Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza sana viongozi wetu wote, Mheshimiwa John Pombe Magufuli - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu - Makamu wa Rais, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa Waziri Mkuu pamoja na wewe Mheshimiwa Spika wetu na waandamizi wengine wote kwa nafasi zao mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nawaomba sana Watanzania tuungane kwa pamoja kumwomba sana Mwenyezi Mungu aiepushe Tanzania na dunia nzima kwa janga hili la dunia, kwa kweli hakuna mbadala katika janga hili.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali ije na mkakati wa kuboresha kukabiliana na majanga kwa kutazama, kutathimini na athari za tabianchi kwa kutenga fedha, wataalam na vifaa ambavyo kwa matukio ya sasa hali hii ya maafa na majanga haiepukiki.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali kupitia Halmashauri iteue shule moja ya msingi na sekondari zenye mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu ili kupata fursa elimu kwa kuwa kwa sasa kundi hili halina mfumo rasmi katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Spika, mwisho, nawaambia wapinzani kuwa kila Mtanzania ameelewa Serikali ya CCM imefanya nini, kwa hiyo propaganda haina nafasi tena katika Serikali ya awamu ya tano, tukutane Oktoba kitaeleweka.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja asilimia 100.