Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa uhai. Nishukuru sana wana Maswa kwa kunichagua kwa kura nyingi sana, nimepata ushindi mkubwa kuanzia kwa Rais, Ubunge hadi kwa Madiwani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niendelee kutoa pongezi sana kwa Mheshimiwa wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya hasa kukusanya maduhuli na kuhakikisha kwamba matumizi ya fedha inayokusanywa na Serikali inafanya kazi iliyotakiwa. Kwa kweli usimamizi umekuwa ni mzuri sana kwa Serikali na matokeo tunayaona kwamba fedha inayokusanywa na Serikali inatumika ipasavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitajikita kwenye jambo moja muhimu. Mheshimiwa Rais wakati anatoa hotuba alisema kwamba jambo ambalo atalipa kipaumbele au Serikali italipa kipaumbele ni kulinda na kudumisha tunu ya taifa letu yaani amani, umoja na mshikamano wa uhuru wa nchi yetu. Nazungumza hili kwa makusudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna janga kubwa la corona ambalo limeitikisa dunia. Naomba nikuambie kitu kinachompeleka mtu hospitali siku zote, nazungumza hili ili watu waweze kunielewa, cha kwanza huwa ni maumivu (pain). Jambo la pili linalompeleka mtu hospitali huwa ni hofu. Hofu ziko mbili; ya kwanza hofu ya disability yaani kupata ulemavu na hofu ya pili huwa ni ya kifo. Haya ni mambo makubwa yanayompeleka mwanadamu hospitali kwenda kupata huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, imetengenezwa hofu na hofu hii ni ya kifo, dunia imetengenezewa hofu ya gonjwa la corona, taarifa zimekuwa exaggerated as if kwamba corona ni gonjwa jipya litakwenda kuangamiza dunia hii. Ni mwamba mmoja tu Dkt. John Pombe Magufuli amesimama imara na kupingana na hofu hii. Naomba Watanzania na Waheshimiwa Wabunge tuungane na juhudi za Mheshimiwa Rais wetu kuondoa hofu hii ambapo ni janga kubwa linakwenda kuleta vifo kwa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, magonjwa yalikuwepo mengi, kuna ugonjwa ulikuwa unaitwa smallpox (ndui), ulikuwa eradicated mwaka 1977 kwa chanjo na ulikuwa unasababishwa na virus. Kuna ugonjwa mwingine wa surua uliuwa watoto wengi, ulipatiwa chanjo na sasa hivi umekuwa controlled. Kuna tatizo kubwa la malaria, tunapata infection ya malaria milioni 200 kila mwaka, hawa watu wangekuwa wanatupenda ugonjwa wa malaria wangeukomesha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, miaka ya nyuma, kuna Profesa mmoja Mjerumani alileta genes ambapo angeweza kuwasambaza kwa mbu wote na wangebadilisha behavior ya kutafuta damu kwa kwa ajili ya ku-nourish mayai yao kutoka kwa binadamu kwenda kwa wanyama na mbu hao wasingesababisha malaria ingekuwa historia kama walivyofanya kwenye chickenpox au smallpox.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna ugonjwa wa HIV umeanza toka mwaka 1981 na wanamjua huyu retrovirus yupo type one na type two, wanajua behavior yao, biashara ipo kwenye antiretroviral, hapo ndipo wanapokunywa maziwa. Wameanza na vidoge vingi kwa wagonjwa wameenda kwenye kidonge kimoja na sasa hivi wanakwenda kwenye innovation ya sindano moja kwa miezi sita. Biashara hii inaenda kwisha kwa sababu muamko umeeleweka, vifo vimepungua kwa asilimia 60 na maambukizi yamepungua kwa zaidi ya asilimia 40 na Tanzania tumepambana nayo vizuri sasa deal imeisha kwenye HIV, the deal now is corona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna ugonjwa huu wa corona umetambulika China type ya kwanza na type ya pili ambayo wanasema imetokea South Africa wanakuja na chanjo wanasema hii ndiyo chanjo ambayo inakwenda ku- solve corona, chanjo ya HIV ya toka mwaka 1981 iko wapi? Kwenye malaria nimedokeza biashara ipo kwenye vimelea vya malaria, neti, antimalaria na ugonjwa huu ni biashara kwao na ndiyo maana wanaendelea kuufuga. Kuna Waitaliano wameleta genes wanasambaza, mbu wamembadilisha anakuwa na jinsia mbili; anakuwa hana mdomo wa kunyonya damu, badala ya kumng’ata binadamu anakwenda kufa kwa sababu hawezi kumng’ata binadamu na spread ya malaria inaisha. Aliyegundua hizi genes alikufa mazingira ya kutatanisha kisa biashara ya antimalaria na neti na wanaotutengenezea net bure tunawajua. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana, kengele imeshagonga.

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)