Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi hii ambayo nimeweza kuipata kwa ajili ya kuchangia hii hoja iliyopo mbele yetu ya hotuba ya Mheshimiwa Rais. Nami kama wengine walivyoanza naomba pia nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa hotuba yake nzuri ambayo imejenga na ina dira ambayo ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nina hoja chache sana kwa sababu nyingi zimeshazungumzwa na waliotangulia, nitachangia kidogo kwenye kilimo kwa sababu naona wengi wameongelea kilimo; upotevu wa baadhi ya mazao ya kutoka kwenye kilimo yameongelewa zaidi, sehemu za kuhifadhia kwamba ni moja ya sehemu inayofanya kuwe na hiyo harvest loss ya 30 percent to 40 percent ambayo imetajwa kwenye ukurasa wa 14 wa hotuba ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, pia nadhani mbegu zinachangia sana katika upotevu wa mazao. Kwa mfano kwenye mahindi kuna mbegu ambayo ipo sasa hivi ambayo hata kama imekomaa yule mkulima akichelewa kidogo tu kuivuna anakuta kwamba tayari yale mahindi anavuna yakiwa yameoza, lakini ile ni ubora wa ile mbegu. Wizara hii ya Kilimo inafanya kazi nzuri sana lakini kwenye suala la mbegu bado kuna changamoto kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la reli; ni kweli sasa hivi reli inajengwa kwa kasi kubwa na hasa SGR, lakini pia tunahitaji ile reli ya zamani kuendelea kuwepo kwa sababu nafahamu kwamba hii reli ambayo sasa hivi ni ya kisasa hata kama itakuwa imekamilika, bado kuna shughuli za usafirishaji zitaendelea kuwepo kwa kutumia reli ya zamani. Kwa hiyo kuna umuhimu sana wa kuimarisha reli ile ya zamani na hasa maeneo ambayo tumekuwa kila siku tukiyasikia miaka na miaka, maeneo ya Kilosa yale nadhani ni Gulwe na maeneo mengine ya Godegode, kila mara reli inachukuliwa na maji na inaigharimu Serikali hela nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, sasa nadhani wakati umefika Serikali ibuni namna gani itafanya hata kama itatumia fedha nyingi sana kuinua matuta makubwa kwenye hii reli ya zamani ambayo ile treni itapita juu kabisa isikutane na yale maji, kitu ambacho kitakuwa sustainable, sio hii ya kila siku zinapelekwa billions za fedha pale, lakini kila mwaka mvua ikija eneo lile reli inachukuliwa.

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee suala la miradi ambayo Mheshimiwa Rais amekuwa akiisimamia ambayo kwa kweli hata Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi ufanyaji kazi wa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli na miradi ambayo imeibuliwa na inaendelea imetubeba sana hata kwenye uchaguzi uliopita.

Mheshimiwa Spika, hii miradi ni endelevu, sina uhakika kama miradi yote hii kwa mfano ya nishati ile ya Bwawa la Mwalimu Nyerere kule lakini nimetoka kuzungumzia SGR na miradi mingine mikubwa; miradi hii sijui kama inaweza ikaisha yote kabla Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, hajamaliza kipindi chake. Kwa kuwa Mheshimiwa Rais anaiheshimu sana Katiba na ameshazungumza kwamba yeye hatoongeza kipindi, ataondoka, sasa yeye yuko very strong lakini ile miradi iko protected namna gani, ile miradi mikubwa aliyoianzisha itaendelezwa kinamna gani?

Mheshimiwa Spika, hapa hoja yangu ni kwamba tunatakiwa tujifunze kutokana pia na matukio ya wenzetu. Hivi karibuni baada ya uchaguzi wa Marekani, siku ya kwanza tu Joe Biden alisaini executive orders za ku-revise vitu alivyovifanya Trump, the same day ambayo aliapa alisani. Kwa hiyo ina maana yeye katika kipindi chote kuna vitu ambavyo alikuwa hakubaliani navyo, alikuwa anasubiri tu akiingia avibadilishe.

