Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Awali ya yote, naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha na mimi kuwa Mbunge katika Bunge hili lako tukufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa, niwashukuru kwa unyenyekevu mkubwa kina mama wa Tanga kwa kuniamini na kunifanya kuwa mwakilishi wao. Nami nawaahidi sitawaangusha na Mwenyezi Mungu anisaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchukua fursa hii pia kuwapongeza Mawaziri wote ambao wameanza kufanya kazi zao vizuri kabisa. Kipekee niwapongeze Mawaziri ambao wameshafika katika Mkoa wetu wa Tanga ili kuweza kutatua changamoto zetu wakiwemo Waziri wetu Mkuu, Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa na Naibu Waziri wa Maji ambaye amekuja kuwatua akina mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa, nimpongeze Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa hotuba nzuri ambayo ni mwendelezo na utekelezaji wa maono yake makubwa kwa taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 26 -28, Mheshimiwa Rais wetu amepanga kuimarisha miundombinu ili kukuza uchumi na sekta ya uzalishaji. Labda niseme kwamba Mheshimiwa Rais ana vipaumbele sahihi kwa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nathibitisha hili kwa usemi ama kauli ya Rais wa 35 wa Marekani, Rais John Kennedy mwaka 1961 aliwahi kusema kwamba: “American economy is good because of its infracture and not infracture of America is good because of its economy”. Natafsiri kwamba uchumi wa Marekani ni mzuri kwa sababu ya miundombinu yake na siyo miundombinu ya Marekani ni mizuri kwa sababu ya uchumi wake. Kwa hiyo, yule aliyekuwa akidanganya wananchi kwamba vitu siyo maendeleo amuulize John Kennedy tangu mwaka 1961 alisema kwamba miundombinu ndiyo mpango mzima na Mheshimiwa Rais amechagua vipaumbele sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika suala la miundombinu, Mheshimiwa Rais amepanga kuendelea na upanuzi wa bandari zetu. Labda niseme kwamba bandari ya Tanga imekaa muda mrefu ikiaminika kwamba kuna mwamba usioweza kuvunjwavunjwa na kina chake kuongezwa. Kwa mapenzi makubwa ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameweza kutenga takribani shilingi bilioni 172 na bandari ya Tanga imeongezwa kina chake tayari imekaribisha meli kubwa zimeweza kutia nanga. Watu wa Tanga tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hilo na tumempa kura nyingi za kishindo lakini tutaendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ili maono yake yatimie katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spia, lakini katika suala la upanuzi wa bandari, naomba kuishauri Serikali. Kupanua bandari ni jambo moja muhimu na zuri kwa kuwa bandari ndiyo uti wa mgongo wa taifa letu lakini ni lazima tujue kwa nini bandari zetu zinapoteza vina vyake.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii ya kubanua bandari zetu imeligharimu taifa fedha nyingi sana. Mradi wa Tanga ni shilingi bilioni 172 lakini upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam unaligharimu taifa shilingi bilioni 336, lakini kuongeza kina bandari ya Dar es Salaam takribani shilingi bilioni 200 na zaidi zitatumika.

Kwa hiyo, nashauri Serikali kama kweli inaamini bandari ndiyo uti wa mgongo wa taifa hili, ni lazima tufanye study kujuwa ni kwa nini kina cha bandari zetu kinapungua. Tunayo mataifa wahisani, JICA na KOICA tushirikiane nao ili kuhahikisha tunafanya study ya kina kujua ni kwa nini vina vya bandari zetu vinapungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatekeleza miradi hii mikubwa lakini kiukweli hatuna wataalam wa Port and Coastal Engineering ambao watashirikiana na wahandisi washauri kuweza ku- implement miradi ile accordingly. Niiombe Serikali yetu pia kama kweli bandari ndiyo uti wa mgongo wa taifa letu tuhakikishe tunawekeza kuhakikisha tunapata wataalam wa Port and Coastal Engineering kwa sababu watu wanaichukulia bahari kama ni kitu cha asili kwamba ni mgodi usiomalizika, this is very wrong concept.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma kidogo port and cost engineering university of Tokya…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshangonga Mheshimiwa.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)