Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru wewe; lakini pia niishukuru familia yangu; tatu nishukuru wananchi wa Jimbo langu la Lulindi walioniamini; nne nishukuru Chama Cha Mapinduzi kwa kuniamini kuwa naweza kufanya hizi kazi kwa ufanisi mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nataka nizungumzie suala la performance; nataka nijaribu kuweka wazi katika jambo hili. Wakati unapotaka kuchunguza performance ya mtu au kitu, cha msingi sana kinachohitajika kutumika pale sio percentage term, unatakiwa utumie an absolute term, maana yangu ni nini? Ni kwamba ukichukua bilioni moja ukazidisha kwa asilimia 10 unapata milioni 100, lakini ukichukua milioni 100 ukazidisha kwa asilimia 27 au asilimia 30 unapata milioni 30. Kwa hiyo, ukisema kwamba eti kwa sababu umetumia percentage kubwa wewe ume- perform, huo ni upotoshaji mkubwa, kwa hiyo nataka nieleweke hapo kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niende katika utendaji wa Serikali. Hakuna hata mtu mmoja ambaye anasema kwa dhati kabisa kwamba, eti Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli hakufanya vizuri kwa dhati kutoka rohoni kwake, atakuwa anatania tu. Kiuhalisia yaliyofanywa ni mengi sana, hatuwezi kuyamaliza hata tukisimulia wiki nzima maajabu hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kwamba suala la maendeleo ni mtambuka. Tunahitaji kuhusisha vitu vingi na sekta mbalimbali kwa ajili ya kutengeneza hayo maendeleo. Barabara za Dar-es-Salaam za mwendokasi, ni jambo zuri sana, lakini nashauri barabara hizi zizingatie pia na ukuaji wa miji ile. Nashauri kwamba barabara hizi ikiwezekana zifike hata Mkuranga kwa ajili ya ku-accommodate watu wanaoishi maeneo kama ya Mbagala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mradi wa bandari Mtwara umetumia pesa nyingi sana, takribani shilingi bilioni
157. Naomba mradi huu uunganishwe haraka sana na reli ya Standard Gauge ambayo itafika kwenye miradi mikakati ya Mchuchuma na Liganga. Tusiendelee tu kuongea mdomoni, tufanye kwa vitendo kama kweli tunataka maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine mradi huu pia uunganishwe na barabara zote za kimkakati zikiwepo barabara zile za ulinzi. Kwa mfano, barabara inayotoka Mtwara – Mtawanya - Mpilipili – Chikoropola - Nanyumbu. Barabara hii nafikiri ni muhimu sana kwa ku-boost maendeleo ya watu wa Kusini na viwanda vya Kusini, hasa kiwanda cha korosho ambacho nakitegemea mimi kama mmoja wa wahamasishaji kipatikane kule lakini kiwe ni kiwanda kikubwa kabisa cha kushawishi watu wengi sana kuuza pale, kusudi tuweze kupata bei nzuri. Hali ilivyo sasa hivi hatuwezi kupata bei nzuri kwa sababu tunauza raw material. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda EPZ iwe ndio msingi wa maendeleo kwa sababu ndiyo inaweza ikasababisha watu wengine wakawekeza kikamilifu. (Makofi)

(Hapa Kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mengi, lakini niseme naunga mkono hoja kwa sababu yaliyo ndani ya Mpango ni mazuri. Nakushukuru. (Makofi)