Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. SOUD MUHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais katika hotuba yake amesisitiza kuziendeleza na kuhifadhi maliasili za nchi. Katika kumuunga mkono na ili kumsaidia kufikia malengo ni vyema changamoto za sekta za maji, ardhi, kilimo na mifugo ambazo zinachangia moja kwa moja uharibifu wa maliasili zishughulikiwe kwa ushirikiano wa kisekta.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ripoti ya Mawaziri saba kuhusu ardhi iletwe Bungeni na kujadiliwa, kwani kuna michango mizuri ya kujenga kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Serikali iwe makini katika kumega hifadhi na mapori ya akiba kwa lengo la utatuzi wa changamoto za sekta za ardhi, mifugo na kilimo. Huu hauwezi kuwa ufumbuzi wa kudumu.