Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, kuna suala la watu wenye ulemavu na wanawake na vijana ambao bado hawajitambui kuhusu vikundi na asilimia kumi na mikopo ya VICOBA. Mikopo yao hawawezi kurejesha marejesho katika Halmashauri zao, wanajisahau na kupelekea madeni makubwa kwenye mabenki na Halmashauri kukaa na madeni hayo kwa kweli hili lionekane na Serikali, lakini pia naishauri Serikali ifanye juu chini iwafanyie semina au mafunzo kwenye Halmashauri zao ili wajue nini maana ya mikopo na wajue kuwa kuna wenzao wanasubiri pesa ile ya marejesho.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la walemavu huwa hawataki kukaa vikundi kutokana na matatizo yao ya kuwa wako mbali mbali kukutana inakuwa vigumu, kwa hiyo asilimia mbili hii inakuwa haina kazi kubwa katika Halmashauri zao.

Mheshimiwa Spika, vilevile watu wenye ulemavu hawana ushauri kuhusu Corona, bado hawafahamu kitu wapowapo tu. Kwa kweli hili Serikali ilitambue na kuwapatia ufahamu walemvu.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la vijana na kuhusu ajira; vijana wengi hawajui kuhusu ajira, wanakwenda wapi vijana, wanazurura zurura vibaya huko nchini. Serikali ilione hili na ajira zikitoka zinakuwa kidogo, wasaidiwe vijana hao.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la madawa ya kulevya pamoja na jitihada zake bado hili janga la madawa lipo, vijana wanateketea Serikali ichukue jitihada kubwa ili liondoke kabisa.

Mheshimiwa Spika, sasa nimpongeze Rais wangu Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli kwa jitihada zake anazoendelea kuzifanya nchini pamoja na watendaji wake wote wana chapa kazi kweli.

Pia nikushukuru wewe Spika kwa jitihada zako unavyolisimamia Bunge tukufu, kwa kweli wewe ni mfano wa kuigwa. Nimshukuru Waziri Mkuu kwa umahiri wake wa kazi zake anazozifanya kwa kweli yeye ni mfano wa kuigwa pamoja na Mawaziri wenzake wote wanachapa kazi kweli.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuleta maoni yangu niloyaona, ahsante na naomba kuwasilisha.