Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na kimsingi naomba ninukuu maneno yafuatayo yaliyosemwa na Mheshimiwa Rais wakati analihutubia Bunge lako Tukufu. Alisema: “Nakwenda kuchangia kwenye maeneo mawili kwa kifupi sana. Nitumie fursa hii kuikaribisha sekta binafsi kuwekeza kwenye viwanda vya kutengeneza bidhaa za mifugo, nyama, ngozi, maziwa, kwato na kadhalika. Katika hilo tunaahidi kutoa vivutio maalum kwa watakaowekeza katika viwanda hivyo ambavyo vitasaidia kuinua vipato vya wafugaji wetu na pia kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania. Hapa nataka niweke bayana kuwa watendaji watakaokwamisha ujenzi wa viwanda tutawashughulikia”. Haya ni maneno ya Mheshimiwa Rais aliyatoa hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, nataka nilipe taarifa Bunge lako Tukufu, global practice na najua hii ni theory kwa international trade mahali popote duniani, Tanzania, Uganda, Kenya, Ethiopia, Somalia na ukisoma katika statistics za dunia Tanzania tumetajwa kuwa nchi namba mbili kwa wingi wa mifugo barani Afrika. Katika hili namuomba sana Waziri wa Viwanda atulie anisikilize lakini pia namuomba Waziri wa Uwekezaji atulie na kunisikiliza.

Mheshimiwa Spika, nataka nilipe Bunge lako Tukufu hotuba ya Rais iliyokuwa imejikita katika kulisaidia Taifa kupiga hatua katika masuala mazima ya viwanda, nimeamua kuchagua eneo dogo na kulifanyia utafiti eneo la mifugo. Angalia hiki kinachofanyika katika nchi yetu ya Tanzania ili kama sisi Bunge tuweze kutoa mchango wa kulisaidia Taifa na kuwasaidia wakulima na wafugaji wetu.

Mheshimiwa Spika, nakupa taarifa wewe na Bunge lako Tukufu gharama za uwekezaji na export ya nyama ambayo imeshasindikwa katika Taifa la Tanzania kwa kiwanda ambacho mtu amewekeza na ameajiri watu, kwa mfano, kiwanda cha Kenya, kilichowekeza na kuwa na uwezo wa kuzalisha kwa mfano nimechukulia mifugo, ng’ombe 1,000 kwa siku, Ethiopia nako ng’ombe 1,000 kwa siku Kenya na Uganda, angalia gharama hizi uone namna gani we are the witch of our own development. Nataka nikuambie wewe na Bunge lako Tukufu mipango ya Serikali na nia ya Rais najua asilimia mia moja ni nia thabiti ya kuhakikisha Taifa linapiga hatua lakini bado hatujafanya harmonization ya sheria, regulation zinakwamisha kupiga hatua kwa sekta nzima ya viwanda katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nakupa mfano, kiwanda kinachochinja ng’ombe 1,000 kwa siku Tanzania kikafanya uzalishaji wa ng’ombe 1,000 kwa kipindi cha mwaka mzima Kenya ili uweze kuzalisha ng’ombe 1,000 kwa mwaka mzima, gharama unazozilipa zile za kawaida tu achana na mambo ya tax, kuna kuja kulipa cooperate tax, PAYE na mambo mengine kwa Kenya inagharimu 1,900,000 kiwanda kinapata kama tozo tozo kutoka Serikalini. Ethiopia kiwanda kinachozalisha nyama ya ng’ombe 1,000 kwa siku, kwa mwezi, kwa mwaka wanalipa 1,008,000.24. Uganda wanalipa 1,900,000. Njoo kwa Tanzania na hii nataka nikuambie na Waziri wetu Mkuu yupo hapa state intervention katika kulinda viwanda vinavyowekezwa na Watanzania au investors wanaotoka nje imekuwa changamoto kubwa kwa Taifa letu. Ndiyo maana tunajenga viwanda vinakaa mwaka mmoja vimekufa, state intervention.

Mheshimiwa Spika, kwa Tanzania kuna bodi na matitiri mengi naomba niyasome uone picha na ninyi Mawaziri mliopo hapa mkasaidie kufikisha vision ya Mheshimiwa Rais katika sekta ya viwanda. Kwa Tanzania kuna kitu kinaitwa livestock and fisheries, ukizalisha nyama kila kilo wanaku- charge shilingi 150 wanasema gharama zao.

