Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Nichukue nafasi hii pia kukupongeza sana wewe kwa jinsi ambavyo unaongoza Bunge hili, lakini nichukue nafasi hii sana kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo amewasilisha hotuba yake na jinsi ambavyo amehakikisha ametekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, hasa kuanzia 2015 hadi 2020.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais ameonesha umahiri mkubwa sana katika jambo hili. Ukiangalia jinsi ambavyo ameanza katika mwaka 2015 hadi kufikia 2020, watu walikuwa wameanza kusema labda ni nguvu ya soda, lakini kwa kweli, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, amefanya kazi kubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais ameifanya katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na wasaidizi wake kwa kweli, hatuna sababu ya kutokuwapongeza, lakini katika kupongeza huko nakumbuka maneno yako ulikuwa siku moja umesema, Spika wa Bunge la Kenya alisema Mtanzania akisimama, anapongeza halafu anakaa chini, lakini utamaduni wetu Watanzania ni kupongeza. Mtu wa Kenya akienda dukani anasema nataka chumvi hasemi naomba, kama sisi Watanzania.

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa pongezi, niende kuchangia kwenye maeneo mawili matatu, kama wenzangu ambavyo wamechangia. Naenda kwenye afya; Wizara ya Afya imefanya kazi kubwa sana. Katika Jimbo langu la Arumeru Magharibi tunaishukuru Serikali sana kwa kutuletea fedha kwenye vituo vya afya. Kituo cha Afya cha Nduruma kimepata milioni 500, Kituo cha Mbuyuni milioni 400, Kituo cha Musa kimepata milioni 200; hii ni kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais katika kipindi chake ameboresha afya, amefanya kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, bado kuna changamoto kubwa katika Jimbo langu la Arumeru Magharibi. Zahanati nyingi tumewahamasisha wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi kwa ajili ya kujenga kwa dhana ile ya kila kata, kila kijiji kujenga zahanati kufikia lenta, kwa maana ya maboma, ili Serikali iweze kumalizia. Naomba kuishauri Serikali, hasa Wizara ya Afya, ni lini sasa itamalizia hayo maboma ambayo wananchi wamejenga katika kuwahamasisha, ili basi lile lengo la kila kijiji kuwa na zahanati, ili hizi zahanati zikamilike?

Mheshimiwa Spika, katika jimbo langu kuna zahanati nyingi sana kama 11 katika Vijiji vya Ilkerin, Bwawani, Kigongoni kule na kadhalika. Hii itasaidia sana kukamilisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi kama Mheshimiwa Rais wetu anavyojali katika masuala ya afya.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Wizara ya afya kwamba, badala ya kuwapa wazee kitambulisho, ni kwa nini sasa Serikali isije kwenye sera yake irekebishe wazee wapewe bima ya afya kama watu wengine. Kwa sababu, katika kupewa vitambulisho hawapati huduma ipasavyo. Hilo nalo naomba Wizara hiyo iliangalie.

Mheshimiwa Spika, suala la upungufu wa Madaktari; hili nalo naomba Serikali ijaribu kuangalia kwa sababu, unakuta Nesi katika baadhi ya maeneo, Serikali imejitahidi sana, lakini bado kuna upungufu katika maeneo machache. Ningeomba Serikali irudie tena kuangalia maeneo hayo kwa ajili ya kupatikana kwa Madaktari katika vituo vyetu vya afya.

Mheshimiwa Spika, suala la barabara. Serikali imejitahidi sana, nchi hii ni kubwa, lakini Serikali imejitahidi kuhakikisha kwamba, imeunganisha wilaya na wilaya, mikoa na mikoa, lakini naomba kuna ahadi ambazo Mheshimkwa Rais pamoja na viongozi wengine wameweza kutoa katika ziara na hasa wakati wa kampeni, basi katika bajeti ijayo barabara hizo zikumbukwe. Kwenye jimbo langu kuna barabara ambayo imefanyiwa tathmini kwa mfano barabara ya Arusha – Mirongoine – Tera kwenda Kongwa. Naomba hii barabara katika bajeti hii isisahaulike.

Mheshimiwa Spika, kuna barabara ambayo tumeahidiwa pia na Mheshimiwa Rais, Barabara ya Mianzini – Timbolo kutokea Sambasha kwenda Ngaramtoni, hiyo ni barabara ya kilometa 18, Mheshimiwa Rais aliahidi kwa kiwango cha lami. Naomba Wizara husika isisahau kwenye bajeti hii; vile vile barabara ya kwenda Hospitali ya Oturumet, Hospitali ya Wilaya, kilometa tatu; na barabara ya kwenda Hospitali ya Seliani, kilometa tatu. Hayo ni maeneo ya huduma ambayo wananchi hawa wanahitaji kwa ajili ya kupata huduma bora. Pamoja na hayo tunaendelea kuipongeza Serikali kwa sababu, kwa kweli inajitahidi kwa kadiri ilivyoweza kuwafikia wananchi wake.

