Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa muda huu uliniopa nizungumze. Ninayo mengi kidogo,kwahiyo nitaenda moja kwa moja kwenye mjadala huu. Pia nikupongeze wewe kwa namna ambavyo unatuongoza, kusema kweli inatupa hamasa kubwa sana kuwa Bungeni hapa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema kwamba naunga mkono kwa asilimia mia moja Mpango ambao umewasilishwa hasa kwasababu nafikiria kwamba mpango huu una uhalisia kwa kiasi kikubwa. Uhalisia kwamba assumptions zilizotumika kwa mfano ya kusema kwamba tunaweza tukaongeza pato la Taifa mwaka ujao kwa 6.3%,wangeweza wakasema 7%, lakini wamesema 6.3%, naamini ni achievable kwasababu ya misingi ambayo tumeijenga. Naamini kwamba kuna mambo mengi ambayo yanaweza yakatuteteresha kwasababu hatujajua dunia ina kwenda wapi kwasababu ya wingu ambalo bado lipo kuhusiana na corona kwenye nchi za nje, lakini naamini endapo hali itabadilika kidogo tunaweza tukafikia hiyo 6.3% kwa mwaka ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana pia wastani wa 8% utafikiwa mwishoni mwaawamu, lakini inawezekana pia hata 7%, ni nzuri sana kwasababu wale wanaojua kanuni ya ukuaji cumulative(limbikizo la ukuaji)wanaita ni the low ofcumulative growth. Kama unaongeza pato lako kwa asilimia 6.0 kwa mwaka unaweza uka-triple hiyo kwa miaka siyo zaidi ya miaka 10. Kwahiyo naamini kwamba tunaweza tukafikia hiyo nanihi yetu ambayo ni pato la uchumi wa kati, kiwango cha juu.Kwahiyo naamini tupo sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho nakosa tu kwenye huuMpango, nilikuwa natamani sana nione mipango ambayo imekaa fungamanishi kama kwa mfano ulivyokuwa mpango wa SAGCOT ambao unaeleza vitu vingi ambavyo vinasaidianaili kuhakikisha kwamba ile corridor inatoa kitu. Sasa kuna mipango kama huo wa SAGGOTambao naamini kwamba bado uko unatekelezwa. Nilikuwa nataka tuone kamalogisticsmapaulogistics plan za kufanya Tanzania hususan Dar es Salaam kuwa ni logistichub ya nchi hizi ambazo zinapakana na sisi, lakini sijauona vizuri. Ndiyo tunajenga vizuri infrastructure ile ya kutufungulia mipaka na kupeleka vitu kwenye mipaka na tuweze kupata a lot of value additions, lakini bado naona haijafungamanishwa sawasawa,ili kuona zile corridor tulizonazo zote zitatusaidia namna gani kuongeza kipato chetu bila kutegemea sana vitu vingine ambavyo ni more primary.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba wengi wanasema kilimo, kusema ukweli ni kizuri, lakini nataka kuwatahadharisha kwamba Mheshimiwa yuko sahihi anaposema kilimo hakilipi kama hatuna viwanda. Bado watakaoweka bei kama tutawauzia primary product watakuwa bado ni walaji wa kule nje, ni walaji wa Ulaya na wanapoona kwamba tunataka kufanikiwa watazidi kutubana, watasema bei ziko hivi bei zitaanza kutuvuruga, kwahiyo njia tu pekee ya kuweza kuhakikisha kwamba beiya mazao yetu inaimarika ni kuhakikisha kwamba tuna-process, tunauza kitu ambacho kinaweza kikahifadhiwa, kikafika kwenye masoko tofauti tofauti kwa bei ambayo siyo ile inakuwa dictated by the consumers. Kama consumers ata- dictate bado utapata matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti,kama ninavyosema kilimo lazima tunapokizungumzia tuseme tutafanyaje tukiunganishe na viwanda ili kiweze ku-process. Niseme kwamba tumezungumza mambo mengi kuhusiana naukuaji nakadhalika, lakini ni lazima tuzungumzie strength. Watu wanapotengeneza plan yoyote unaangalia strength zako ni nini na ni sawa tukasema ni uongozi bora, amani, utulivu, mshikamano na vitu vyote hivyo na siasa safi, lakini kitu ambacho hatujakiona ni ile strength tuliyojenga kwa kutuliza uchumi wetu ukawa tulivu ambao mfumuko wa bei upo chini, wenye exchange rate ambayo ni nzuri nakadhalika ambayo inatufungulia milango ya kuweza kuisaidia Serikali yetu kuweza kukopa kwa bei nafuu kabisa.(Makofi)