Mheshimiwa Spika, cha pili, kuna kitu kinaitwa Bodi ya Nyama, Mawaziri nyie mpo hapa kama nasema uwongo prove me wrong, nimefanya utafiti. Kuna kitu kinaitwa Bodi ya Nyama they take one percent ya FoB kwenye production ambayo imezalishwa na kiwanda. Kuna kitu kinaitwa Chamber of Commerce wanachukua shilingi 55,000 kila certificate per consignment ambayo inakuwa exported. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukifanya calculation mwekezaji atakayekwenda kuwekeza kwenye kiwanda cha kuzalisha nyama kwa mwaka mmoja kwa Tanzania nje ya cooperate tax na mambo mengine analipa fedha zisizopungua 860,000,000 wakati Kenya mtu analipa 1,000,000 peke yake. We cannot survival, hatuwezi ku-survival Mawaziri wangu na ndiyo maana viwanda vingi vinafunguliwa tunapiga makofi tunafungua viwanda haviwezi kukabiliana na ushindani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu wanafanya state intervention na maana ya state intervention ni kwamba wawekezaji wanapoingia na Rais hapa nimeisema vision ya Rais wa Nchi, vision ya Rais wa nchi anasema tutatoa some sort of incentive katika viwanda, lakini wito wangu ninaotoa kwa Serikali yangu sikivu, ndiyo maana mnalalamika hapa, amesema kaka yangu pale, mbuzi wanakwenda kuuzwa Kenya, kiwanda wanawezaje ku-compete na Wakenya, Mkenya mimi juzi nilikuwa Dubai niliamua tu kufanya survey,nimekwenda nyama zote Dubai zinaandikwa imported from Kenya wakati Kenya hawana mbuzi. Afrika nchi zenye mbuzi hata Ethiopia tunawasifu, lakini hawana mbuzi, Ethiopia wanakondoo, mbuzi wanatoka Tanzania na kiasi kidogo Somalia.

Mheshimiwa Spika, ninachokwambia nenda kwenye masoko ya nje,kama utakuta kuna nyama imeandikwa imetengenezwa kutoka Tanzania, hakuna nahii nawaambia Mawaziri wa Mifugo, wasisubiri Rais Magufuli aje atoe matamko wachukue hatua. Yaani if I was the Minister, today ingetoa declaration ya kuhakikisha tozo zote ya ovyo zinazokwamisha viwanda vya nchi hii na kufanya Watanzania wanakosa ajira, ni bora utumbuliwe umefanya maamuzi kwa maslahi ya Taifa. Wafanye kazi Mawaziri wangu, wasiogope Rais yupo nyumayao. Mheshimiwa Mwambe you are Minister kaka yangu tunakuamini, bado kijana mdogo tunajua uwezo wako, shirikiana na Wizara ya Mifugo saidieni Taifa hili kwa mustakabali wa Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, la pili, Rais jana alizungumza, nilisikiliza hotuba yake na hiyo pia iko katika packageya hotuba aliyotoa hapa Bungeni, suala la uwekezaji tuna changamoto kubwa sana, naomba nikwambie, kazi inayofanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu hakika tunaweza tusiitambue kwa sababu kuna mambo mengine tunaweza tusiyaone Waziri Mkuu na Ofisi yake wanafanya kazi nzito sana katika kusaidia uwekezaji kwenye Taifa hili.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nilipe Bunge lako Tukufu taarifa, Rais jana alipokuwa anatoa takwimu watu wanakwenda kwenye benki wanakopa hela kubwa sana za kuwekeza, wanakimbilia mahakamani. Natoa mfano mdogo sanasana, nenda kachukue takwimu za iliyokuwa Bank M take statisticsangalia list ya watu waliokwenda kuchota bilioni za shilingi za Watanzania mle halafu uwekezaji fedha zimetoroshwa sijui Canada, sijui Kenya na mpaka leo ninavyokwambia its true Ofisi ya Waziri Mkuu imefanya kazi kubwa sana angalau kuna bilioni 200 zimeokolewa kupitia Bank ya Azania.

Mheshimiwa Spika, hili nalisema kwa uchungu kwa sababu hapa Bungeni tunayo Kamati inayoshughulikia Uwekezaji na Mitaji, sina maana waanze kufukua makaburi kujua nani kakopa, lakini ukiangalia kwenye list ya waliokopa, mbaya zaidi hukuti mtu wa ngozi ya namna yangu,I am very sorry to say this, tunaweza tukapigiana kelele na Wabunge hapa vimikopo tunachukua vidogo vidogo kwenye taasisi za fedha, nataka niseme with confidence na with evidence,Taifa hili bado linapigwa sana. Wizi wa rasilimali za nchi bado haujakoma kwenye nchi hii, lazima kama Bunge tudhamirie kwa dhati kusaidia vision ya nchi, Rais atiwe moyo na Bunge sisi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)