Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa na hali ya uzima na afya wakati huu. Pia nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kunirejesha tena kwa mara ya pili katika Bunge lako hili Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nikupongeze wewe maana kipindi kile tulikuwa pamoja tumefanya kazi pamoja, pamoja na Mheshimiwa Spika, lakini pia nimpongeze na Rais wangu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuniteua na kuniamini na kunirejesha tena katika Bunge hili Tukufu. Kwa kweli tushukuru Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ni mfupi, tuna mengi ya kusema, lakini tutapopata ndio tumefanikisha. Mpango huu umefika kwa wakati muafaka na Mpango huu mambo yake mengi yaliyokuwamo humu yamejikita pamoja na hotuba ya Mheshimiwa Rais, yameendana pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kuchangia kuhusu Mpango huu, kwanza huu Mpango nataka kusema umefika wakati muafaka na hili suala langu ambalo ninalolitaka kulisema hapa hivi sasa na suala hili la muda mrefu na suala hili linanikereketa, nikienda nikirudi bado lipo ndani ya nafsi yangu, lakini hivi sasa hivi nataka kulitoa katika Mpango ambao uliofika hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia kuhusu sehemu ya Muungano, sehemu ya Muungano kuna magereza ya Zanzibar pamoja na magereza ya Bara. Magereza ya Zanzibar na magereza ya Bara, magereza ya Bara yanafanya kazi kwa wakati wake na magereza ya Zanzibar yanafanya kazi kwa wakati wake. Naomba kwa Mpango huu ili kuunganisha huu Muungano wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, je, haiwezekani magereza haya yakaweza kuunganishwa, ikawa kitu kimoja kama ilivyo Polisi na Jeshi? Hilo lilikuwa linanikereketa na leo hii limefika mahali pake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kusema kuhusu suala la afya; suala la afya na wagonjwa na sukari, shinikizo la damu pamoja na pressure. Magonjwa haya yametawala nchini, yako mengi, haya magonjwa hayaambukizi, lakini ni magonjwa sugu, yanaumiza na wala hayana dawa. Maana kuna wenzetu ambao wamepata maradhi haya wanyonge, maskini, hawana kipato cha kuweza kujiwezesha ili kujitibu magonjwa hasa shinikizo la damu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa una sukari, ukiambiwa usile hiki, usile hiki unaweza ukapona, ukaifuata miiko yake, lakini shinikizo la damu gumu. Kwa hiyo naomba Mpango huu pamoja na Serikali yangu iweze kuwaona wagonjwa hawa wa sukari, pressure pamoja na shinikizo la damu ili wawezeshwe wapate dawa za kuweza kujitibu ili waendelee na wao kufanya kazi zao kama tunavyozifanya hivi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu Chuo cha Hombolo; hiki chuo kizuri nilikwenda nikakitembelea, kizuri sana na kina mambo yote ya sayansi na teknolojia. Hata hivyo, hiki chuo kiko mbali. Sasa umbali wake ni nini? Ni kuhusu barabara ya kuendea Hombolo kwani ni mbovu, chafu, haifai. Naomba barabara ya Hombolo kwa Mpango, Mwenyezi Mungu akatujalia, basi barabara ile mwaka huu iwezeshwe, itengenezwe ili watoto na siye tuweze kuwapeleka kule ili waweze kwenda kusoma katika kile Chuo cha Hombolo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie pia kuhusu suala la ukosefu wa nyumba za askari; ukosefu wa nyumba za askari ni mkubwa hasa kwa Mkoa wetu wa Kusini, Mkoa wetu wa Kusini una wilaya mbili, Wilaya ya Kati na Wilaya ya Kusini, lakini Wilaya ya Kusini ni mkoa bora, ni mkoa mama ambao unaweza kuchukua watalii wakawa wanakwenda kutalii katika wilaya ile, lakini nyumba za askari hakuna na wala hawana mahali pa kukaa, wanahangaika hangaika isipokuwa kituo kidogo kipo Paje, pale kidogo lakini Jambiani hakuna Kituo cha Polisi, naomba napo kiende kikajengwe kituo cha polisi…

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Kengele imeshagonga.

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: …ili na wao waweze kujisikia. Ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)