Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uweza wa kusimama hapa. Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sikumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyojipambanua kwamba yeye maendeleo kwake hayana itikadi za kivyama. Kama angefuata itikadi za vyama maendeleo tunayoyasema Dar es Salaam yasingekuwepo. Dar es Salaam tunajua fika ilikuwa ni ngome ya wapinzani lakini amefanya maendeleo ya barabara, maji, elimu iliyopelekea wananchi wa Dar es Salaam sasa nao kumlipa fadhila ya kuifanya Dar es Saalaam ya kijani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru na nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mpango, amekuja na Mpango kwelikweli kama jina lake. Hata hivyo, Mpango huu wanaohusika ni wataalam wake ambao ni rasilimali watu. Mimi nijikite kwenye rasilimali watu. Haya yote tunayoongea humu, yote tunayojadili humu, wanaoenda kuyatekeleza ni rasilimali watu, ni watumishi wetu, lakini kuna sehemu hawa watumishi hawatoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Waheshimiwa Wabunge wamesema kuhusu kilimo, lakini ukiangalia nchi ina shortage ya Maafisa Ugani 6,000 badala ya 12,000. Sasa hawa 6,000 hawawezi kutumika kwa nchi kumfikia kila mkulima, suala hili tuliangalie kwa makini. Hata hao waliopo vitendea kazi walivyonavyo ni vichache sana. Tumesikia kuna Kata zina vijiji 15, lakini Afisa Ugani huyu hata baiskeli hana, atamfikiaje huyu mkulima? Kama kweli tunataka kilimo kiwe ni uti wa mgongo, tuwaangalie hawa Maafisa Wagani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajivunia GePG ambapo mtandao uliotengenezwa na watumishi wetu wa Serikali. Hii ni software tungekuwa tunainunua kwa wataalam wengine ingetumia bilioni za fedha. Kwa hiyo, tuwaendeleze hawa watumishi wetu kielimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi imefikia wakati watumishi wanaogopa kwenda kusoma kwa sababu ya nyaraka zinazotoka utumishi. Mtumishi sasa hivi akienda kusoma, anaambiwa muda wake alioenda shule hautahesabiwa kwenye promotion yake. Sasa tunaenda kuzalisha wale walioenda kusoma na aliyebaki akaendelea na ule muundo anakuwa mwandamizi, yule aliyetoka na elimu yake anakuwa junior kwake. Sasa hii inapunguza utendaji kazi ndani ya Serikali. Huyu mwenye elimu kubwa angemshauri huyu lakini sasa huyu ni mwandamizi kwake, atamshaurije na huyu ni senior wake? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Utumishi niwaombe, tuangalie hizi nyaraka. Kuna sheria za kiutumishi, lakini nyaraka ndani ya sheria za kiutumishi zimekuwa nyingi mno, zinaleta mkanganyiko. Sasa hivi mtumishi ukimwambia nenda kasome ataleta sababu zisizo na msingi, lakini ukimfikia kwa karibu anakwambia ngoja kwanza nipande kwenye huu muundo nifikie daraja la uandamizi ndiyo nitaenda kusoma lakini sasa wanadumaa na utaalam unabadilika kila wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kuiangalia hii miundo, tutabaki tunawalaumu wataalam hawafanyi kazi lakini kumbe kuna kitu kimewakwamisha. Naomba tuliangalie hili kwa umakini. Tuna vijana ambao ni wazalendo wa kweli. Mfano ni hii Wizara ya Fedha ambayo imekuja na huu Mpango, wanakesha, wanaumiza vichwa kuja na Mpango kama huu, lakini sasa miundo inawakamata. Tuliangalie suala hili na kama tunataka nchi hii iendelee, tuwekeze kwenye rasilimali watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais ana utashi kabisa wa kuwekeza kwenye rasilimali watu. Ukiangalia Ilani ya Uchaguzi imesema hivyo; ukiangalia hotuba yake hapa imesema hivyo; Mpango umekuja unasema hivyo, lakini je, tunatekeleza sisi tunaomsaidia? Nizidi kuiomba Menejimenti ya Utumishi wa Umma, hebu angalieni nyaraka zenu za kiutumishi, zimekwamisha kabisa haya maendeleo na huu Mpango wanaoenda kuutekeleza ni rasilimali watu hii hii. Tukiyafanya hayo, Tanzania inaenda kubadilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)