Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi uliyonipatia ya kuweza kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais. Awali ya yote nipende kumshukuru sana Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye amenijaalia uzima na afya njema hatimaye nimekuwa mmoja wa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwashukuru sana wanawake wa Mkoa wa Mbeya kwa namna ambavyo wamenipatia kura nyingi ambazo zilisababisha jina langu kupelekwa kwenye Kamati Kuu Taifa. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu ambaye ndiyo Mwenyekiti wetu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa. Namshukuru yeye pamoja na Kamati Kuu kwa kupendekeza jina langu nami nimekuwa Mbunge sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nikupongeze wewe kwa kuwa Mbunge wa Mbeya Mjini. Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson Mwansasu hongera sana kwa kuwa Mbunge wa Mbeya Mjini na Mbeya Mjini sasa imetulia kama lilivyo jina lako. Napenda vile vile kuwashukuru sana wananchi wa Mbeya Jiji na wananchi wa Mkoa wa Mbeya wote kwa ujumla kwa namna ambavyo waliweza kukichagua Chama Cha Mapinduzi kwa kura nyingi za heshima. Napenda kuwashukuru Watanzania wote kwa ujumla. Tanzania yetu sasa inapendeza, imekuwa ni ya kijani na ina amani ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa nzuri anazozifanya ambapo Tanzania yetu sasa inatambulika dunia nzima na inaheshimika dunia nzima kwa namna anavyoleta maendeleo kwenye nchi yetu. Nawapongeza sana Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri kwa nafasi zao hizo. Natambua ni watu makini na ni mahiri sana watazitendea haki kwa maana ya kuisaidia Serikali ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya wanawake wa Mkoa wa Mbeya katika kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais, namshukuru sana Mheshimiwa Rais alisema kwamba kwenye hotuba ile atavipa vipaumbele sana vikundi tofauti tofauti kwenye mikopo kwa maana ya kwamba viendelee kusonga mbele. Naomba sana Mheshimiwa Rais kwa hotuba hii awape kipaumbele wanawake wa Mkoa wa Mbeya na Tanzania yote kwa ujumla, maana akiwezeshwa mwanamke, mwanamke ndiyo kila kitu, mwanamke ndiyo mama ambaye anajali familia, anasaidia Watoto, anamjali hata baba pia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuomba asilimia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kengele imenikatili, lakini nitaandika kwa sababu napenda sana kuongelea habari za wanawake namna gani waweze kusaidiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)