Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri na Naibu wake pamoja na timu nzima ya Wizara kwa kazi nzuri na hotuba nzuri ya bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia ya leo ni kama kijiji, hivyo suala la elimu ni muhimu sana kuliko wakati wote uliopita. Tulizoea kulinganisha ubora wa bidhaa (product competitions) kwa brand „nation brand‟ Elimu bora ni muhimu sana kwa nchi yetu kuwa na nation competitive advantage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza mindombinu na mitaala ya elimu iboreshwe kulingana na dunia ya leo. Napendekeza elimu kwa vitendo ianze toka shule za msingi elimu ya vitendo ijikite kwenye kilimo ufundi, ujasiriamali na TEHAMA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi za Mashariki ya Mbali, (tiger countries) zimefanikiwa sana kwenye uchumi wao kutokana na elimu bora ikiwa na nafasi kubwa katika orodha ya sababu za hayo mafanikio yao. Pamoja na muundo wa elimu ya nchi yetu napendekeza Wizara iweke mikakati ya kuboresha miundombinu na maslahi ya Walimu. Tunapoenda kwenye uchumi wa kati elimu ni muhimu sana hasa elimu inayowatayarisha vijana kujitegemea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.