Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa hii nafasi adhibu uliyonipa ya kuchangia hotuba wa Mheshimiwa Rais. Kwanza, namshukuru sana Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema kwa kunisababisha kurudi tena Bungeni kwa kipindi cha pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee nimshukuru mume wangu mpenzi Anold Wanyambelwa kwa kunisaidia kukaa vizuri na kuishi vizuri na Wajumbe mpaka Wajumbe wakanielewa. Nashukuru sana na Mungu akubariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wetu kipenzi kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Kafanya kazi mbili kwa wakati mmoja. Mheshimiwa Rais Mungu ambariki sana kwa sababu kwanza amefanya kazi ya kujenga nchi na uchumi wa Watanzania na sasa tumetoka kwenye uchumi wa chini, tuko kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kafanya kazi ya pili ya kukijenga Chama cha Mapinduzi kikaimarika kupitia kazi nyingi na nzuri alizozifanya zilizopelekea tukapata kura za kishindo. Mungu akubariki sana Mheshimiwa Dkt. Magufuli, Rais wetu kipenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania hatuhitaji Katiba Mpya bila maendeleo. Watanzania tulikuwa tunahitaji barabara tumeletewa barabara na Mheshimiwa Rais. Tena bahati mbaya jamani, pamoja na Ubunge wangu, yawezekana kidogo nimesababishwa kuwa mshamba na Mheshimiwa Rais nilipofika Dar es Salaam juzi nimepotea. Nimekutana na barabara nzuri sana ambazo zimetengenezwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Magufuli aliona ni vyema akafanya maendeleo kwa Watanzania; kajenga Vituo vya Afya. Badala ya kuchukua shilingi bilioni 400 na kuzipeleka kwa Wabunge wakae kwa ajili ya kujadili Katiba mpya, akaona ni vyema apeleke kwenye maendeleo ya wananchi. Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mungu akubariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunataka uzazi salama na siyo Katiba na sasa wanawake tunazaa salama. Ndiyo maana katika Bunge moja tu mimi nimezaa watoto wawili kwa kipindi cha miaka mitano na sasa niko salama. Mheshimiwa Dkt. Magufuli, Mungu akubariki sana. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Magufuli ameona zile shilingi bilioni 400 badala ya kutuletea sisi kujilipa wakati wa kujadili Katiba mpya, amesababisha tumepata maji vijijini. Mheshimiwa Dkt. Magufuli sasa wanawake umewatua ndoo kichwani. Mungu akubariki sana kwa kuimarisha ndoa za wanawake, kwa sababu ndoa nyingi zilikuwa zinavunjika kwa kufuata maji mbali, kusubiri maji na kukaa muda mrefu kwenye vituo vya kutafuta maji. Mungu akubariki sana Mheshimiwa Dkt. Magufuli, tunakuombea uendelee na mwendo huo huo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kipekee nimshukuru sana Rais wangu kwa kuwajali wajasiriamali wadogo wadogo, wakiwemo mama ntilie, bodaboda, baba lishe, mama lishe kwa kuboresha vitambulisho vyao hadi kupanda hadhi kuonekana kama vitambulisho vya Taifa ili na wao waweze kukopesheka katika mabenki pamoja na kampuni na mashirika mengine ya kifedha. Niseme Mwenyezi Mungu ambariki sanaMheshimiwa Magufuli adumu miaka 200. Ingekuwa siku zinarudishwa nyuma tungemrudisha nyuma sasa ndiyo akawa unaanza mwaka wa kwanza ili mbele bado miaka kumi inayofuatia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana ndugu zangu Mawaziri walioteuliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Mheshimiwa Magufuli kafanya kazi nyingi na kubwa sana kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Alifanya kazi kama Mbunge, kama Waziri, alifanya kazi kama Diwani na kiongozi wa chini kabisa na ndiyo maana tumesimama imara na ndiyo maana Chama Cha Mapinduzi leo tunajivuna kwa kazi nzuri Mheshimiwa Magufuli alizozifanya ambazo zimetusababishia kutembea kifua mbele na kupata ushindi wa kishindo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa basi kama alivyowaambia Mheshimiwa Rais sasa hivi wanatakiwa mfanye kazi. Hizo nafasi alizowapa ni deni sio kwamba eti amewachagua kwa sababu humu watu wengine hawatoshi, kuna wengine hapa tunawasubiria ili kusudi tu ushindwe kufanya kazi ili na sisi tupate nafasi hizo. Niwaombe sana, wamsaidieni Mheshimiwa Rais kufanya kazi kwa nguvu zote kwa juhudi, sasa hivi sio muda wa kukaa ofisini. Pia nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuwajali akinamama. Mheshimiwa Rais kwa kweli Mungu ambariki sana, sana na ndiyo maana sasa hivi wanawake wengi tuko Bungeni, tumekuwa asilimia kubwa sana lakini kwa wale waliokwenda majimboni wameshinda, ushindi wa kishindo. Kwa hiyo, tunasema wanawake tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana ndugu zangu, tunapokuwa tuna mihemko ya kisiasa tuiache pembeni sasa tufanye kazi kwa manufaa ya Watanzania wote. Fimbo aliyowachapa mwanzoni ndugu zetu wale rafiki zetu majirani msije mkaitamani tena maana kipindi kijacho wakiendelea kutoka nje maana yake hata wao wawili waliopo humu basi wataondoka jumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)