Mheshimiwa Spika, sasa naongelea hili kwenye miradi mikubwa ambayo Mheshimiwa Rais ametuanzishia na inakwenda vizuri na ni muhimu sana kwenye kujenga uchumi wa nchi yetu; iko protected namna gani? Ili asije akaingia mtu, maana yake kwa sasa Mheshimiwa Rais yuko madarakani kila mmoja anam-support, lakini mioyo yetu tunaifahamu wanadamu, kubadilika ni wakati wowote. Hatujui, je, miradi hii itaendelezwa akiondoka? Sasa mimi pendekezo langu hapa ni kwamba ikiwezekana ziimarishwe institutions ambazo zitalinda hii miradi ili isije ikaguswaguswa na wengine watakaokuja mpaka iishe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukizungumza hivyo unaigusa kidogo Katiba, lakini nimewahi kusema hapa kwamba Katiba sio Msahafu au Biblia, hata Mheshimiwa Rais wakati anaingia nakumbuka kwenye hotuba yake ya kwanza alipokuja hapa aligusia Katiba na hakuna mahali aliposema kwamba labda Katiba ile haifai. Labda ninukuu kidogo kwenye ukurasa wa 12 wa Hotuba ya Mheshimiwa Rais ya mwaka 2015; naomba ninukuu, anasema; “Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mchakato wa Katiba Serikali yangu imepokea kiporo cha mchakato wa Katiba ambao haukuweza kukamilika katika Awamu iliyopita kutokana na kutokamilika kwa wakati kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura.

Anaendelea, anasema; napenda kuwahakikishia kuwa tunatambua na kuthamini kazi kubwa ya kizalendo iliyofanywa na wananchi walioshiriki hatua ya awali ya ukusanyaji wa maoni kuhusu Katiba mpya. Pia tunatambua kazi nzuri ya Tume ya Marekebisho ya Katiba na Bunge la Katiba lililopita lililotupatia Katiba inayopendekezwa. Tutatekeleza wajibu wetu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Marekebisho ya Katiba; napenda mtuamini hivyo.”

Mheshimiwa Spika, naomba ili miradi hii asije akaichezea atakayekuja tuangalie utaratibu, hata kama utakuwa ni wa Azimio la Bunge.

SPIKA: Mheshimiwa Mwakasaka.

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, naam!

SPIKA: Hii ajenda ya sijui nani ataondoka, nani atakuja siipendi sana kwa sababu tunaishia kuwatia hofu wananchi; tuamini Mungu ni mwema na tupo na Rais yupo. (Makofi)

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, mimi hoja yangu hapo ni kwenye namna gani tutailinda hii miradi ili isije ikaishia njiani. Ndiyo maana nilitoa mfano huu wa Marekani, kwamba kwa mfano Trump angekuwa amepewa wigo mpana wa kugusa vitu vingine, maana yake aligusa vidogovidogo tu, zile executive orders, Biden akaweza kuzibadilisha, lakini Trump hakuwa mtu wa kawaida, lakini kuna vitu alizuiliwa kwenye Katiba asiviguse. Kwa hiyo, maana yangu hapa ni kuzi-strengthen institutions kwa mfano Mahakama na Bunge.

Mheshimiwa Spika, leo kwa mfano Bunge tukiazimia hapa kwamba miradi fulani ambayo ni ya kimkakati hata likija Bunge lingine isibadilishwe au isisimamishwe na kama itakuwa iko kwenye Katiba yule mtu hatogusa hii ndiyo concern yangu. Kwa sababu hii ni legacy kubwa Mheshimiwa Rais atakapoondoka ataiacha, miradi hii aliyoianzisha ni very productive kwenye economy lakini…

SPIKA: Yaani hoja yako naielewa, tunaielewa vizuri sana.

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

SPIKA: Kwa mfano Makao Makuu ni Dodoma, hatutarajii tena aje mtu mwingine aseme ana Makao yake Makuu Sumbawanga au mahali pengine.

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, iko protected wapi? Akija mtu akisema anataka kurudisha Dar es Salaam?

SPIKA: Ahsante sana, bahati mbaya sasa na muda nao umekuwa…

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naunga mkono hoja.