Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naomba nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kupata fursa hii. Vilevile nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja iliyo mbele yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zaidi ya asilimia 93 ya Wabunge waliochangia wameongelea sekta ya kilimo. Hii inaonesha ni namna gani sekta hii inagusa maisha ya watu na umuhimu wake. Sisi kama Wizara ya Kilimo tunakiri na kupokea baadhi ya changamoto ambazo wamezisema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo mambo ambayo katika kipindi cha miaka mitano ijayo, Wizara na Serikali kwa ujumla imejipanga kuhakikisha tunaondoa hizi changamoto zinazotukabili katika sekta ya kilimo. Changamoto ya kwanza ni mbegu na viuatilifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, siri na future ya sekta ya kilimo ni research and development. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo Ilani imetupa targets za ku-attain katika kila zao ambazo ni lazima tuzifikie na target hiyo siri yake ni mbegu. Kwa hiyo, kama Wizara tutakapokuja katika mpango hatua ya kwanza tuliyoamua suala la mbegu litakuwa ni suala la uzalishaji wa mbegu kwa solution za ndani. Kwa kipindi cha miaka mitano ijayo tutawekeza shilingi bilioni 179 kwa ajili ya research and development and seed multiplication. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ni vizuri Waheshimiwa Wabunge wakaelewa. Tunapozungumzia mbegu kwanza hili ni suala la dunia na Tanzania ni sehemu ya dunia na sisi hatuwezi kujiondoa katika hiyo seti. Kwa hiyo, tunawekeza katika research kwa ajili ya ku-develop mbegu za aina ya OPV na hybrid lakini wakati huo huo kutunza mbegu zetu za asili na sisi kama Wizara tunakuja hapo mbele Mwenyezi Mungu akitujaalia na sheria maalum ya kulinda traditional seeds ili ziweze kufanyiwa purification na ziweze kufanyiwa maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi mbegu tunazozijadili ni nne, ni traditional seed (mbegu zetu za asili), OPV, hybrid na sasa kuna teknolojia ya GMO. Sisi kama nchi tumesema hatutumii mbegu za GMO na hatutaruhusu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeweka utaratibu wa wazi kwamba hybrid seed ambayo inajulikana parent seeds wake (wazazi wawili), labda nitumie lugha rahisi, tunapozungumzia mbegu za hybrid tunazungumzia mbegu mbili za kiume na kike zenye sifa mbili tofauti zinazofanyiwa cross breeding. Hapa msingi wake ni mbegu za asili. Unaweza ukakuta mbegu ya mahindi ya asili A ina sifa ya kuwa na uzalishaji mkubwa lakini haina uwezo wa ku-resist magonjwa. Mbegu B ina sifa ya ku-resist magonjwa lakini uzalishaji wake ni mdogo. Wataalam wetu wanafanya kazi ya kuzi-breed hizi mbegu mbili ili kupata mbegu ambayo inaweza kuwa na sifa zote mbili na kumsaidia mkulima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama nchi potential demand yetu ya mbegu ni tani 371,000. Hii ndiyo potential demand yetu lakini mbegu tunazozalisha za kisasa ni tani 76,000 na tani 11,000 ni mbegu tunazoagiza kutoka nje na mbegu zinazobaki ni mbegu zetu za asili ambazo tumekuwa tukizitumia katika hatua mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano zao kama alizeti, tunakiri kama Wizara tumechukua hatua katika suala la kupambana na gap ya mafuta. Hivi karibuni Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuwa Kigoma kuzindua usambazaji wa miche ya michikichi. Tumegawa miche ya michikichi zaidi ya 1,000,000. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sasa hivi kama Wizara tunahitaji uzalishaji wa tani 5,000 za hybrid seed na OPV seed za alizeti ili tuweze kufikia uzalishaji tunaouhitaji wa mbegu za mafuta. Ni kweli viwanda vya kuchakata mafuta vinakabiliwa na changmoto kubwa sana katika suala la uzalishaji wa mbegu. Nilitaka nitoe tu commitment ya Wizara katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya pili ambayo tunachukua, Rais katika hotuba amesema suala la ngano. Nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge wa Hanang, hivi sasa tunavyoongea Wizara ya Kilimo imesaini MoU na wanunuzi na wachakataji wa ngano ndani ya nchi. Tunatengeneza utaratibu ambao tumekubaliana na private sector kwamba hatoagiza ngano kutoka nje kabla ya kununua ngano yote ya ndani. Sasa tunavyoongea tumejiwekea lengo la kuzalisha metric tonnes 150,000 katika msimu huu unaokuja na tutagawa jumla ya tani 36,000 ya mbegu kwa ajili ya kuzalisha ngano katika Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Dodoma tumefanya pilot project hapa Bahi ambapo ndiyo sehemu ambayo mbegu ya ngano imeonekana ina-mature kwa muda mfupi kuliko wakati wowote, katika Wilaya ya Bahi na Mkoa wa Rukwa tunagawa hizi mbegu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulichokubaliana na wanunuzi ni nini? Kilimo ni biashara, lazima u-define volume and price. Kwa hiyo, tulikaa na wanunuzi tukawauliza wananunua ngano kutoka nje kwa bei gani? Tukapiga mahesabu na tukakubaliana watanunua kilo moja kutoka kwa mkulima kwa shilingi 800 bei ya chini mpaka Sh.1,000 kilo moja ya ngano. Sasa hivi wakulima walikuwa wanauza kati ya shilingi 500 na shilingi 600 na walikuwa hawana uhakika wa soko. Nataka nimhakikishie Mbunge wa Hanang hivi sasa tunavyoongea Kampuni ya Bakhresa wako Wilaya ya Hanang, awasiliane na DC wake wanachukua zile tani 400 zilizoko pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, secret ya kilimo ni economies of scale. Mimi nataka niseme sisi wote ni wajumbe wa Baraza la Madiwani, niwaombe sana tusipokuwa makini tutajenga Taifa la wachuuzi badala ya Taifa la wazalishaji. Wizara tuko tayari kuwasaidia kwa ajili ya kuanzisha block farming na katika bajeti ijayo tengeni maeneo kama Wilaya ya Manyoni kama kwenye suala la korosho tuweze kuzalisha mazao mbalimbali na sisi tutawasaidia mbegu, wataalam, vitendea kazi ili tuweze kulifikia lengo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba kama Wizara ya Kilimo tumejiwekea target...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Muda wako umekwisha Mheshimiwa.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, namalizia tu. Tumejiwekea lengo la kukua kwa asilimia 10 katika kipindi cha miaka mitano ijayo badala ya asilimia 5. Tunawaomba support, ushirikiano wenu na ni lazima tukubaliane kama nchi kuwekeza katika kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)