Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Serikali yetu inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa John Magufuli kwa kazi kubwa sana inayofanya katika kuwaletea wananchi maendeleo na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa CCM kwa kiwango kikubwa.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa usimamizi mzuri wa Wizara hii pamoja na wasaidizi wake. Naipongeza Serikali kwa ujenzi na kuimarisha miundombinu, uboreshaji wa huruma za afya na elimu ikiwemo kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali itenge fedha za kutosha ili kuwezesha kukabiliana na majanga na maafa yanayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Mheshimiwa Spika, mengine nakubaliana na mipango ya Serikali. Nashauri kupunguza kodi kwa vifaa vya kujikinga na maradhi. Ahsante.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.