Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kunipa nafasi ya kuweza kuongea mbele ya Bunge hili. Nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Busanda kupitia Chama Cha Mapinduzi walionipatia kura za kutosha na leo nawawakilisha kama Mbunge ndani ya Bunge hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia ya Bunge la Kumi na Moja, lakini katikati kulikuwa na achievement speech, ilikuwa katikati tarehe 16 Juni, kulikuwa na taarifa tena ndani ya Bunge hili ambayo Rais alionesha mambo yaliyofanyika. Mwezi Novemba tumekuwa na hotuba nyingine ambayo tunaizungumzia leo Bunge la Kumi na Mbili, Bunge letu la kwanza la Kumi na Moja lilionesha dira na falsafa ya Mheshimiwa Rais anakotaka kuipeleka nchi hii, lakini tarehe 16 Juni, alionesha yale yaliyofanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi wote ni mashahidi nikiwemo mimi kwenye taarifa hizi na kwa macho yetu, hakuna sekta aliyoizungumzia ambayo haikufanyiwa maboresho. Kama ni barabara, kiwango cha cha lami kimeongezeka, lakini kama ni barabara za TARURA zimeongeza, japokuwa zinaharibika kila mvua inaponyesha. Vituo vya afya vimeongezeka vimejengwa vipya 1,769, katika hivyo zikiwepo hospitali za mkoa, ikiwemo vituo vya afya. Hii inaonesha wazi kwamba dira na falsafa iliyokuwa imetolewa imetekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye hotuba hii ya Bunge la Kumi na Mbili ambapo ndipo kuna kazi kubwa tunatakiwa kufanya sisi, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais, yapo maono makubwa ambayo nimeyaona kwenye hotuba hiyo na wataalam kazi kubwa tuliyonayo sasa sisi kama Wabunge hasa nikiwemo mimi ni kwenda kuhamasisha yale yaliyoandikwa huko ndani yaweze kutokea. Kwa sababu hotuba ni kitu kimoja lakini utekelezaji ni kitu cha pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika sekta ya afya page namba 65 wameonyesha wazi kwamba sasa tunakwenda kwenye bima kwa wote. Mtego upo kwa Waziri wa Afya, tunapokwenda kwenye bima kwa wote kipi kilianza kati ya kuku na yai, ni kuku au yai? Inaanza kwanza huduma iwe bora ili watu wahamasike kuingia kwenye Bima ya Afya au bima ya afya kwanza ndiyo huduma iwe bora? Kwa hiyo, kuna kazi fulani wataalam wanatakiwa kuifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema kwenye ukurasa namba 44, STAMICO itaboreshwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wachimbaji wadogo wa madini wanasaidiwa. Kazi kubwa tuliyonayo ambayo naiona Rais ametuwekea mezani hapa, je, huduma hizi tunazotaka kuzifanya wataalam tulionao na sisi wenyewe tunazo service level agreement zetu? Kwa sababu inaonekana mwananchi anaweza kuwa huduma katika level yoyote, service level agreement ni ipi, kiwango gani cha huduma tunatakiwa tumpe, hapo ndiyo kuna changamoto. Tunaye Afisa Kilimo je, anakwenda kwenye shamba darasa na haya mashamba tunayoyazungumza hapa ndani ambayo yanaonekana yatakuwa ni mikataba kati ya wanunuaji na wakulima wenyewe yapo, anaweza kuwa haendi kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatakiwa service level agreement na watu wetu nini wa delivery. Kwa sababu unamuuliza mtu anakwambia nimeingia kwenye OPRAS, nimeingia sijui wapi, anaonekana anafanya vizuri lakini ukimuuliza kuna shamba darasa mahali hakuna. Kwa hiyo, mimi najielekeza kama Mbunge kuingia kwenye maeneo haya kuona namna gani tutafanya ili viongozi sisi pamoja na wataalamu wetu waweze kutoa kile ambacho Mheshimiwa Rais anatarajia hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo mambo mengi yaliyozungumzwa hapa ambayo nategemea yakifanyika tutakapokwenda kufunga Bunge hili tutakuta maendeleo yetu yamekwenda kasi. Ninao mfano mmoja mdogo, nilipokuwa natoka kwenye kampeni nafika airport Dar es Salaam nilimwambia mtu mmoja usinipitishe Ubungo kwa sababu tukipita huko wanajenga ile interchange itatuletea shida. Akaniambia wewe inaonekana ni wazamani sana kumbe barabara ilishakamilika, tukapita pale juu na bahati mbaya alikuwa ni mwanangu ananiambia baba wewe umepitwa na wakati, tukapita juu tukashuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, yapo mambo makubwa yamekwishafanyika, tutowe nafasi sasa na akili zetu kuhakikisha kwamba yale yaliyosemwa yanaweza kutokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nisitumie muda mrefu sana, naomba niunge mkono hoja, ahsante sana.