Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Mpango wa Miaka Mitatu wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunafahamu kwamba Serikali yetu imewekeza kwa kiwango kikubwa katika upanuzi wa bandari zetu. Nafikiri ni maono makubwa pia ya Rais wetu kuboresha bandari zetu kwa sababu amepanua barabara ya Morogoro lakini pia amejenga na reli, yote haya ni ili kuleta ufanisi katika biashara ya bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba Serikali iweke mpango kuhakikisha ina-enforce law ili basi ile slow moving traffic katika barabara ya Morogoro na fast moving traffic zisiweze kuchanganyika pamoja ili intended use ya zile fly overs ambazo zimetengenezwa ziweze kuleta maana katika Taifa letu. Ndugu zetu wanaotumia maguta, mikokoteni ni muhimu kwa Taifa letu pia lakini haileti mantiki tuweze kutengeneza fly over ili fast moving traffic zikimbie halafu unavuka unashuka chini unakutana na guta na mkokoteni. Naomba sheria na taratibu nzuri ziwekwe ili kuhakikisha kwamba watumiaji hawa wanatafuta namna ya kufikisha mizigo yao sokoni Kariakoo lakini sio kwa kutumia barabara ile iliyopanuliwa na inayotaka mgari yaende haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie pia kwenye suala zima la parking lots. Serikali imekuwa ikikusanya mapato kwa maana ya parking fees katika mitaa yetu wakati zile barabara zimetengenezwa kwa upana ule kwa sababu maalum. Leo sehemu ya barabara inatumika kama parking lots, hii inakwenda kinyume na matumizi halisi ya barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali iweke mpango na kwa kuwa sasa tunakwenda kuwa na adequate public transport, tunazo DART lakini tutakuwa na treni za mjini, Serikali iweke Mpango wa kutengenza parking kule ambapo DART inaanzia ili mtu anapotoka nyumbani kwake aweze ku-park gari yake sehemu salama na aingie katikati ya Majiji yetu bila ku-congest majiji yetu kuliko kutumia maeneo ya barabara. Hii inakwenda against na mipango halisi ya ku-design barabara zile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba kuchangia maana halisi ya DART (Dar es Salaam Rapid Transit) au DORT (Dodoma Rapid Transit), mana halisi ni kuhakikisha kwamba katika kila kituo chetu cha mwendokasi kunakuwa na schedule ya kupita kwa magari yale. Kwa maana kwamba labda gari ya kwanza itaanza saa 11, nyingine itakuwa saa 11:10 ndiyo maana ya Rapid Transit. Kama hatuwezi kuweka hizo schedule zikafahamika Rapid Transit hazitakuwa na maana, zitakuwa sawasawa na daladala zetu tu, hamna tofauti. Kwa hiyo, niiombe Serikali iweke Mpango wa kuhakikisha kwamba hizi tunazoziita Rapid Transit zinafika kwenye kituo kwa interval ambazo zitakuwa known kwa wananchi ili nao waweze kutoka katika nyumba zao na waweze kutumia usafiri bila kukaa muda mrefu katika vituo vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanua bandari zetu na imepanua pia bandari ya Tanga lakini kiukweli TRA wanachangia kuhakikisha bandari ambazo ziko nje ya Dar es Salaam hazipati wateja kwa sababu tax clearance inachelewa. Dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu ni Mbunge wa Tanga Mjini amekuwa aki-hustle kutafuta wateja watumie Bandari ya Tanga baada ya kuwa imeshaongezwa kina chake lakini unfortunately wateja wanakimbilia Bandari ya Dar es Salaam kwa sababu tax clearance inachelewa bandari za mikoani.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Kengele imeshagonga Mheshimiwa, ahsante sana.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)