Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pia naomba nami niungane na wenzangu kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye ametujaalia tumepata nafasi ya kuwatumikia Watanzania tukiwa wamoja katika Bunge hili Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumshukuru pia Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli. Huyu Rais amejidhihirisha hasa kuanzia kwenye uchaguzi wetu ambapo alihakikisha hata sisi wanyonge tunapata nafasi ya kufika hapa kupitia Chama Cha Mapinduzi ambacho anakiongoza kama Mwenyekiti wa Chama.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nidhahiri maneno mengi yanaweza yakasemwa juu ya huyu Rais, lakini nataka niwaambie Watanzania wote na Bunge hili Tukufu kuna wakati na mimi sitaki tufike huko tutakuja tujilaumu na kusema tunge, haya yasingetokea. Naomba tusifike huko tukafikia kwenye maneno ambayo Wanyakyusa wanasema pride comes after a fall. Naomba Watanzania na Bunge hili lifike wakati lijitathmini juu ya huyu Rais na ikiwezekana Wabunge tuungane, tufikie wakati tutoe tamko. Sio kwamba Rwanda ni wajinga walipofikia pale, sio kwamba Wachina ni wajinga walipofikia pale. Niwaombe Bunge hili, najua maneno haya wengi hawayapendi, lakini naomba tusifikie wakati wa kujilaumu tukasema tungelifanya hivi kwa huyu Rais basi Tanzania ingefika hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 imemfanya Rais wetuna Chama Cha Mapinduzi kufikisha asilimia 84.4. Ilani bora ya sasahivi ya Chama Cha Mapinduzi, naomba sasa ifikishe Rais huyu kuzidi miaka mitano ijayo.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie hotuba hii na kuunga mkono kwenye maeneo machache. Naomba nifike kwenye eneo la kilimo ambapo zao la cocoa ambapo ukiitaja cocoa unaisema Kyela moja kwa moja, ni zao ambalo limetufikisha hatua ya kujiona na sisi tuna dhahabu. Hata hivyo, zao hili kwa sasahivi halimnufaishi mkulima kupitia kitu kinachoitwa stakabadhi ghalani. Wataalam wetu hawajatufikirisha vizuri, wamelichukua desa lao kama lilivyo wamelihamisha. Wamedesa mfumo unaotumika kwenye mazao ya msimu wameleta kwenye mazao ya muda wote.Cocoa sio zao la msimu ni zao ambalo lipo muda wote wa mwaka na zao hili sio zao ambalo linalimwa kwenye mashamba makubwa, ni vivuli kwenye nyumba za watu. Watu wanaokota kilo moja moja, kilo tano tano. Sasa huyu mtu ukidesa mfumo wa korosho au kahawa ukauleta kwenye mfumo wa zao kama hili, unafeli nahapo ndiyo unapofeli mfumo huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye zao la cocoa sasahivi mtu anashindwa kusubiri siku nane za kuvundika cocoa ndipo akauze anaamua kuuza kwa Sh.2,500, wakati yule anayenunua mtu wa kati anapata zaidi ya Sh.5,000. Kwa kweli hili suala naomba kusema halijatusaidia wana Kyela na ni lazima tukae chini wataalam waishauri Serikali vizuri tuweze kutatua hili tatizo ili mnufaika awe ni yule aliyelengwa na ushirika ili suala la kumfanya apate faida yeye sio mtu wa kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kyela pia tunalima mpunga. Ni bahati mbaya sana, sasahivi kuna maneno yanaenea kwamba mchele wa Kyela umepungua ladha! Sio kweli. Ladha ya mchele wa Kyela ni ile ile ilakuna watu wanauza mchele wao kwa kutumia jina hilo. Naomba Wabunge na Watanzania wote waelewe mchele wa Kyela ni ule ule. Tunachoomba kwa Serikali sasa ni kwamba tuna mito minne mikubwa, sasa tunahitaji skimu za umwagiliaji ili tuwaoneshe mpunga wetu ulivyo bora ukiwa mwingi zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji ni tatizo kubwa sana, lakini naomba hebu tujikite pia kwenye sera zetu. Sera ya Maji inasema mtu asitembee zaidi ya mita 400, lakini kwenye kituo kimojawachote watu 250. Maana yake ninini? Maana yake nikwamba kwenye saa 12 ina maana wanatakiwa kuchoka watu 20 kila saa moja na kila dakika tatu achote mtu mmoja na hapo ni kwamba maji yachuruzike muda wote. Sasa naomba hili suala liangaliwe na wataalam ili kuweza kuweka vizuri na takwimu zetu zikae vizuri tofauti na zilivyo kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zetu sasahivi zinatia aibu. Mheshimiwa Rais anajitahidi kujenga barabara nzuri, lakini ndani ya muda mchache zinaharibika na tatizo lingine linaloharibu barabara ni kwamba viwango vyetu bado hatujaviweka vizuri, lakini bado tuna matatizo ya matuta barabarani. Hebu tujiulize, je mpaka sasa tunaingia kwenye uchumi wa kati tunahitaji matuta kudhibiti spidi? Matuta haya yanaharibu barabara lakini kwa uchumi wetu sio mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana niunge mkono hoja ya Mheshimiwa Rais kwa kusema Wabunge tujitathmini, sisi ndiyo walinzi wa Rais wetu. Ahsante sana. (Makofi)