Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwa ufupi tu kuhusiana na maombi yangu ya kupandisha hadhi Chuo cha Maendeleo ya Jamii (FDC) kilichopo Tarime Mjini kuwa VETA. Chuo hiki kwa sasa kinatoa huduma kwa wananchi wa Tarime nzima Rorya na Serengeti. Hivyo ili kuendana na azma ya Serikali ya Tanzania ya viwanda ni lazima vyuo vya ufundi viwe vingi. Tumekuwa tukiomba chuo hiki kuwa cha ufundi ili tuweze kukidhi hitaji la muda mrefu wa kuwa na chuo cha ufundi, tutashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni wimbi kubwa la walimu toka Kenya wanakuja kufundisha shule binafsi za Tarime. Hiyo tunaomba Wizara iingilie kati maana tunao Walimu wa kutosha kuweza kuajiriwa, hivyo vibali vinatolewaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, uboreshaji wa elimu kuanzia sera za elimu, mitaala yetu pamoja na miundombinu yetu, inatoa taswira pana ya nini tufanye kama Taifa kwa ufupi tu. Tarime tumejenga Maabara hatuna vifaa wala wataalam wa maabara, tuna uhaba wa Walimu wa Sayansi na ndiyo maana watoto wanafeli. Tusiangalie Quantity tuangalie Quality. if we need to have quality education then input lazima ziwe effective. Madaftari, vitabu, madawa, madawati, walimu wenye motivation, nyumba za walimu na posho ya ziada, posho ya pango, posho ya safari na usafiri, kupandishwa madaraja, chakula mashuleni, ukaguzi wa shule zetu na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi ni hayo, mengi yamechangiwa naomba kuwasilisha.