Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nitaanza namna hii; nasoma Hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati akilifungua Bunge mwaka 2015 alisema: “Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mchakato wa Katiba, Serikali yangu imepokea kiporo cha mchakato wa Katiba ambao haukuweza kukamilika katika awamu iliyopita. Akaahidi kwamba anatambua na kuthamini kazi kubwa ya kizalendo iliyofanywa na wananchi walioshiriki, hivyo ataiendeleza”.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo ni mwaka wa sita, nataka nimwulize au niiulize Serikali, mchakato wa Katiba mpya umefikia wapi? Habari ya Katiba mpya siyo yangu, siyo yako, wala siyo ya Rais, ni ya Watanzania wote ambao walishiriki mchakato mzima. Wimbi la kutaka Katiba mpya lilionekana kabla ya kuanza mchakato mzima ina maana ni hitaji la wananchi ambao wamekuwa wakilitaka muda wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme, demand ni kubwa, hauwezi ku-resist. Unaweza ukawa-suppress watu wasiongee lakini ukweli ni kwamba ahadi aliyoahidi Mheshimiwa Rais kwamba amepokea mchakato wa Katiba, ni lazima aitekeleze. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini nimeanza na Katiba? Ni kwa sababu tumeona changamoto kubwa. Mheshimiwa Rais katika hotuba yake ya 2015 na 2020 mara kadhaa ameongelea mchakato wa uchaguzi; ameongelea kushukuru na kuona mchakato ulivyoendelea, lakini mchakato wa Katiba ni mchakato wa wadau. Wadau wa Katiba ni Vyama vya Siasa, ni wananchi, lakini ni Tume. Sasa inafikiaje tunakuja kuona mdau mmoja ndiyo anaona kwamba mchakato ulikuwa ni huru na haki? Ukweli ni kwamba wananchi wanalalamika, wanaona mambo yalienda ndivyo sivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais anaipongeza Tume kwamba imeweza kubakiza fedha kati ya bajeti ya shilingi bilioni 331 iliyotengwa, ilitumia shilingi bilioni 232, kwa hiyo, ilibana matumizi. Tume ilibana matumizi kweli, lakini tuliona kwa vitendo Tume ambavyo haikuweza kufanya kazi sana.

(Hapa kengele ya kwanza ililia)

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, muda wangu naona umepunguzwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tume haikuweza kufanya kazi kubwa kama ambavyo ilitarajiwa. Tume ilikabiliwa na changamoto kubwa; huko chini tuliona maafisa au wasaidizi wa Tume wakigeuka na kuvaa nguo ya kijani badala ya kuwa wadau. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeingia katika uchaguzi ambao Tume ya Uchaguzi anapaswa kuwa referee. Hakuna mchezo ambao unakuwa huru na haki ambao player mmoja kama Simba au Yanga ione kwamba haki imetendeka. Siku zote watu wanamwangalia refa, hawana uhakika kama mchezo utachezwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niulize swali lingine, siku moja kabla ya uchaguzi tulishuhudia makaratasi mengi yamepigwa kura na kusambazwa mtaani, a day before. Nataka nijue majibu yakija, hizi karatasi zilizokuwa zimepigwa kura, zinasambazwa mtaani, mimi binafsi nilizikamata, zilitoka wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pengine Tume hawakufanya, labda ni Maafisa Wasaidizi waliopewa dhamana. Ndiyo maana tumekuwa tukisema tunahitaji Tume huru ili mshindi atakapokuja ndani hapa kila mmoja aguse kifua aseme, nimeshinda uchaguzi. Siyo tunasema umeshinda uchaguzi, kila mmoja ana wasiwasi kama ameshinda kweli. Hiyo ndiyo aina ya Tume huru tunayoitaka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine, tunatamani marekebisho makubwa katika Tume ya Kusimamia Uchaguzi. Wasimamizi Wasaidizi wengi wameonekana sio waaminifu. Hata hivyo, katikati ya mchakato tumeona kubadilishwa kwa Wakurugenzi kinyume na Kanuni za Maadili tulizozisaini, kitu ambacho hakikuwa sahihi. Hiyo ilikuwa ni utangulizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nirudi kwenye changamoto kubwa ambayo hata Mheshimiwa Rais ameisema. Kuna changamoto kubwa ya maji. Katika hotuba ya 2015 Mheshimiwa Rais aliahidi kumtua mwanamke ndoo. Mwaka 2020 nimesoma kwenye hotuba yake anasema: “Katika maeneo mengine Mheshimiwa Rais ameona watu wanalalamika kukosa maji. Bado kuna changamoto kubwa ya maji.

(Hapa kengele ya pili ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa kengele ya pili.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)