Mheshimiwa MWENYEKITI,tunapoangalia mipango hii mara nyingi tunajua tunatumia cash budget, sasa tukianza kuzungumza mpango kwa kuanzia kwenye matumizi kwa kuorodhesha vitu gani tunataka vifanywe, kwanza niseme naomba Mungu ajaalie kwamba pamoja na mafanikio tuliopata kwenye miundombinu, kule Vunjo wamesahau. Naomba wasisahau zile barabara zetu kule Vunjo,lakini kama tutaorodhesha kila mtu aorodheshe vitu, the shopping distance is huge,TARURA inataka pesa,TANROADs inataka pesa, halafu bado wengine wanasema Serikali ijenge viwanda, hili hapana, Serikali haiwezi kujenga viwanda, zaidi Serikali iwezeshe kwenye viwanda vya kimkakati ambavyo tunatakiwa Serikali kama tunavijua kwenye maelekezo ya hotuba za Rais. Hiyo ya kuwezesha viwanda vya kimkakati hata kama ikiingia ubia lakini kuhamasisha, sera ziwe safi,blue print iwepo, mambo yawe sawasawa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,kusema kweli hatuwezi kusema Serikali ikajenge viwanda vya alizeti nakadhalika hatutaweza hiyo, tuwezeshe watu na ndiyo kazi yetu kwenye zile kamati ambazo zinahusika. Kwahiyo nataka kusema hiyo tuwe makini,kwasababu hatuwezi kuorodhesha. Nimejifunza kitu cha msingi sana na nimefurahia sana Wabunge fulani wameanza kusema kwanini tusipate fedha namna hii. Kwasababu cha kwanza ni mapato, je, yanatoka wapi? Kuna Mheshimiwa Shabiby alisema pengine mapato tuongeze tozo kwenye matumizi ya mafuta na tena akatoa pia mawazo ya namna hii, yale ndiyo mambo tunataka tujue kwasababu ukishapata zile fedha ukimpa Rais wetu anazitumia vizuri, anajua kuzisimamia kwa ufanisi,zitazaa vyovyote tunavyotaka, lakini tuangalie na nashukuru wale wanaozungumzia kwamba tuzibe mianya ya pesa kupotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti,tax effort yetu we mention kwenye hizi documentis 13%,12.9% ndiyo revenue effort tuliyofanya mpaka mwaka jana na tunaendelea kusema mwaka unaokuja 13.3% ndiyo tax effort, nchi nyingine hata hapo Kenya 23% ya GDP, uwiano kati ya mapato ya Serikali na GDP, pato la Taifa ni 20%, sisi tunasema 13% ni ndogo sana, ina maana kwamba njia tunazotumia kutoza kodi na njia tunazokusanya mapato yetu ni finyu. Aidha, vile vyombo vyetu vinavyoshughulika na ukusanyaji wa mapato vijiunde upya vi-think out of the box, what is happening?Effort yoyote Mheshimiwa Rais aliyofanya kupata hela kwenye madini na nini lakini bado eti revenue effort 13% ofGDP isnothing, tunataka tupate 20% whichmeans tunapata 28 trilioni, tunge- finance vitu gani? TARURA ingepatapesa mpaka tushindwe kuzungumza, lakini ninavyoona ni kwamba kuna kitu kiko hafifu hapo katikati kwenye ukusanyaji, sijui zinaenda wapi hizo hela. Kwanini iwe 13% au sisi tuna overstateGDP yetu pengine I do not know, lakini kama kweli takwimu ziko sahihi 13% ni ndogo toka tukiwa kule sisi miaka ya 1996, kwahiyo tunazungumza kwamba effort yetu lazima ifikie 20%, sasa mpaka leo hii 13%, tuna matatizo lazima tuanzie hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema tuna-demand barabara na vitu vingine, je, mapato yanatoka wapi? Kwasababu hutapata kule kwenye Wizara ya Viwanda wanapata 6%, kilimo wanapata 6% of approved budget, it willnever work. Kwasababu hiyo tuna over state hizi revenue ndiyo sababu tunapanga vitu ambavyo ni hewa,havitatekelezeka,where is the money?The money is the cash budget, sasa niseme hivi kwanini nimeanza kusema kwamba tuna strength moja ya kukopesha. Revenue ya Serikali ya matumizi inatokana na vitu viwili taxrevenueyaani mambo ya kodi na tozo; pili, mikopo. Sasa mikopo inaweza ikatokana kwenye mabenki ya ndani napensionfunds nakadhalika yaani vianzio vya ndani, lakini pia zinaweza zikatoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa nje na tunaambiwa kwamba nanii yetu iko chini sana, yaani uhimilivu wetu wa ukopaji bado tunaweza tuka-affordhata mara tano, sasa kwanini tusikope zaidi, tunaogopa nini kukopa kwasababu tunajenga rasilimali, tunajenga mtaji, nchi hii ina balance sheet yake,liabilities and assets. Watu wanaposema sijui deni hili siyo himilivu, deni walikuwa wanapiga ile gross hawaondoi ile rasilimali tuliyotengeneza,assetskwahiyo lazima uchukue asset - liabilities unapata net liability au netasset.

Sasa sisi ukiangalia kwa mfano vitu ambavyo vimejengwa Awamu hii ya Tano thamani yake na deni letu, ni kama hatuna deni yaani ukiangalia kwa uhimilivu watu wa Taifa letu,uhimilivu wa balance sheet ya kwetu,network yetu ni nzuri kwasababu tumekopa tumeweka kule, hata kama tungekuwa tumekopa mara ngap,i tutaingiza kwenye asset inazaa vizuri.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Dkt. Kimei.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie…

MWENYEKITI: Tayari ni kengele ya pili.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Sasa nina mengi sana, lakini...

MBUNGE FULANI: Unga mkono hoja.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI:Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.(Makofi)