Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kushukuru kwa nafasi hii uliyonipatia. Napenda pia kukishukuru Chama changu cha Mapinduzi na UWT kwa Mkoa mzima wa Shinyanga kwa kuniteua kuwa mwakilishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ushindi wa kimbunga alioupata kwa mwaka huu. Ilikuwa si kazi rahisi lakini kwa matendo makubwa aliyoyafanya ameweza kushinda na wananchi wakaweza kumwamini na kumpa nafasi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia jinsi Serikali inapaswa katika mpango mpya huu wa kutengeneza ajira milioni nane na uchumi wetu uweze kupanda kwa asilimia nane. Serikali imejikita sana kwa wafanyabiashara ambao kwa sasa hivi tukiangalia kwa hali halisi wako ICU, ukiangalia tunawanyonya sana na wakati tuna lengo kubwa la kutengeneza hizi ajira milioni nane ili kufikia asilimia nane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza, naishauri Serikali iwawezeshe vijana na wanawake kwa kuwapa mitaji ya kutosha kwa sababu hii ndiyo nguvu kazi tuliyonayo. Hawa vijana wakitengenezewa ajira upya, NEMC wakitoa masharti ambayo ni nafuu, nina uhakika kila nyumba ina uwezo wa kuwa na viwanda vidogovidogo vya kuchakata vitu mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwa Mkoa wangu wa Shinyanga kuna vijana wadogo tu wenye miaka 25 wanatengeneza chaki, kuna kina mama wa kawaida tu wamekopeshwa na Halmashauri matrekta makubwa ya kufanyia kazi, mitaji ya milioni 50 wanafanya kazi vizuri. Mheshimiwa Rais aliongelea katika page ya 11 kwamba hii mifuko ya ukopeshaji ikichanganywa na kuwa pamoja itawezesha Halmashauri kutoa kiasi cha pesa cha kutosha. Kwa sasa hivi, hela zimegawanywa katika mifuko mbalimbali, kwa hiyo inafanya kwamba hata zile hela zilizokuwepo kwenye Halmashauri hazitoshi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kama Serikali inaweza ikafuatisha maoni ya Mheshimiwa Rais, hii mifuko ikawa mmoja itasaidia kwa kiasi kikubwa, itaongeza zile asilimia kumi za Halmashauri, itaenda kama ku-boost. Katika zile Halmashauri, wataangalia Serikali ina Halmashauri ngapi watazigawanya kama ni kwa pro rata au kwa ratio ya mikoa au kwa ratio ya wananchi ambao wako katika eneo lile ambao ni wanawake, vijana na walemavu. Hawa wakipewa mitaji ya kutosha watasaidia kui-boost hii ajira kwa kila mtu na tutakuwa tumepata ajira milioni nane na mapato ya nchi yataongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali hizi certificate zinazotolewa na Halmashauri ziweze kutumika kama dhamana, watu wanateseka sana kwenye dhamana. Kama Serikali inatoa hizi certicate katika Halmashauri ni wakati sasa hizi certicate hata benki wazikubali kwa sababu Halmshauri inazikubali kwa wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuwapa mikopo. Ni wakati na benki nazo iviamini hivi vikundi watumie zile certificate kuwapa mikopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba kwa huu Mpango mwingine wa miaka mitano, asilimia za mikopo ya wanawake itoke kwenye asilimia 4 iende kwenye asilimia 7. Ninyi mtaona kwa namna ya pekee wanawake tukiwezeshwa tunaweza. Hata kwenye kura mnatutumia sisi, mnatuita wanawake ni jeshi kubwa lakini wanawake sisi ni jeshi mmetupa asilimia 4, sisi wanawake ndiyo tunaokaa katika jamii tunailinda. Kwa hiyo, naamini kwamba tukitoka kwenye asilimia 4 tukapewa asilimia 7 tuta-boost ajira nyingi za wanawake na mapato ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba Serikali ipokee mchango wangu na naunga mkono hoja na naomba Serikali iunganishe ile mifuko iwe sehemu moja. Ahsante sana. (Makofi)