Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu Mwenye Rehema, kwa kutujalia wote kuweza kuwepo hapa siku ya leo. Kipekee na kwa dhati ya moyo wangu…

NAIBU SPIKA: Samahani Mheshimiwa Mbunge kidogo. Waheshimiwa dakika ni tano na kengele itagongwa moja. Karibu Mheshimiwa Judith Kapinga.

MHE. JUDITH KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama nilivyotangulia kusema, awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu Mwenye Rehema kwa kutujalia kuwepo hapa siku ya leo. Kipekee na kwa dhati ya moyo wangu, napenda kumshukuru Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli kwa maono makubwa aliyonayo kwa taifa letu la Tanzania. Namwombea afya zaidi, nguvu zaidi na hekima zaidi ili aweze kutuongoza katika utekelezaji wa maono haya kwa kipindi hiki cha miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli imeeleza nia ya dhati ya Serikali kuboresha mfumo wa elimu ili kuleta tija kwa wahitimu. Pamoja na kuipongeza Serikali kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya elimu, mfumo wetu wa elimu bado unalalamikiwa sana. Sababu kuu ni moja, bado haujaweza kumzalia matunda kijana wa Kitanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia taifa letu lina vijana wengi wenye talanta ambao iwapo mfumo wa elimu ungeboreshwa na kuzingatia teknolojia wangeweza kujiajiri, kuajiri vijana wengine lakini pia wangeweza kuchangia kikamilifu katika pato la taifa. Ndiyo maana leo napenda nijielekeze kuchangia ni kwa namna gani mfumo wa elimu unaweza kuboreshwa na kuzingatia teknolojia ili tuweze kufikia ajira milioni 8 ambazo tumeahidi katika Ilani yetu ya Chama Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tulipokaa hapa ukiangalia ulimwengu matajiri kumi wakubwa duniani saba kati yao wamepata utajiri aidha kwa njia ya mtandao (internet) ama kwa njia teknolojia bandia, sidhani kama ni Kiswahili sahihi ila wenzetu Wazungu wanasema artificial intelligence ama kupitia TEHAMA. Nikitoa mifano michache, ukimwangalia Jeff Bezos tajiri wa kwanza duniani amepata utajiri wake kupitia mtandao wa Amazon wa kununua na kuuza bidhaa anaingiza bilioni 127 kwa saa moja na ameajiri watu si chini ya laki moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, angalia na matajiri wengine ambao ni wadogo, Mark Zuckerberg tajiri mdogo kuliko wote duniani ameajiri watu 52,000 anaingiza mamilioni ya shilingi kupitia mitandao ya jamii tunayoitumia hapa kama WhatsApp, Facebook na Instagram.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia matajiri wengine wadogo kabisa Larry Page, Sergey Brin wote wanaingiza mamilioni ya shilingi kwa saa moja na wameajiri siyo chini ya watu 135,000. Siwezi kuwaelezea wote lakini taswira hii inatuambia teknolojia ndiyo mwarobaini wa changamoto za ajira za vijana wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni rai kwa Serikali ya chama changu kuweza kuangalia upya mifumo yetu ya elimu ili kuboresha masomo ya sayansi. Ubunifu unaanzia kwenye kujua ABCs za computer. Lazima tuboreshe masomo yetu ya sayansi yazingatie mafunzo ya computer kuanzia elimu ya msingi kwa sababu huko ndiko ubunifu unakoanzia na siyo kusubiria kuwafundisha watoto vyuo vikuu wakati vichwa vyao tayari vimekomaa. Matajiri wote hawa walipata mafanikio kwa sababu mifumo ya elimu iliwaandaa, iliwakuza kiubunifu na iliwasaidia na ndiyo maana wengi wao walivyofika chuo kikuu waliweza kubuni program hizi ambazo zinatatua changamoto za dunia za teknolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia leo vijana wetu wanaomaliza form four na form six mfumo wa elimu umewasaidia vipi? Mfumo wa elimu unapaswa kumsaidia kijana kwa ujuzi wa kujitegemea kwa ngazi yoyote anayoishia. Kinachosikitisha zaidi vijana wetu wa chuo Kikuu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JUDITH KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja. (Makofi)