleo ya Taifa. Pia napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema zake kwa kunijaalia afya njema hata nimesimama katika Bunge hili na kuchangia hoja hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma Mapendekezo ya Mpango ni mazuri sana na yana faida kubwa kwa Watanzania wote. Nami nitajikita zaidi katika hoja ya kukuza na kuchangia uchumi wetu kupitia zao la parachichi. Nina- declare interest nami ni mdau katika biashara ya parachichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ya parachichi ni kubwa sana na ni zao ambalo linaweza kutuletea kipato kikubwa hasa kutuletea pesa nyingi za kigeni kama tukilizingatia na kama Serikali hii itaweza kuliona ni zao bora kabisa la biashara kama mazao mengine kama korosho, pamba au kahawa. Zao hili likisimamiwa vizuri linaweza kutukuzia uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao hili limekuwa likilimwa na wakulima wadogo wadogo lakini kama likiwekewa mkakati, likatangazwa na wananchi wote wakahimizwa hasa wa Mikoa ya Njombe, Kilolo (Iringa) na Mbeya (Tukuyu) ambapo zao hili linapatikana kwa wingi na ni zao bora kabisa tutaweza kukuza uchumi wa Taifa. Zao hili mpaka sasa limeajiri wanawake wengi sana katika viwanda vya ku- process wakati matunda haya yakipelekwa nje ya nchi. Wanawake wengi ndiyo wanatumika ku-process zao lile mpaka kusafirishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijikite kuzungumzia changamoto ya zao hili. Kama mimi nikiwa mdau nimeweza kuona changamoto mbalimbali hasa kwenye kusafirisha tunda hili. Matatizo yenyewe ni jinsi ya kusafirisha mazao haya kutoka Njombe kwenda nchi kama Europe kwa sababu zao hili linauzika zaidi Europe pia Middle East hapa Dubai na Arabuni yote kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo kwa sasa ni usafiri hasa kwenye kontena aina ya CL. Kwa Tanzania katika bandari yetu ya Dar es Salaam hakuna kontena kama hizo, inabidi mfanyabiashara wa zao hili aweke booking Nairobi, kontena litoke Mombasa lije mpaka Njombe, likifika Njombe ndiyo upakie ule mzigo urudi tena Mombasa ndiyo uweze kuondoka. Sasa tatizo linakuja wapi? Pale inapotokea tatizo lolote au delay yoyote njiani na mkulima au mfanyabiashara anakuwa ameshachukua matunda yako pale kwenye park house, sasa inapochelewa labda siku moja au siku mbili yale matunda yakija kusafirishwa kufika sehemu husika tayari yanakuwa ni reject. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu Tukufu iangalie jinsi gani itatusaidia au itawasaidia wakulima na wafanyabiashara wa zao hili kuhakikisha kuna zile kontena za CL au facility za usafiri madhubuti pale Dar es Salaam ili at least mkulima tunda linaposafirishwa kufika kule Ulaya liwe katika hadhi na ubora wa Kimataifa. Ombi langu sasa kwa Serikali ni kuangalia hivyo vitu muhimu hasa upande wa makontena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ningeomba zao hili lihamasishwe sehemu mbalimbali, najua hata Bukoba au Ngara linakubali kabisa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa, kengele imeshagonga. (Makofi)