Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nianze kwa kuunga mkono hoja iliyosomwa hapa Bungeni na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa umahiri mkubwa kabisa lakini niwapongeze pia mawaziri wote na watendaji katika ofisi yake.

Mheshimiwa Spika, nitajikita kwenye hoja tu moja kubwa ambayo ilisemwa karibu na wachangiaji wote na ni hoja ya corona.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niseme ni kweli mlipuko wa virusi vya corona licha ya adhari kubwa za kiafya umekuwa ni tishio kubwa kwa mafanikio ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika bara la Afrika lakini pia na dunia nzima. United Nations economic commission for Africa wamekadiria kwamba ukuwaji wa uchumi wa bara letu la Afrika unaweza kuanguka kwa kati ya asilimia 2 mpaka 3 katika mwaka huu 2020.

Mheshimiwa Spika, lakini Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) tayari wameshatangaza kwamba uchumi wa dunia unaingia kwenye mdororo katika mwaka 2020, economic research. Sasa sisi kama nchi kama zilivyo nchi nyingine tumeanza kupata madhara katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na Waheshimiwa Wabunge wengi waliochangia wamezisema sehemu mbalimbali hususani upande wa utalii kuna shida kubwa na mnyororo mzima wa sekta ya utalii, lakini mapato yanayotokana na biashara mbalimbali ndani na nje ya nchi tunaona tatizo, lakini pia usafiri wa anga biashara za maua tunaona shida uzalishaji viwandani nk.

Mheshimiwa Spika, lakini kubwa kutokana na hali hiyo Serikali imeunda kikosi kazi cha wataalam ambacho kinaendelea kufanya uchambuzi wa kina wa athari hizi zinazojitokeza na niseme tu kwamba hii kazi ni muhimu ikafanyika kwa umakini na ndiyo iweze kuwa msingi wa kuandaa programme ya kiuchumi ya kukabiliana na janga hili vinginevyo tunaweza kuishia alarmist lakini bila fact kutoka kwenye sekta mbalimbali ili tuweze kuhakikisha tunaanda mikakati ambayo kweli ni hakika na timu hii inajumuisha wenzetu kutoka Zanzibar wako kwenye kamati ya kitaalam lakini pia kwenye kamati ya kitaifa ambayo inaongozwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini vile vile, katika Wizara yangu tumeelekeza pia na Wizara zote za kisekta ikiwemo benki kuu kukutana na wadau mbalimbali kwa majadiliano ili tupokee mapendekezo yao na baadhi tumeshapokea Tanzania Association of two operators, tumepokea kutoka Umoja wa Mabenki Tanzania Hurting operatos, Shirikisho la Vyama vya Utalii, Tanzania Private sector foundation, kuna ma casino kadhaa lakini Tanzania horticulture Association na wadau wengine na tunawashukuru sana kwa michango yao milango iko wazi tunaomba na wengine watuletee mapendekezo yao katika Sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nitakacho fanya sasa, naomba nitoe tu vidokezo vya mikakati ambavyo inaandaliwa hivi sasa na viko katika sehemu tu kuu tatu. Sehemu ya kwanza ni ugharamiaji wa mahitaji ya msingi ya vifaa ya kujikinga na corona lakini pia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya kutokea huduma za afya ili ni jambo la msingi sana ili tuweze kuokoa maisha ya watu wetu kwa hiyo maana yake ni kwamba ni pamoja na vituo mahususi vya kutolea huduma, tiba za dharura lakini pia lengo kubwa likiwa ni kuzuia maambukizi ya corona kwa hiyo, lazima tufikirie gharama za vifaa kinga person protective equipment masuala ya barakoa, ventilators, gaunt za wahudumu wa afya na madaktari na n.k.

Mheshimiwa Spika, ikiwa ni pamoja pia na gharama za kutafuta namna ya kuongeza madaktari na watumishi wengine wa afya kwa hiyo, hii ni block ya kwanza na vyanzo vya kugharamia eneo hili ambavyo tunafikiria ni pamoja na bajeti kuu ya Serikali hususani kasima ile ya dharura, mapato ya halmashauri michango ya hiari ya wananchi, makampuni binafsi na umma, misaada ya fedha na vifaa na mikopo nafuu kutoka kwa taasisi za fedha za kimataifa.

Mheshimiwa Spika, pia nchi rafiki na ninapenda nitumie nafasi hii kama mfano tu kutambua mchango wa Twiga Minerals Cooperation Limited ambayo tayari wameahidi kutoa mchango wa dolla za kimarekani 1.8 milioni ambazo zitatumika kusaidia Isolatin Untis Mlonganzila na vituo vingine vya karantini, mabibo hostel. Lakini pia kusaidia Isolation centre Musoma, Shinyanga na Geita, pia ziko fedha kwa ajili ya kusaidia shughuli za kupambana na janga hili katika ngazi za local Government na tunawashukuru sana kwa dhati na tunaomba na wengine waige mfano huu mzuri makampuni mengine, mabenki, taasisi na wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali pia inaendelea kushauriana na IMF na benki ya dunia kuhusu namna nchi yetu inaweza kunufaika na programme za dharura za Taasisi hizo ili kukabiliana na hili janga. Kwa upande wa World Bank na IFS wana programme inaitwa Fast track COVID – 19 facility na IMF wana rapid crediting facility for low income country’s tunaendelea na majadiliano tuone namna ambavyo Tanzania inaweza ikanufaika na sehemu hizi.

Mheshimiwa Spika, nguzo ya pili, ni kupunguza makali ya mdodoro wa uchumi hasa katika sekta ambazo zimeadhirika na nimeshayaeleza, sekta ambazo tayari kuna dalili za kuumia kwa hiyo, hatua ambazo tunafikiria ni pamoja na kuhakikisha hifadhi ya chakula ya kutosha nchini, kuchukua hatua za kibajeti ikiwa ni pamoja ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi katika baadhi ya maeneo na kuzielekeza kuongeza nguvu kukabiliana na corona, lakini kukarabati miundombinu ya usafirishaji ili tuweze kuwafikia wananchi wetu hasa walioko vijijini lakini tutaongeza kasi ya kulipa madeni na malimbikizo ya madai mbalimba lakini pia kuchukuwa hatua za kikodi na za kiutawala zinazolenga kutoa huweni kwa sekta binafsi.

Mheshimiwa Spika, nguzo ya tatu ya mpango ambao unaandaliwa, ni hatua ya kuilinda sekta ya fedha na lengo ni kuhakikisha mabenki yetu yanaendelea kuwa na ukwasi wa kutosha tuna akiba ya fedha ya fedha ya kigeni ya kutosha lakini sarafu pia iendelee kuwa imara na itakuwa ni muhimu tudhibiti ongezeko kubwa la mikopo chechefu lakini hususani kwa kuwapa nafuu mabenki…

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Malizia.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mhehsimiwa Spika, tutatoa unafuu kwa mabenki ili yaweze kufanya loan rescheduling kwa maelezo hayo machache, nilitaka tu niliakikishie tu Bunge lako tukufu kwamba Serikali ipo kazini kuandaa mpango wa kupambana na madhara ya corona ya kiuchumi na muwe na uhakika tutakapo kamilisha tutawasilisha kwa maamuzi ndani ya Serikali na Bunge litapata taarifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru naunga mkono hoja. (Makofi)