Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri lakini nitoe maoni juu ya maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, afya; madaktari bado ni changamoto mfano Wilaya ya Handeni ambayo ina madaktari watano tu ikiwa na upungufu wa madaktari 24 na ukizingatia haihudumii Handeni peke yake bali Wilaya jirani kama Kilindi na Manyara.

Mheshimiwa Spika, ukubwa wa Wilaya hii kama sikosei unaweza kuwa inalingana na Mkoa wa Kilimanjaro, hivyo utaona ni kiasi gani watu hawa wanataabika. Hivyo niiombe Serikali itusaidie juu ya tatizo hili ambalo limekua ni la muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, elimu; tatizo la uchache wa madarasa linalopelekea mrundikano wa wanafunzi katika madarasa. Serikali imeleta elimu bure na kuhamasisha wazazi wengi kupeleka watoto hivyo ili lile lengo la awali litimie tunaomba nyongeza ya madarasa na shule ili kupunguza umbali wa kufuata elimu unaopelekea watoto wetu wa kike kukatishwa masomo kutokana na mimba za utotoni.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la maji limekua ni mtihani mkubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Handeni. Kuna mradi ambao umechukua muda mrefu sana wa HTM. Tunaomba kujua tatizo ni nini? Athari za ukosefu wa maji Handeni ni kubwa mno.

Mheshimiwa Spika, viwanda;- tuna uhitaji mkubwa sana wa kiwanda cha matunda. Wale wote wanaopita njia ya Segera - Korogwe na hata kuelekea Tanga Mjini mtaona ni jinsi gani Mkoa wetu umejaaliwa kwa matunda ya kila aina. Lakini cha kusikitisha matunda haya yanatuzidi nguvu, ni mengi kuliko matumizi yanaoza. Hivyo niombe serikali tuangalie juu ya hilo.

Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kuwasilisha.