Mheshimiwa Spika, niingie kwenye suala la ajira; vijana wetu wengi wanakosa ajira, lakini Serikali imejitahidi kuimarisha sekta binafsi na hata ndani ya Serikali katika kuajiri vijana wetu. Ushauri wangu kuna Mfuko ule wa Akinamama na Vijana na watu Wenye Ulemavu; naishauri Serikali iangalie hiyo Sera ya Mfuko huo kwa sababu, utakuta vijana kuanzia miaka 18 mpaka 35 ndio wanaostahili kupata huo mkopo kwenye halmashauri zetu, lakini ukienda mbali zaidi ukiangalia watu wanaoweza kufanya biashara vizuri ni kuanzia miaka 18 mpaka angalau 40 mpaka 45.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Serikali iangalie hiyo sera, ili kwa sababu ya ukosefu wa ajira kuanzia 18 mpaka 45 waweze kuingizwa kwenye sera ili waweze kupata hiyo mikopo. Hata hivyo, tunaendelea kuishukuru Serikali kwa sababu, imeondoa riba kwenye Mfuko huo na sasa wengi wananufaika isipokuwa upande wa vijana kuna changamoto kidogo kwa sababu ya hayo mambo magumu. Naomba pia, kuishauri Serikali kuangalia uanzishwaji wa vokundi kuanzia watu watano mpaka na kuendelea. Kwa sasa hivi ni watu 10, wananchi bado wanaona kidogo inawawia vigumu kuanzisha hivyo vikundi kuanzia watu 10 na kuendelea, lakini wakati ule ilikuwa watu watano angalau wananchi wanapata kujiunga vizuri na kuanzisha vikundi kwa ajili ya ujasiriamali. Nina uhakika eneo hili likiboreshwa suala la upungufu wa ajira ambalo kila siku sisi Wabunge na hasa mimi ninavyozungumzia kwenye jimbo langu, kila siku wananchi wananchi wanasema tutafutie ajira. Eneo hili tukiliboresha vizuri nadhani kwamba, wananchi wetu watapata ajira.

Mheshimiwa Spika, suala la NIDA; Mheshimiwa Rais katika hotuba yake alisema ataboresha vitambulisho vya Wamachinga na baadae viwe kama vya NIDA, lakini naomba watu wanaohusika na NIDA hasa Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa kweli, wananchi wanateseka sana katika maeneo mbalimbali kupata huduma kwa sababu ya ukosefu wa vitambulisho hivyo vya Taifa. Hebu iangaliwe kwamba, kuna nini hasa kinachopelekea mpaka wananchi hawawezi kupata vitambulisho kwa wakati, ili waweze kupata huduma. Hasa ukizingatia kwamba, kitambulisho cha Taifa kwa sasa wananchi walio wengi wanahitajika kuwa nacho kwa ajili ya kupata huduma katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, suala la maji; kwanza niishukuru Serikali kwa kutupatia mradi mkubwa wa maji wa bilioni 500 katika Jiji la Arusha ambao unahudumia hasa katika jimbo langu na maji hayo yametoka kwenye jimbo langu. Mheshimiwa Rais alikuja kuzindua mradi huo mkubwa kwa kweli, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa sababu ameonesha ni kiongozi ambaye watu. Ninachoweza tu kusema hapa naomba sasa niikumbushe Wizara iangalie yale maeneo ambayo Mheshimiwa Rais ameahidi, ili maji yaweze kuwafikia waweze kupata. Kwa mfano maeneo yale ya Floraid, Lemong’o, Lemanda, kule Ngutukoit, Losinoni Juu, Losinoni Kati mpaka huku chini kuja Oldonyosambu. Naamini Wizara itajitahidi kwa jinsi ambavyo inamuunga Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, la mwisho, suala la ulinzi na usalama wa wananchi wetu. Kama tunavyojua Serikali yoyote duniani ni Serikali ambayo inahakikisha wananchi wake wanaishi kwa salama na amani. Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli imefanya kazi kubwa sana ukizingatia katika kipindi hiki chote cha miaka mitano uhalifu umepungua kwa kiwango kikubwa mno.

Mheshimiwa Spika, nina tatizo kidogo la kushirikiana. Nimwombe Waziri anayehusika wa Ulinzi, kuna mgogoro mkubwa sana na Waziri wa Maliasili, kuna mgogoro ambao haujakaa vizuri kwenye jimbo langu. Ningemwomba Waziri angefika kule kwenye Msitu wa Meru. Wananchi kule…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)