Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya upendeleo kabisa maana nimeomba muda mrefu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza na mimi kwa sababu ni mara ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, naomba niseme maneno yafuatayo. Nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema ambaye muda wote amenipa uhai na afya ya kuwa hapa. Pili, nawashukuru wananchi wa Jimbo la Chemba kwa kunipa kura nyingi za kutosha. Tatu, kwa sababu ya muda nakishukuru Chama cha Mapinduzi kwa kunipa uteuzi na hatimaye kuwa Mbunge na leo niko hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nichangie kidogo kwenye elimu. Naishukuru Serikali sana kwa sababu ya elimu bure. Hata hivyo, zipo changamoto ambazo zimesababishwa na elimu bure na moja kubwa ni miundombinu. Tumekuwa na idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaoingia kila mwaka. Changamoto ambayo tunapata hasa zile Halmashauri ambazo hazina uwezo kuna matamko yanakuja kwamba lazima muwe na madarasa, madawati lakini Halmashauri zenyewe hazina uwezo wa kujenga madarasa lakini pia hazina uwezo wa kununua madawati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano mmoja wa athari ambazo zinatokana na haya matamko. Miaka mitatu au minne iliyopita Halmashauri ya Chemba ililazimika kutumia fedha zote za own sources kuhakikisha inanunua madawati lakini mpaka leo tunadaiwa kila mahali. CRDB wanatudai, watu walio-supply vyuma wanatudai toka mwaka 2016 mpaka leo. Sasa mimi nafikiria lazima kuwa na mpango maalum wa kuhakikisha tunakuwa na mfuko ambao au kuwa na mkakati wa kuhakikisha Serikali inachangia kwenye zile Halmashauri ambazo hazina uwezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo sio rahisi sana lina madhara makubwa sana kwa Halmashauri hizi mpya. Ziko Halmashauri zina uwezo zinakusanya shilingi bilioni 9 mpaka 12 kwa mwaka hata ukiwaambia wajenge hospitali wanaweza! Sasa tumekuwa na changamoto kubwa sana hiyo. Naomba sana Serikali iangalie namna bora kwenye hizi Halmashauri ambazo hazina uwezo wasitamke tu, tutafukuza Wakurugenzi, ma-DC lakini ukweli ni kwamba fedha hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimetoa mfano wa hali iliyotokea na sasa hivi ni hivyo hivyo. Sasa hivi tumeambiwa tujenge madarasa, tununue madawati, Halmashauri yangu zaidi ya asilimia 40 watoto wanakaa chini. Tungependa kila mtoto akae kwenye dawati lakini mimi Mbunge nina uwezo wa kununua madawati ya shule zote za Halmashauri? Haiwezekani! Tumeaambiwa tununue madawati, fedha hakuna na ni kweli fedha hakuna, nini cha kufanya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopanga hii mipango lazima i-reflect hali halisi iliyopo huko. Tusipofanya hivyo mipango yetu itakuwa tunaongea tu. Bahati nzuri niseme ukweli kwamba nimesikia michango mizuri sana ya Wabunge, nilikuwa nafikiria tofauti na hali sasa sijui kama Mawaziri wanachukua hiyo mipango inayoelezwa hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili naomba niongee kuhusu kilimo. Mimi ni mkulima mzuri kabisa. Hata tunayoyaongea kwamba tumetumia shilingi bilioni 180 kwenye kilimo mimi ambaye ni mkulima mkubwa pale Chemba sijawahi kuona kitu hicho. Pia huo mkakati wetu wa kilimo ukoje? Mimi mwenyewe nikilima hata kutafuta soko mpaka niende Nairobi, sijawahi kuona Afisa Kilimo wala mtu yeyote anayenifuta kuniuliza sasa ndugu yangu umelima tufanye ABC, changamoto kubwa ni masoko ya mazao haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo ni kubwa mno. Tunaongelea kulima, tunaongelea kilimo cha umwagiliaji, Jimbo tu maji ya kunywa hawana, sasa huu umwagiliaji utakuwaje? Hatuna uwezo wa kujenga mabwawa ili tupate maji ya kunywa halafu tunafikiria tujenge kwanza mabwawa kwa ajili ya kilimo. Hii inanipa changamoto kwa kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana Serikali na wakati mwingine najiuliza hivi nani ana wajibu wa kutafuta soko la mazao tunayolima? Tunasema asilimia 75 ni wakulima, mimi nalima lakini watu wengi walioko vijijini, leo utasikia gunia la ufuta Sh.90,000 lakini kesho Sh.40,000.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)