Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwepo na utaratibu wa kurudisha vyeti vya vyuo kwa wale wanaopotelewa vyeti vya NECTA pale aliyepotelewa akiwa na ushahidi usiotia shaka wa kupotelewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ada elekezi za shule hazitekelezeki labda vitu kama michango ya majengo kwa shule binafsi yapigwe marufuku. Private investiment inawahusu vipi wazazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kuanzishwe Bodi ya Elimu na Walimu wasajiliwe na wawe responsible nayo hasa mambo yanayohusu maadili. Vyuo Vikuu viwe categorized kwa level zake lakini viwe na specialize hata kama kutakuwepo na kozi nyingine zaidi, lakini chuo kijulikane kwa specialization moja au mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Sera ya Elimu iangaliwe upya, kwani jamii tuliyonayo leo ya vijana kutopenda kazi, kusema uongo na unafiki ni zao la sera isiyokuwa na dira ya wapi tunaenda na nini tunataka ku-achieve.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwango kisichoridhisha cha mshahara wa shilingi 570,000/= haiwezi kukidhi maisha ya mtu, lazima Serikali ibuni njia nyingine za kuwasaidia Walimu vitu kama Transport Allowance, Accommodation Allowance na Teaching Allowance.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upandishwaji wa madaraja kwa Walimu unachukua muda mrefu sambamba na malipo ya vyeo hivyo vipya.
Vile vile nashauri kuwepo na chombo cha kusikiliza rufaa za wanafunzi ambao huwa wanakata pale wanapokuwa hawajaridhishwa na usahihishaji wa NECTA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima Wizara ibuni namna nyingine ya kutambua uwezo wa wanafunzi kwani njia moja tu ya mtihani siyo sahihi. Pia kuna uwezo na vipawa mbalimbali nje na kukariri majibu ya mtihani, kila mtu awe awarded kwa uwezo wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wa Nursery School wasajiliwe na watambuliwe rasmi katika mfumo wa Walimu. Jiji la Tanga ni kati ya mikoa iliyosahaulika na kuwa na vyuo vichache vya Serikali.