Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuchangia katika Mpango huu wa Tatu wa Maendeleo lakini pia nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii. Kwanza kabisa, nimpongeze Rais kwa usimamizi mzuri wa miaka mitano hii kwa ambacho kimefanyika, ni very impressive. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nataka nijikite kwenye suala la mchango wa sekta binafsi. Nimejaribu kupitia hapa Mpango, naona sekta binafsi tunategemea ichangie almost 40.6 trillion shillings na nikafanya average kwa mwaka ni 8.12 trillion, huo sio mchango mdogo sana kwa sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu ambacho nimekuwa najiuliza, nimekaa sekta binafsi kwa muda mrefu, labda kwa upande mwingine ningeomba Serikali pia ihusike kwenye ku-support sekta binafsi. Kwa nini nasema hivi? Ni kwa sababu unapoiweka sekta binafsi kwenye Mpango halafu huishirikishi mipango kidogo inakuwa gumu maana tunawaacha wanakuwa separate halafu baadaye tunaenda kukamua maziwa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nayasema haya? Sasa hivi nimetoka kwenye Kamati tulikuwa na semina nikajaribu kuuliza swali kwa watu wa TANTRADE kwamba nyie kazi yenu kwa sehemu kubwa ni kuhakikisha mnatafuta masoko na mnashauri. How many times mmechukua muda wa kwenda kushauri sekta binafsi, maana nitaenda nitamkuta Mheshimiwa Musukuma na biashara yake ya mabasi naanza kuchukua kodi pale, lakini Mheshimiwa Musukuma amekuwa anaongea humu anasema darasa la saba ndiyo matajiri au ndiyo mabilionea tunaweza kuona kama anafurahisha lakini reality ipo kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kitu kimoja kifanyike, ni lazima Serikali ijikite kwenye kuhakikisha tunashirikisha sekta binafsi kwenye mipango yetu, maana wapo matajiri au wafanyabiashara ambao leo hawajui hata Ilani ya CCM inalenga nini lakini wapo kule. Wale watu wanakopesheka kwenye mabenki na wana uzoefu wa biashara, kwa hiyo, tukiwatumia vizuri wanaweza wakatusaidia kwenye kukuza uchumi. Maana hapa basically tunachojaribu kukiangalia ni nini? Tunajaribu kuangalia possibility ya ku-raise pesa kutoka sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ambacho nashauri ni kitu kimoja, tuangalie Serikali iweze kuwatafuta hawa watu, tusiwatafute kwenye makundi maana wafanyabiashara wa Tanzania kwa sehemu kubwa kila mmoja anaficha mambo yake, hakuna mtu ambaye yuko tayari kufunguka. Ukiita semina ya wafanyabiashara hapa hakuna ambaye yupo tayari kufunguka, lakini tukijaribu ku-identify labda wafanyabiashara kumi potential, tukaangalia huyu mtu uwezo wake ni mkubwa katika industry fulani na bado benki anaweza akakopesheka. Huku mfanyabiashara kupata bilioni 300, bilioni 400 benki unampelekea idea ya biashara maana tunahangaika na viwanda hapa, kuna mwingine yupo kwenye mabasi lakini anaweza akajenga viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafute kupitia TANTRADE, iende imshauri, tuwatembelee hawa watu tusikutane nao tu wakati tunatafuta kodi maana haya mambo hata kwenye halmashauri zetu huko yaani Afisa Biashara ni kama Polisi, yeye atatembelea duka lako, atatembelea sehemu yako ya biashara anakagua leseni au anakagua vitu vingine. Wapate muda wa kuwatembelea watu hawa, ujue huyu mtu ana shida gani, sometimes mtoe hata out maana private ukijaribu kuangalia wanaotu-train private aliongea mtu mmoja aliyekuwa anachangia asubuhi, kwamba investment hata kwenye Makampuni ya Simu na Serikalini huku ni tofauti, yaani unayemweka am-audit mtu wa private, mtu wa private anajua zaidi kwa sababu wale watu wame-invest hela nyingi Zaidi, sisi tumekuwa tunasafirishwa tufanye kazi private, tunasafirishwa sana na makampuni nje, sio kusema yule mtu hakusafirishi tu bila manufaa, anataka uelewe ili kurudi umfanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hali kadhalika hata watumishi wetu umma watafute muda wa kukaa na watu wa private, wawaulize matatizo yao ni nini. Wawatembelee hata ofisini, wawatoe hata out jioni wakae sehemu waongee hizi bajeti ziwepo, maana hawa watu washirika, mtu wa kukuchangia trilioni 40 kwa miaka mitano huwezi tu kuwa unakuta naye kwenye tax collection, hapana lazima tuwatafute tushirikiane nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limekuwepo, watu wengi sana wameongelea habari ya TRA, niombe Serikali. Nimekuwa kwenye biashara, tunafanya kazi na Serikali, una-supply mzigo au contractor anafanya kazi, baada ya hapo kuna raise certificate, ipelekwe wizarani, baadaye iombewe hela hazina ije ilipwe, inachukua almost miezi miwili au miezi mitatu ndio hela inakuja. Hela inafika kuna maelekezo sasa hivi kwamba kabla ya kumlipa mkandarasi au supplier yoyote yule, uanze kwanza kuwauliza TRA kwamba huyu mtu anadaiwa. Sasa hata yule niliyefanya naye biashara taasisi ya umma naye amegeuka tax collector, leo hanilipi hela yangu kwamba kama nadaiwa ile hela anaihamisha moja kwa moja inaenda TRA. Jamani nafanya kazi na wewe, ni mfanyabiashara unajua ofisi yangu, nilipe kwanza maana sisi tunakopa kwenye mabenki, hawa ndio partners, sasa leo ukichukua bilioni yote na mtu wa TRA anakwambia unadaiwa, sometimes anakwambia ile ilipe kwanza, ikishalipwa kwanza tutakuja tuta-negotiate, hela haiwezi kuingia kule ikarudi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninachoomba, TRA wasiwe Polisi, hawa ni partners, ni watu wa kufanya nao biashara, tuwashirikishe lakini tushirikiane nao maana wako registered, kila mfanyabiashara tunajua alipo na hizi trilioni 40 ndio hao wanaotakiwa wazichangie lakini tusiwa- discourage kwenye biashara. Nasema hili kwa sababu haya mambo yanatokea sana hawa watu wanakata tamaa kuendelea kuwekeza hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka nije nalo, kwa sababu ya muda nilikuwa najaribu kupitia, nikaangalia historia ya Northern Ireland, wale watu wakati wanataka kuanzisha viwanda…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda umekwisha Mheshimiwa, lakini unaruhusiwa kupeleka mchango wa maandishi, kwa hiyo usiwe na wasiwasi.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)