Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukua fursa hii kuwapongeza viongozi wote wa Wizara kwa juhudi kubwa za kuendeleza elimu kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chama cha Walimu Tanzania, CWT ishauriwe kupunguza mchango kwa Walimu au kuondoa kabisa. Pia michango waliochangisha waoneshe ni kwa namna gani imewasaidia walimu ili walimu wanufaike na michango yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bodi ipange mpango mkakati wa kufuatilia wanafunzi ambao wamepata ajira au kujiajiri lakini mpaka sasa hawajarejesha mikopo ili fedha hizo zisaidie kuongeza idadi ya wanafunzi kukopeshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti,, wanafunzi wa kike waliopata bahati mbaya ya ujauzito nashauri Wizara iwaruhusu kuendelea na masomo baada ya kujifungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara isaidie ujenzi wa mabweni ya wasichana katika maeneo ya vijijini ili kuwanusru wasichana wetu wadogo.