Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii adhimu kuweza kuchangia katika hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa Bungeni mwaka 2020 lakini na ile ya mwaka 2015.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, niwashukuru wananchi wa Jimbo la Manonga kwa kunipa kura nyingi lakini pia kumpa kura nyingi Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kwa kukichagua Chama cha Mapinduzi. Kama unavyotambua leo ni tarehe 5 Februari, Chama cha Mapinduzi, chama adimu, chama kikongwe Barani Afrika na duniani kinakwenda kutimiza miaka 44 toka kuzaliwa kwake. Chama hiki kina heshima kubwa sana siyo tu ndani ya nchi bali na Afrika kwa ujumla. Ni chama ambacho kinajihuisha kila baada ya miaka mitano na tunatarajia mwakani kitajihuisha tena. Kwa hiyo, ni chama pendwa na kinafanya kazi ambayo Watanzania wanakitarajia na wanakitegemea kwa asilimia kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo na kukitakia happy birthday Chama cha Mapinduzi, nijielekeze kwenye hoja ya msingi. Kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa hotuba zenye maono na mwelekeo wa nchi yetu tunataka kwenda wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya mwaka 2015 alionyesha upingaji mkubwa wa ufisadi, rushwa na matumizi mabaya ya madaraka. Alizungumzia pia masuala ya kufufua Shirika letu la Ndege, ujenzi wa reli na mambo mbalimbali. Leo tumeshuhudia ufufuaji wa Shirika letu la Ndege, tuna zaidi ya ndege 8, ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme ambayo itakuwa bora katika Afrika Mashariki na Kati, lakini pia ujenzi wa Bwawa kubwa la Stiegler’s lenye uwezo wa kuzalisha umeme zaidi ya megawatt 2,115.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba yake amezungumzia kutengeneza ajira zaidi ya milioni 8. Naomba kuchangia kwenye ajira na niwaombe watu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Elimu na Wizara ya Ajira waungane kama timu moja kutengeneza ajira za vijana wetu ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hizi ajira milioni 8 niwaombe watengeneze ajira milioni 1 nje ya Tanzania. Watengeneze fursa za Watanzania kufanya kazi nje ya nchi yetu. Yapo mambo ambayo tunaweza tukanufaika nayo kupitia ajira hizi ambazo Wizara itazitengeneza. Kupitia Balozi zetu ambazo zipo nje wanaweza kutengeneza mfumo ambao ukawatengenezea vijana wa Kitanzania waliomaliza vyuo vikuu wakapata kazi formal na informal katika katika nchi hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ajira inaleta ukuaji wa uchumi katika nchi. Mfano nchi kama Philippine wananchi wake zaidi ya milioni 12 wanafanya kazi nje ya nchi na wanapata faida kubwa sana. Mfano tukitengeneza ajira milioni moja wakachangia kila mwezi ndani ya nchi yetu dola mia moja tu wakarudisha kuwapa wazazi wao, tutatengeneza dola milioni 100 zitakazoingia kila mwezi ndani ya nchi yetu. Dola milioni 100 kwa mwezi uki-multiply by miezi kumi na mbili tutapata zaidi ya dola bilioni 1.2, hili ni soko ambalo tunatakiwa tulitumie.

Mheshimiwa Naibu Spika, wapi tunaweza tukaanzia? Sisi tuna Kiswahili, hii ni bidhaa adimu ambapo nchi nyingine hawana na kama wanayo lakini si kwa undani wake. Tutumie nafasi hii kukitangaza Kiswahili, tufanye lobbing katika nchi kama South Africa ambao wanataka kuanzisha kufundisha Kiswahili katika nchi yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mambo ya Nje iongee na South Africa tupeleke vijana wetu wakafanye kazi kule, tupeleke vijana wetu Namibia, Zimbabwe, hata kama tukitoa offer katika vijina 100, 20 tutawalipa sisi itaweza kutengeneza ajira kwa vijana wetu. Badala ya kuzagaa mitaani wataweza kupata fursa ya kufundisha Kiswahili ndani ya Afrika lakini pia hata Marekani ikiwezekana kwa sababu viko vyuo vikuu Marekani wanafundisha Kiswahili badala ya kuliacha suala hili liwe la mtu mmoja mmoja ambapo walimu wanajitafutia ajira wenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata katika sekta ya afya tuna uwezo wa kutengeneza ajira za madaktari wetu. Inawezekana tukawa na uchumi mdogo wa kuajiri wanafunzi wote lakini tunaweza kutengeneza ajira za vijana wetu katika sekta ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, muda wangu siyo rafiki sana, napenda kupongeza hotuba ya Mheshimiwa Rais na naunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)