Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili nami kuwa mmoja wa wachangiaji katika hotuba yetu ya leo ya mipango. Katika kuchangia nitajikita kwenye vile vitu ambavyo vinaleta impact ya haraka. Mipango ya haraka ambayo pesa yake inapatikana kwa haraka ambayo italiingizia Taifa faida kwa haraka. Nitachangia vitu viwili, nitachangia utalii na kilimo, nikipata nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia katika hotuba ya leo inaonekana kabisa wazi kwamba, sekta ya utalii ni ya pili kwa uchangiaji kwa Taifa kwa sababu, inachangia asilimia 17.5, lakini ukiangalia katika mpango wake wa miaka mitano katika hotuba unasema kwamba, itakua hadi kufika asilimia 28. Sasa ukiangalia katika sekta hii ambayo kuna nchi zinaishi kwa kutegemea utalii peke yake kwa mfano, nchi nyingi sana zinategemea utalii hata hapo ukichukua hiyo Seychelles waliyokuwa wanaitajataja hapo, ukiangalia hata Ufaransa asilimia nayo inategemea utalii kama watu hawafahamu, Misri, Thailand, Morocco. Sasa nchi kama Tanzania ambayo uwekezaji wake katika utalii hauna gharama kwa sababu vitu vingi tayari ni vya asili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia katika vivutio, Tanzania ni nchi ya pili ukitoa Brazil, lakini hakuna mkakati wowote wa kutangaza utalii kwenye hii nchi na hakuna mkakati wowote wa kuonesha kwamba, utalii unaweza ukachangia zaidi ya asilimia 80 ya mapato ya nchi hii.

MWENYEKITI: Chief Whip, wakati Mheshimiwa Shabiby anazungumzia jinsi ambavyo sekta ya utalii ni muhimu kiasi hicho, humu kwenye ukumbi hamna cha Waziri wa Utalii wala Naibu wake, wana yao tu. Endelea Mheshimiwa Shabiby.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sasa ukiangalia nini tunakwama? Tunakwama sana kwenye advertise, kwenye utangazaji. Hatutangazi kabisa utalii kwenye hii nchi wala hakuna mpango wa kutangaza. Kwa hiyo, ushauri wangu kwenye hizi Balozi zetu lazima pawepo na wale commercial attaches lazima wawepo. Tunaita muambata wa kibiashara kwa sababu, ukiweka muambata wa kibiashara kwenye kila ubalozi utakuwa unatangaza utalii, unatangaza uwekezaji, unatangaza na biashara nyingine kwa hiyo, tunakuwa na watu wa diplomasia ya uchumi ndani ya zile balozi kwa hiyo, tunakuwa tunaangalia nchi. Kwa mfano, nchi kama America tunahitaji watalii, basi tunampeleka muambata yule ambaye yeye anakuwa ni mtaalamu wa kutangaza utalii. Tunaangalia nchi fulani tuna mawasiliano nayo labda kwa ajili ya kilimo, tunampeleka muambata wa kiuchumi ambaye anahusika na kilimo, kwa hiyo, tunakuwa tunafanya hivyo. Hiyo itasaidia kuutangaza utalii wetu vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia leo hii mbuga ya Serengeti ni mbuga bora duniani, lakini haifahamiki kama Masai Mara ya Kenya. Sasa hapo unaweza ukajiuliza ni kitu gani kwa sababu, watalii wengi wanaokwenda Kenya wanakuja kwa ajili ya kuangalia Masai Mara ndio baadaye waje Serengeti au waje Kilimanjaro. Hata Kilimanjaro inatangazika sana Kenya kuliko Tanzania kwa hiyo, tunachezea na hapa ndio mahali ambapo pana pesa kabisa nyingi. Mimi huwa sitaki kutoa ile mipango ambayo itafanyika huko ya maneno maneno, hapana, huu ni mpango ambao uko wazi na hii ni hot cake kabisa, haina shida kwenye hii pesa ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia leo Brazil kwa nini imekuwa ya kwanza duniani, ni kwa ajili ya utalii wa bahari. Sisi huku tuna utalii wa asili, lakini leo bahari kama pale Kigamboni, bahari mali kabisa, beach zake ni safi, leo yamejaa magereji, yamejaa maviwanda, yaani hata mpango wa kutumia ardhi haueleweki. Mimi Mbunge niko muda mrefu, hata hivi kusimama basi, maana saa nyingine mnaongea tu halafu vitu havitekelezeki. Sasa Mheshimiwa Waziri lazima aangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu watu wanalalamika kuhusu habari ya utalii sijui asilimia 10 hiyo iliyoongezwa kwenye utalii. Lazima vitu vingine watu wawe wazalendo, kumleta mtalii mmoja haya makampuni ya binafsi yanachukua dola 5,000, kwa hiyo, wewe kuongezewa dola 10 tu unapiga kelele utalii Tanzania utakufa, utakufa kwa msingi gani? Hauwezi kufa utalii kwa ajili ya dola 10, haiwezekani kitu kama hicho. Cha msingi tu ni kuutangaza utalii watalii waje wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi lingine katika utalii, lazima tuwe na regulations, private regulations, katika kama zilivyokuwa sekta nyingine. Leo ukija huku kwenye sekta labda ya Mawasiliano kuna TCRA, ukienda labda huku Uchukuzi kuna hawa wengine hawa sijui LATRA, ukienda kwenye Nishati kuna EWURA. Huku nako lazima kutengenezwe regulation ya private ili iangalie na kudhibiti maslahi pamoja na kuchukua hao wadau nao kuangalia watafanyaje, ili utalii uendelee kukua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye masuala ya kilimo; hii lazima watu mkubali, tunapanga vitu vingi sana, lakini bahati nzuri unanifahamu vizuri ni mkulima, mfugaji, mfanyabiashara, vyote nafanya. Nchi hii tusidanganywe na mambo mengi sana, kama tutadharau kilimo, kilimo tumebadilisha slogan za kila aina; kilimo ni uhai, kilimo sijui ni uti wa mgongo, sijui nguvu kazi, sijui kilimo kwanza, sasa hivi kilimo cha biashara, lakini mafanikio hakuna. Hata Mheshimiwa Bashe wakati anajibu mpango huu, mpango huu, mpango huu, wakati hela hazipo na hautekelezeki. Hii ni hadithi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tajiri namba moja wa Tanzania kwanza ni mkulima anayelima kuanzia nusu eka mpaka eka 50. Hii yote mnazungumza tu hela zimebanwa, sijui hela mtaani hakuna, kwa nini hamshangai mwezi wa Januari, Februari na Machi wakati mkulima yuko shamba ndio hela hamna ninyi? Si mjiulize? Ukiingia mwezi wa Januari, Februari na Machi, hakuna anayepanda basi, hakuna anayeingia dukani, hakuna anayenunua chochote na huko mabenki nako pesa hakuna, hakuna kila sehemu, lakini kuna mkakati gani? Kuna mpango gani wa kumnyanyua huyu mtu? Hakuna mpango wowote wa kumnyanyua huyu mtu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza Habari ya irrigation. Irrigation ya Tanzania tunaangalia tu mito kwa nini hatuangalii na nchi kavu kama Dodoma na sehemu nyingine? Tunatafuta dola, lakini tunapoteza dola kila siku ya Mungu kununua ngano. Tunapoteza dola kila siku ya Mungu, hizo alizeti tunasema viwanda, alizeti inayolimwa Tanzania inatosha kwa miezi mitatu tu alizeti imeisha, kwa hiyo, viwanda vinasimama. Ngano, kwa miaka hiyo ya Awamu ya Kwanza, Basutu, wale wanaotoka Arusha, mashamba ya Basutu yalikuwa yanalisha nchi nzima ya Tanzania ngano, leo hata eka moja ya ngano hailimwi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya Saudi Arabia hakuna mvua. Mvua inanyesha baada ya miaka mitano, inanyesha mvua mara moja, lakini wanalima ngano tani laki saba kwa mwaka. Mwaka jana kuja mwaka huu 2019/2020 wamelima tani laki saba. Hapa Tanzania kuna bahati ya mvua mpaka tunaichukia, eka mbili hakuna, halafu tunazungumza kitu gani? Halafu tunachukua hiyo hiyo pesa tunayoitafuta, dola, tunaenda kununua ngano ambayo tunaweza tukalima tukajilisha. Tunaenda kununua mafuta ya kula ambayo tunaweza kuleta hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango ya irrigation tusidanganyane wala tusipakane mafuta hapa, Wizara ya Fedha haitoi pesa kwenye Wizara ya Kilimo, wala tusitake kupambana, haitoi pesa kabisa. Hayo mambo ya irrigation ni maneno tu. Labda Wabunge wageni, kama hamjui, hizi hela zinazopangwa zote ukija kuangalia zimetoka robo au hata robo isifike. Sasa mipango ya Wizara itaenda vipi? Nawashangaa tunang’ang’ania tu TARURA, TARURA, kama kilimo hakuna, TARURA watabeaba nini huko kwenye mabarabara hayo? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda cha mwisho, nashauri. kodi ya mafuta inayotolewa…

MWENYEKITI: Wabunge wageni mnawaona Wabunge wenyeji wanavyochambua hoja? (Makofi/Kicheko)

Endelea Mheshimiwa malizia.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa kitu kimoja, hii habari ya TARURA; watu wanazungumza tunatoa mazao yetu, yepi? Kama sio kupita sisi Wabunge kwenye barabara, wale wazee wameshazoea wanataka hela tu. Mwananchi akiwa na hela hata ukimpitisha shimoni hapa mradi kichwa kionekane yeye anaona barabara si ziko kama lami tu. Kinachotakiwa hapa ni kuwajengea mazingira wao kupata pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe ushauri, kwenye barabara hizi tunachangia shilingi 263 kutoka kwenye mafuta, kila lita moja na kwenye umeme tunachangia shilingi 50 kila lita; nashauri, mimi nina vituo vya mafuta na mafuta yanapanda na kushuka, kwa nini pale tusiongeze shilingi 37 iwe shilingi 300 iende kwenye kilimo ili iweze kuchukua hili eneo? Kwa sababu, kama kuna mtu mwingine na mimi mwenyewe nina mabasi na malori silalamiki kupandishwa mafuta, sasa nione mtu alalamike humu. Ipandishwe shilingi 37 iende kwenye kilimo, tunachangia tu EWURA, sijui nani TARURA, TARURA wenyewe hawa ni wezi tu mimi nawashangaa mnapiga kelele, barabara wanapata hela hawatengenezi lolote. Huku kuwatoa sasa hivi hawahusiki kwa Madiwani, wamekuwa Mungu mtu, nashangaa Wabunge hamzungumzi hapa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana TARURA sasa hivi Madiwani ndio wana mikakati ya barabara zile. Diwani ndio anayesema barabara ya kimkakati ni barabara fulani kutoka pale kwenda pale, lakini leo TARURA wamekuwa wao Mameneja wa Wilaya, Mameneja wa Mikoa wamekuwa kama Mungu mtu kwa sababu, hawawajibiki kwa Madiwani. Wabaki kwenye management, lakini lazima mipango yao irudi kulekule kwa Madiwani. Ahsante. (Makofi)